< Zaburi 12 >

1 Msaada, Yahweh, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; nao waaminifu wametokomea.
Help, Adonai; for the godly man ceases. For the faithful fail from among the children of men.
2 Kila mmoja anasema kwa jirani yake maneno matupu; kila mmoja anaongea kwa midomo yenye sifa za uongo na maneno ya udanganyifu.
Everyone lies to his neighbor. They speak with flattering lips, and with a double heart.
3 Yahweh, katilia mbali midomo yenye sifa za uongo, kila ulimi unanena kwa nguvu mambo makubwa.
May Adonai cut off all flattering lips, and the tongue that boasts,
4 Hawa ni wale ambao wamesema, “Kwa ndimi zetu tutashinda. Wakati midomo yetu itakapo ongea, ni nani atakaye kuwa mtawala juu yetu?”
who have said, “With our tongue we will prevail. Our lips are our own. Who is lord over us?”
5 “Kwa sababu ya vurugu zilizopo kinyume na maskini, na kwa sababu ya kuugua kwao wahitaji, Nitainuka,” asema Yahwe. “Nitawaletea usalama wanao hitaji.”
“Because of the oppression of the weak and because of the groaning of the needy, I will now arise,” says Adonai; “I will set him in yesha' ·salvation· far from those who malign him.”
6 Maneno ya Yahwe ni masafi, kama fedha iliyo safishwa katika tanuru duniani, iliyo ng'arishwa mara saba zaidi.
Adonai’s words are flawless words, as silver refined in a clay furnace, purified seven times.
7 Wewe ni Yahwe! Unaye watunza. Una wahifadhi wacha Mungu kutoka katika hiki kizazi cha waovu na hata milele.
You will keep them, Adonai. You will preserve them from this generation forever.
8 Waovu hutembea kila pande pale uovu unapoinuliwa kati ya wanadamu.
The wicked walk on every side, when what is vile is exalted among the sons of men.

< Zaburi 12 >