< Zaburi 14 >

1 Mpumbavu husema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wamepotoka nakufanya uovu haramu; hakuna hata mmoja atendaye dhambi.
For the Leader. A Psalm of David. The fool hath said in his heart: 'There is no God'; they have dealt corruptly, they have done abominably; there is none that doeth good.
2 Yahwe anatazama chini kwa wanadamu kutoka mbinguni aone kama kuna yeyote anayeelewa, amtafutaye Mungu.
The LORD looked forth from heaven upon the children of men, to see if there were any man of understanding, that did seek after God.
3 Wote wamegeukia njia nyingine. Kwa pamoja wamepotoka. Hakuna yeyote atendaye mema, hakuna, hata mmoja.
They are all corrupt, they are together become impure; there is none that doeth good, no, not one.
4 Je, hawajui lolote, wale wafanyao uovu, wale wanao kula watu wangu kama vile wanakula mkate, lakini hao hawamuiti Yahwe?
'Shall not all the workers of iniquity know it, who eat up My people as they eat bread, and call not upon the LORD?'
5 Wao wana tetemeka kwa hofu. Kwa kuwa Mungu yuko pamoja na kusanyiko la wenye haki!
There are they in great fear; for God is with the righteous generation.
6 Ninyi mnataka kumfedhehesha mtu maskini japo kuwa Yahwe ni kimbilio lake.
Ye would put to shame the counsel of the poor, but the LORD is his refuge.
7 Oh, kwamba wokovu wa Israeli ungetokea Sayuni! Wakati Yahwe akiwarudisha watu wake kutoka utumwani, ndipo Yakobo atashangilia na Israeli itakuwa na furaha!
Oh that the salvation of Israel were come out of Zion! When the LORD turneth the captivity of His people, let Jacob rejoice, let Israel be glad.

< Zaburi 14 >