< Zaburi 11 >

1 Ni kwako Yahweh ninapata usalama; ni kwa namna gani utasema na mimi, “Ruka kama ndege hadi mlimani”?
In Adonai, I take refuge. How can you say to my soul, “Flee as a bird to your mountain!”
2 Tazama! Waovu wana andaa pinde zao. Wana tayarisha gizani mishale yao kwenye kamba ili kufyatua mioyo ya wenye haki.
For, behold, the wicked bend their bows. They set their arrows on the strings, that they may shoot in darkness at the upright in heart.
3 Ikiwa misingi imeharibiwa, mwenye haki atafanya nini?
If the foundations are destroyed, what can the upright do?
4 Yahweh yuko katika hekalu takatifu; macho yake yanatazama, yakiuchunguza ubinadamu.
Adonai is in his holy temple. Adonai is on his throne in heaven. His eyes observe. His eyes examine the children of men.
5 Yahweh huwachunguza wote wenye haki na waovu, bali huwachukia wapendao kuwaumiza wengine.
Adonai examines the upright, but the wicked and him who 'ahav ·affectionately loves· violence his soul hates.
6 Yeye huwanyeshea waovu makaa ya mawe na moto wa jehanamu; upepo uunguzao utakuwa ni sehemu yao kutoka katika kikombe chake!
On the wicked he will rain blazing coals; fire, sulfur, and scorching wind shall be the portion of their cup.
7 Kwa kuwa Yahweh ni mwenye haki, Naye hupenda haki; wenye haki watauona uso wake.
For Adonai is righteous. He 'ahav ·affectionately loves· righteousness. The upright shall see his face.

< Zaburi 11 >