< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
Hijo mío, si saliste fiador por tu prójimo, Si empeñaste tu palabra a un extraño,
2 basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
Si te enredaste con tus palabras, Y quedaste atrapado con los dichos de tu boca,
3 Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
Haz esto ahora, hijo mío, y líbrate. Ya que caíste en las manos de tu prójimo: Vé, humíllate e importuna a tu prójimo.
4 Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
No concedas sueño a tus ojos, Ni adormecimiento a tus párpados.
5 Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
Líbrate como gacela de la mano [del cazador], Como un ave de la trampa.
6 Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
Mira a la hormiga, oh perezoso, Observa sus caminos y sé sabio,
7 Hana akida, afisa au mtawala,
La cual, sin tener jefe, Ni gobernador, ni soberano,
8 lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
Prepara en el verano su comida. En el tiempo de la cosecha guarda su sustento.
9 Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
¿Hasta cuándo estarás acostado, oh perezoso? ¿Cuándo te levantarás de tu sueño?
10 Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
Un rato duermes, otro dormitas, Un rato cruzas los brazos y descansas.
11 ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
Te llega la miseria como un vagabundo, Y tu necesidad como un hombre armado.
12 Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
Hombre depravado es el hombre inicuo, Que anda en la perversidad de su boca,
13 akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
Guiña con un ojo, menea los pies, Hace señas con los dedos.
14 Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
En su corazón hay perversidades, Maquina maldades, y continuamente busca rencillas.
15 Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
Por tanto, su calamidad vendrá de repente. Súbitamente será quebrantado y no habrá remedio.
16 Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
Seis [cosas] aborrece Yavé, Y aun siete repugna su alma:
17 Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
Ojos altivos, boca mentirosa, Manos que derraman sangre inocente,
18 moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
Corazón que maquina planes perversos, Pies presurosos para correr al mal,
19 shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
Testigo falso que habla mentiras, Y el que enciende discordias entre sus hermanos.
20 Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Hijo mío, guarda el mandamiento de tu padre, Y no abandones la instrucción de tu madre.
21 Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
Átalos continuamente a tu corazón, Enlázalos en torno a tu cuello.
22 utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
Cuando camines, te guiarán. Cuando duermas, te protegerán. Hablarán contigo al despertar.
23 Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
Porque el mandamiento es lámpara, La enseñanza es luz Y camino de vida las reprensiones de la instrucción.
24 Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
Te guardarán de la mala mujer, De la blandura de la boca de la mujer extraña.
25 Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
No codicies en tu corazón su hermosura, Ni dejes que te cautive con sus párpados.
26 Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
Porque si la prostituta busca una hogaza de pan, La adúltera caza una vida preciosa.
27 Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
¿Tomará el hombre fuego en su seno, Sin que ardan sus ropas?
28 Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
¿Andará un hombre sobre brasas, Sin que se quemen sus pies?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
Así sucederá con el que se une a la mujer de su prójimo. Ninguno que la toque quedará impune.
30 Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
¿No desprecian al ladrón aunque robe Para llenar su estómago cuando tiene hambre?
31 Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
Si es sorprendido, tiene que pagar siete veces Y entregar todo lo que tiene en su casa.
32 Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
Pues el adúltero es hombre sin cordura, Destructor de sí mismo es el que lo hace.
33 Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
Heridas y deshonra hallará, Y su afrenta no será borrada.
34 Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
Porque los celos son la ira del hombre. En el día de la venganza no perdonará,
35 Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.
Ni aceptará algún rescate. No se aplacará aunque ofrezcas muchos regalos.

< Mithali 6 >