< Zaburi 1 >

1 Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
Blagor možu, ki ne hodi po sovetu krivičnih in ne stopa na grešnikov pot ter ne sedeva v zboru zasmehovalcev;
2 Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
Nego veselje njegovo je v postavi Gospodovi, in postavo njegovo premišljuje noč in dan.
3 Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
Je namreč kakor drevo zasajeno ob vodnih potocih, katero sad svoj rodi o svojem času, in listje njegovo ne odpada: zatorej karkoli bode počel, posrečilo se mu bode.
4 Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Ne tako krivični; nego kakor pleve, katere veter raznaša.
5 Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Zatorej ne ostanejo krivični v óni sodbi; ne grešniki v zboru pravičnih.
6 Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.
Ker Gospod pozna pravičnih pot; pot pa krivičnih izgine.

< Zaburi 1 >