< Mithali 23 >

1 Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
Cuando te sientes a comer con un ʼadón, Considera bien lo que está delante de ti,
2 na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
Y pon cuchillo a tu garganta Si tienes gran apetito.
3 Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
No codicies sus manjares delicados, Porque son pan de engaño.
4 Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
No te afanes por hacer riquezas. Sé prudente y desiste.
5 Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
Si les diriges una mirada, ya no están. Les salieron alas como un águila que vuela a los cielos.
6 Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
No comas pan con el avaro, Ni codicies sus manjares,
7 maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
Porque como piensa en su corazón, así es. Come y bebe, te dirá, Pero su corazón no está contigo.
8 Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
Vomitarás el bocado que comiste Y perderás tus suaves palabras.
9 Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
No hables a oídos del insensato, Porque despreciará la prudencia de tus razones.
10 Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
No cambies de lugar el lindero antiguo, Ni entres en el campo de los huérfanos,
11 maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
Porque su Redentor es fuerte, Y defenderá contra ti la causa de ellos.
12 Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
Aplica tu corazón a la enseñanza, Y tus oídos a las palabras sabias.
13 Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
No retraigas la corrección al muchacho, Si lo castigas con vara, no morirá.
14 Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol h7585)
Lo castigarás con vara, Y librarás su alma del Seol. (Sheol h7585)
15 Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
Hijo mío, si tu corazón es sabio, También a mí se me alegrará el corazón,
16 sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
Mi ser interno también se alegrará Cuando tus labios hablen cosas rectas.
17 Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
No tenga tu corazón envidia de los pecadores. Más bien, persevera en el temor a Yavé en todo tiempo.
18 Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
Porque ciertamente hay un porvenir, Y tu esperanza no será frustrada.
19 Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
Escucha tú, hijo mío, sé sabio, Y dirige tu corazón por el buen camino.
20 Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
No estés con los bebedores de vino, Ni con los comedores de carne,
21 maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
Porque el ebrio y el glotón empobrecerán, Y el dormitar hará vestir harapos.
22 Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
Escucha a tu padre que te engendró, Y no desprecies a tu madre cuando sea anciana.
23 Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
Adquiere la verdad y no la vendas, También sabiduría, instrucción y entendimiento.
24 Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
El padre del justo se alegrará en gran manera. El que engendra un hijo sabio se gozará con él.
25 Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
Alégrense tu padre y tu madre, Y regocíjese la que te dio a luz.
26 Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
Dame, hijo mío, tu corazón Y observen tus ojos mis caminos.
27 Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
Porque fosa profunda es la prostituta, Y pozo angosto la mujer extraña.
28 Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
También ella, como asaltante, acecha, Y entre los hombres multiplica a los traicioneros.
29 Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
¿Para quién es el ay? ¿Para quién las tristezas? ¿Para quién las contiendas? ¿Para quién el quejido? ¿Para quién las heridas sin causa? ¿Para quién los ojos enrojecidos?
30 Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
Para el que se detiene en el vino, Para los que prueban licores mezclados.
31 Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
No mires al vino cuando rojea, Y lanza destellos en la copa, Porque se entra suavemente,
32 Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
Pero al fin, muerde como una serpiente. Pica como una víbora.
33 Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
Tus ojos mirarán cosas extrañas, Y tu corazón hablará cosas perversas.
34 Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
Serás como el que está acostado en alta mar, Como el que duerme en el palo de un velero,
35 Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”
Y dirás: Me golpearon y no me dolió, Me azotaron, pero no lo sentí. Cuando despierte, lo volveré a buscar.

< Mithali 23 >