< Yoshua 14 >

1 Maeneo haya ya nchi ambayo watu wa Israeli waliyapokea kama urithi wao katika nchi ya Kanaani. Urith huu uligawanywa kwao na Eliazeri kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya mababu wa familia zao kati ya watu wa Israeli.
And these are the inheritances which the children of Israel took in the land of Canaan, which Eleazar the priest, and Joshua the son of Nun, and the heads of the fathers' houses of the tribes of the children of Israel, distributed unto them,
2 Urithi wao ulichaguliwa kwa kupiga kura kwa makabila tisa na nusu, kama vile Yahweh alivyoagiza kwa mkono wa Musa.
by the lot of their inheritance, as the LORD commanded by the hand of Moses, for the nine tribes, and for the half-tribe. —
3 Kwa kuwa Musa alikuwa amewapa urithi makabila mawili na nusu ng'ambo ya Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi wowote.
For Moses had given the inheritance of the two tribes and the half-tribe beyond the Jordan; but unto the Levites he gave no inheritance among them.
4 Kabila la Yusufu kwa uhalisia yalikuwa makabila mawili, Manase na Efraimu. Na hakuna sehemu yoyote ya urithi waliyopewa Walawi katika nchi, lakini walipewa miji ya kuishi ndani yake pamoja na sehemu ya malisho ya mifugo yao na kwa ajili ya riziki zao.
For the children of Joseph were two tribes, Manasseh and Ephraim; and they gave no portion unto the Levites in the land, save cities to dwell in, with the open land about them for their cattle and for their substance. —
5 Watu wa Israeli walifanya hivyo kama vile Yahweh alivyomwagiza Musa, basi waliiganywa nchi.
As the LORD commanded Moses, so the children of Israel did, and they divided the land.
6 Kisha kabila la Yuda lilikuja kwa Yoshua huko Giligali. Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi, akamwambia,”Unajua kile Yahweh alichomwambia Musa mtu wa Mungu juu yako na mimi huko Barnea.
Then the children of Judah drew nigh unto Joshua in Gilgal; and Caleb the son of Jephunneh the Kenizzite said unto him: 'Thou knowest the thing that the LORD spoke unto Moses the man of God concerning me and concerning thee in Kadesh-barnea.
7 Nilikuwa na umri wa miaka arobani wakati Musa mtumishi wa Yahweh aliponituma kutoka Kadeshi Barnea kuipeleleza nchi. Nilimletea taarifa tena kama nilivyotakiwa kufanya katika moyo wangu.
Forty years old was I when Moses the servant of the LORD sent me from Kadesh-barnea to spy out the land; and I brought him back word as it was in my heart.
8 Lakini ndugu zangu walioenda pamoja nami waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa woga. Lakini mimi nilimfuata Yahweh kabisa.
Nevertheless my brethren that went up with me made the heart of the people melt; but I wholly followed the LORD my God.
9 Musa aliapa katika siku hiyo akisema, “Hakika nchi ambayo miguu yako imetembea juu yake itakuwa urithi wako na kwa watoto wako milele, kwasababu umemfuata kabisa Yahweh Mungu wangu.
And Moses swore on that day, saying: Surely the land whereon thy foot hath trodden shall be an inheritance to thee and to thy children for ever, because thou hast wholly followed the LORD my God.
10 Tazama! sasa, Yahweh amenihifadhi hai kwa miaka hii arobaini na tano, kama alivyosema - tangu kipindi kile Yahweh alivyomwambia Musa neno hili, wakati huo Waisraeli walikuwa wakitembea jangwani. Tazama! sasa katika siku hii ya leo nina miaka themanini na mitano.
And now, behold, the LORD hath kept me alive, as He spoke, these forty and five years, from the time that the LORD spoke this word unto Moses, while Israel walked in the wilderness; and now, lo, I am this day fourscore and five years old.
11 Bado hata siku hii ya leo nina nguvu kama nilivyokuwa katika siku ile ambayo Musa alinituma. Nguvu zangu za sasa ni sawa na nguvu zangu za kipindi kile, kwa ajili ya vita na kwa kwenda na kwa kuja.
As yet I am as strong this day as I was in the day that Moses sent me; as my strength was then, even so is my strength now, for war, and to go out and to come in.
12 Sasa basi, nipe nchi hii ya milima, ambayo Yahweh aliniahidi katika siku hiyo. Kwa kuwa ulisikia katika siku hiyo kuwa Wanakimu walikuwa huko katika miji yenye ngome. Itakuwa kwamba Yahweh atakuwa pamoja nami na ya kwamba nitawafukuzia mbali, kama vile Yahweh alivyosema.”
Now therefore give me this mountain, whereof the LORD spoke in that day; for thou heardest in that day how the Anakim were there, and cities great and fortified; it may be that the LORD will be with me, and I shall drive them out, as the LORD spoke.'
13 Kisha Yoshua alimbariki Kalebu mwana wa Yefune na alimpa Hebroni kama urithi wake.
And Joshua blessed him; and he gave Hebron unto Caleb the son of Jephunneh for an inheritance.
14 Hivyo Hebroni ikawa urithi wa Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi hata leo, kwasababu alimfuata kabisa Yahweh, Mungu wa Israeli.
Therefore Hebron became the inheritance of Caleb the son of Jephunneh the Kenizzite, unto this day; because that he wholly followed the LORD, the God of Israel.
15 Basi, jina la Hebroni hapo mwanzo lilikuwa ni Kiriathi Arba ( Arba ambaye alikuwa ni mtu mkuu miongoni mwa Wanakim). Kisha nchi ikawa na raha bila vita.
Now the name of Hebron beforetime was Kiriath-arba, which Arba was the greatest man among the Anakim. And the land had rest from war.

< Yoshua 14 >