< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
No conviene la nieve en el verano Ni la lluvia en la cosecha, Ni la honra al necio.
2 Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
Como pájaro que aletea y golondrina que vuela, Así la maldición sin causa no se cumple.
3 Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
El látigo para el caballo, el cabestro para el asno Y la vara para la espalda del necio.
4 Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
No respondas al necio según su necedad, Para que no seas tú como él.
5 Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
Responde al necio como merece su necedad, Para que él no se estime sabio.
6 Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
El que envía mensaje por medio de un necio Corta sus pies y bebe violencia.
7 Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
Al lisiado le cuelgan las piernas inútiles. Así es el proverbio en la boca del necio.
8 Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
Como sujetar una piedra en la honda, Así es el que da honores al necio.
9 Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
Como espina que cae en la mano de un borracho, Así es el proverbio en boca de los necios.
10 Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
Como arquero que dispara contra cualquiera, Es el que contrata a insensatos y vagabundos.
11 Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
Como perro que vuelve a su vómito, Así el necio repite su insensatez.
12 Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
¿Has visto a alguien sabio en su propia opinión? Más se puede esperar de un necio que de él.
13 Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
Dice el perezoso: El león está en el camino, Hay un león en la plaza.
14 Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
Como la puerta gira sobre sus bisagras, Así también el perezoso en su cama.
15 Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
El perezoso mete su mano en el plato, Y le repugna aun llevar la comida a su boca.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
El perezoso se cree más sabio Que siete hombres que responden con discreción.
17 Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
El que se mete en pleito ajeno Es como el que agarra un perro por las orejas.
18 Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
Como el loco furioso que lanza dardos encendidos y flechas mortales,
19 ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
Así es el que engaña a su prójimo Y luego dice: Solo era una broma.
20 Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
Sin leña se apaga el fuego, Y donde no hay chismoso, cesa la contienda.
21 Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
El carbón para las brasas y la leña para el fuego, Y el pendenciero para encender la contienda.
22 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
Las palabras del chismoso son manjares, Que bajan hasta lo más recóndito del ser.
23 Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
Como escoria de plata echada sobre un tiesto Son los labios enardecidos y el corazón perverso.
24 Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
Disimula con sus labios el que odia, Pero en su interior trama el engaño.
25 Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
Aunque hable amigablemente, no le creas, Porque siete repugnancias hay en su corazón.
26 Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
Aunque con disimulo encubra su odio, Su perversidad será descubierta en la congregación.
27 Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
El que cave una fosa, caerá en ella, Y al que ruede una piedra, le caerá encima.
28 Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.
La lengua mentirosa odia a los que aflige, Y la boca lisonjera causa ruina.

< Mithali 26 >