< Mithali 7 >

1 Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
Hijo mío, guarda mis palabras Y atesora mis mandamientos dentro de ti.
2 Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
Guarda mis mandamientos y vive, Y mi enseñanza como la niña de tu ojo.
3 Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
Átalos a tus dedos. Escríbelos en la tabla de tu corazón.
4 Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
Dí a la sabiduría: Tú eres mi hermana. Llama al entendimiento [tu] íntimo amigo,
5 ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
Para que te guarden de la mujer ajena, De la seductora [que] lisonjea con sus palabras.
6 Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
Pues cuando desde la ventana de mi casa Observaba entre las celosías,
7 Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
Vi entre los ingenuos. Observé entre los jóvenes A un joven falto de entendimiento
8 Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
Que pasaba por la calle cerca de la esquina de ella. Caminaba en dirección a la casa de ella
9 Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
Al anochecer, cuando ya oscurecía, En medio de la noche y la oscuridad.
10 Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
Y ahí estaba una mujer que [salía] a encontrarlo, Astuta de corazón, vestida de prostituta,
11 Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
Bullanguera y desenfrenada. Sus pies no pueden permanecer en casa,
12 Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
Unas veces en las calles, otras en las plazas, Acecha en todas las esquinas.
13 Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
Lo agarró y lo besó, Y descaradamente le dijo:
14 leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
Prometí sacrificios de paz. Hoy pagué mis votos.
15 hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
Por tanto salí a encontrarte, A buscar diligentemente tu rostro, y te hallé.
16 Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
Preparé mi cama con colchas. La tendí con lino de Egipto.
17 Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
Perfumé mi cama con mirra, áloes, y canela.
18 Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
Ven, deleitémonos con caricias hasta el alba. Embriaguémonos de amores,
19 Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
Porque mi esposo no está en casa. Emprendió un largo viaje.
20 Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
Llevó consigo una bolsa de dinero. El día de luna nueva volverá a su casa.
21 katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
Lo rindió con la mucha suavidad de sus palabras. Lo sedujo con sus labios lisonjeros.
22 Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
Súbitamente se fue tras ella, Como el buey al matadero, Como un venado que se enredó en la trampa,
23 mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
Como ave que se lanza contra la red, Sin saber que le costará la vida, Hasta que una flecha le traspasa el hígado.
24 Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
Ahora pues, hijos, escúchenme. Presten atención a las palabras de mi boca:
25 Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
No dejes que tu corazón se aparte a los caminos de ella, Ni te extravíes por sus sendas.
26 Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
Porque ella dejó muchos heridos, Y aun los más fuertes fueron asesinados por ella.
27 Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)
Su casa es el camino al Seol, Que desciende a las cámaras de la muerte. (Sheol h7585)

< Mithali 7 >