< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
La sabiduría edificó su casa. Labró sus siete columnas.
2 Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
Degolló sus animales, Mezcló su vino, Sirvió su mesa,
3 Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
Y envió a sus criadas A pregonarlo desde las más altas cumbres de la ciudad:
4 “Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
¡El que sea simple, venga acá! Al falto de entendimiento le quiero hablar:
5 Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
¡Vengan, coman de mis manjares, Y beban del vino que mezclé!
6 Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
¡Dejen la necedad y vivan, Pongan sus pies en el camino del entendimiento!
7 Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
El que corrige al burlador se acarrea insultos. El que reprende al perverso se acarrea afrenta.
8 Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
No reprendas al burlador, no sea que te aborrezca. Reprende al sabio, y te amará.
9 Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
Da al sabio, y será aun más sabio. Enseña al justo, y aumentará su saber.
10 Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
El temor a Yavé es el principio de la sabiduría, Y el conocimiento del Santísimo es el entendimiento.
11 Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
Porque por mí se aumentarán tus días, Y años de vida se te añadirán.
12 Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
Si eres sabio, para ti mismo eres sabio, Y si eres burlador, solo tú llevarás el daño.
13 Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
La mujer necia es alborotadora. Es simple y nada sabe.
14 Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
Se sienta en la puerta de su casa, O en los lugares más altos de la ciudad
15 Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
Para llamar a los que pasan, A los que van directo por sus sendas:
16 Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
¡Todos los ingenuos vengan acá! Y dice a los faltos de cordura:
17 Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
¡El agua robada es dulce! ¡El pan comido en oculto es sabroso!
18 Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)
No saben ellos que allí están los muertos, Y que sus invitados están tendidos en lo profundo del Seol. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >