< Waamuzi 8 >

1 Watu wa Efraimu wakamwambia Gideoni, “Ni nini hiki umetutenda? Haukuita wakati ulipokwenda kupigana na Midiani.” Wakamwambia kwa nguvu.
And the men of Ephraim said unto him: 'Why hast thou served us thus, that thou didst not call us when thou wentest to fight with Midian?' And they did chide with him sharply.
2 Akawaambia, “Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi? Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?
And he said unto them: 'What have I now done in comparison with you? Is not the gleaning of Ephraim better than the vintage of Abiezer?
3 Mungu amewapa ushindi juu ya wakuu wa Midiani-Orebu na Zeeb! Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?” Hasira yao ikashuka chini aliposema hili.
God hath delivered into your hand the princes of Midian, Oreb and Zeeb; and what was I able to do in comparison with you?' Then their anger was abated toward him, when he had said that.
4 Gideoni alikuja Yordani na akavuka juu yake, yeye na watu mia tatu waliokuwa pamoja naye. Walikuwa wamechoka, lakini bado waliendelea kufuatilia.
And Gideon came to the Jordan, and passed over, he, and the three hundred men that were with him, faint, yet pursuing.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali wape mikate kwa watu wanaonifuata, kwa kuwa wamechoka, nami niwafuatilia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.
And he said unto the men of Succoth: 'Give, I pray you, loaves of bread unto the people that follow me; for they are faint, and I am pursuing after Zebah and Zalmunna, the kings of Midian.'
6 Na wakuu wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako? Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?”
And the princes of Succoth said: 'Are the hands of Zebah and Zalmunna now in thy power, that we should give bread unto thine army?'
7 Gideoni akasema, “Bwana akitupa ushindi juu ya Zeba na Salmunna, nitainyunyiza ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.
And Gideon said: 'Therefore when the LORD hath delivered Zebah and Zalmunna into my hand, then I will tear your flesh with the thorns of the wilderness and with briers.'
8 Akatoka huko, akaenda Penieli, akawaambia watu maneno hayo hayo; lakini watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyojibu.
And he went up thence to Penuel, and spoke unto them in like manner; and the men of Penuel answered him as the men of Succoth had answered.
9 Akawaambia pia watu wa Penieli, akasema, “Nitakapokuja kwa amani, nitauangusha mnara huu.”
And he spoke also unto the men of Penuel, saying: 'When I come back in peace, I will break down this tower.'
10 Sasa Zeba na Salmuna walikuwa huko Karkori pamoja na jeshi lao, karibu na watu elfu kumi na tano, wote waliosalia nje ya jeshi lote la watu wa Mashariki, kwa kuwa walianguka watu 120, 000 waliofundishwa kupigana na upanga.
Now Zebah and Zalmunna were in Karkor, and their hosts with them, about fifteen thousand men, all that were left of all the host of the children of the east; for there fell a hundred and twenty thousand men that drew sword.
11 Gideoni akapanda barabara iliyochukuliwa na wakaazi wa hema, Noba na Yogbena. Akalishinda jeshi la adui, kwa sababu hawakuwa wanatarajia shambulio.
And Gideon went up by the way of them that dwelt in tents on the east of Nobah and Jogbehah, and smote the host; for the host was secure.
12 Zeba na Salmuna walikimbia, na Gideoni alipowafuata, akawatwaa wafalme wawili wa Midiani-Zeba na Salmunna- na kulifanya jeshi lote kuwa na hofu.
And Zebah and Zalmunna fled; and he pursued after them; and he took the two kings of Midian, Zebah and Zalmunna, and discomfited all the host.
13 Gideoni, mwana wa Yoashi, alirudi kutoka kwenye vita kwenda kupitia Heresi.
And Gideon the son of Joash returned from the battle from the ascent of Heres.
14 Akamkimbilia kijana mmoja wa watu wa Sukothi na kutafuta ushauri kutoka kwake. Kijana huyo alimwelezea viongozi wa Sukothi na wazee wake, watu sabini na saba.
And he caught a young man of the men of Succoth, and inquired of him; and he wrote down for him the princes of Succoth, and the elders thereof, seventy and seven men.
15 Gideoni akaja kwa watu wa Sukothi, akasema, “Tazameni Zeba na Salmuna, ambao mlinidhihaki kwa ajili yao, nikasema, 'Je! mmemshinda Zeba na Salmuna? Hatujui kwamba tunapaswa kulipa jeshi lako mkate.”
And he came unto the men of Succoth, and said: 'Behold Zebah and Zalmunna, concerning whom ye did taunt me, saying: Are the hands of Zebah and Zalmunna now in thy power, that we should give bread unto thy men that are weary?'
16 Gideoni akawachukua wazee wa mji, naye akawaadhibu watu wa Sukothi pamoja na miiba ya jangwa na michongoma.
And he took the elders of the city, and thorns of the wilderness and briers, and with them he taught the men of Succoth.
17 Akaangusha mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji huo.
And he broke down the tower of Penuel, and slew the men of the city.
18 Gideoni akamwambia Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliwauawa Tabori?” Wakajibu, “Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa. Kila mmoja wao alionekana kama mwana wa mfalme.”
Then said he unto Zebah and Zalmunna: 'Where are the men whom ye slew at Tabor?' And they answered: 'As thou art, so were they; of one form with the children of a king.'
19 Gideoni akasema, 'Wao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Bwana anaishivyo, kama mngewaacha hai, nisingewauwa.”
And he said: 'They were my brethren, the sons of my mother; as the LORD liveth, if ye had saved them alive, I would not slay you.'
20 Akamwambia Yetheri (mzaliwa wake wa kwanza), “Simama uwaue!” Lakini kijana huyo hakutoa upanga wake kwa kuwa aliogopa, kwa sababu alikuwa bado kijana mdogo.
And he said unto Jether his first-born: 'Up, and slay them.' But the youth drew not his sword; for he feared, because he was yet a youth.
21 Ndipo Zeba na Salmuna wakasema, simama mwenyewe, utuue! Kwa maana kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake. Gideoni akasimama na kumwua Zeba na Salmuna. Pia aliondoa mapambo yaliyokuwa juu ya shingo za ngamia zao.
Then Zebah and Zalmunna said: 'Rise thou, and fall upon us; for as the man is, so is his strength.' And Gideon arose, and slew Zebah and Zalmunna, and took the crescents that were on their camels' necks.
22 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mtoto wako, na mjukuu wako; kwa sababu umetuokoa mikononi mwa Midiani.”
Then the men of Israel said unto Gideon: 'Rule thou over us, both thou, and thy son, and thy son's son also; for thou hast saved us out of the hand of Midian.'
23 Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala mtoto wangu hatatawala juu yenu. Bwana atatawala juu yenu.”
And Gideon said unto them: 'I will not rule over you, neither shall my son rule over you; the LORD shall rule over you.'
24 Gideoni akawaambia, “Nina haja yangu niitakayo kwenu kwamba kila mmoja wenu atanipe pete kutoka kwenye nyara zake.” (Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)
And Gideon said unto them: 'I would make a request of you, that ye would give me every man the ear-rings of his spoil.' — For they had golden ear-rings, because they were Ishmaelites.
25 Wakamjibu, “Tunafurahi kukupa.” Wakatandika vazi na kila mtu akatupa pete kutoka kwenye nyara zake.
And they answered: 'We will willingly give them.' And they spread a garment, and did cast therein every man the ear-rings of his spoil.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilikuwa shekeli 1, 700 za dhahabu. Nyara hizi zilikuwa ni pamoja na mapambo ya makoja, vidani, nguo ya rangi ya zambarau waliyovaa na wafalme wa Midiani, na zaidi ya minyororo iliyokuwa karibu na shingo za ngamia zao.
And the weight of the golden ear-rings that he requested was a thousand and seven hundred shekels of gold; beside the crescents, and the pendants, and the purple raiment that was on the kings of Midian, and beside the chains that were about their camels' necks.
27 Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete na kuiweka katika mji wake, huko Ofra, na Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu. Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.
And Gideon made an ephod thereof, and put it in his city, even in Ophrah; and all Israel went astray after it there; and it became a snare unto Gideon, and to his house.
28 Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli na hawakuinua vichwa vyao tena. Na nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini siku za Gideoni.
So Midian was subdued before the children of Israel, and they lifted up their heads no more. And the land had rest forty years in the days of Gideon.
29 Yerubaali, mwana wa Yoashi, akaenda akakaa nyumbani kwake.
And Jerubbaal the son of Joash went and dwelt in his own house.
30 Gideoni alikuwa na wana sabini, waliokuwa uzao wake, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
And Gideon had threescore and ten sons of his body begotten; for he had many wives.
31 Mwanamke wake, aliyekuwa Shekemu, akamzaa pia mwana, na Gideoni akampa jina lake Abimeleki.
And his concubine that was in Shechem, she also bore him a son, and he called his name Abimelech.
32 Gideoni, mwana wa Yoashi, akafa katika uzee mzuri, akazikwa huko Ofra katika kaburi la baba yake Joashi, wa jamaa ya Abiyezeri.
And Gideon the son of Joash died in a good old age, and was buried in the sepulchre of Joash his father, in Ophrah of the Abiezrites.
33 Ikawa, Gideoni alipokufa, watu wa Israeli wakageuka tena na kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali. Wamlifanya Baali Berith kuwa mungu wao.
And it came to pass, as soon as Gideon was dead, that the children of Israel again went astray after the Baalim, and made Baal-berith their god.
34 Watu wa Israeli hawakukumbuka kumtukuza Bwana, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka kwa mikono ya adui zao kila upande.
And the children of Israel remembered not the LORD their God, who had delivered them out of the hand of all their enemies on every side;
35 Hawakuweka ahadi zao kwa nyumba ya Yerubaali (yaani Gidioni), kwa ajili ya mema yote aliyoyafanya katika Israeli.
neither showed they kindness to the house of Jerubbaal, namely Gideon, according to all the goodness which he had shown unto Israel.

< Waamuzi 8 >