< Yoshua 13 >

1 Sasa Yoshua alikuwa mzee wakati Yahweh alipomwambia, “Umekuwa mzee, lakini bado kuna nchi kubwa ya kuteka.
Now Joshua was old and well stricken in years; and the LORD said unto him: 'Thou art old and well stricken in years, and there remaineth yet very much land to be possessed.
2 Nchi iliyosalia ndio hii: mikoa yote ya Wafilisti, na mikoa ile ya Wageshuri,
This is the land that yet remaineth: all the regions of the Philistines, and all the Geshurites;
3 (tangu Shihori, iliyoko mashariki mwa Misri, na upande wa kaskazini kuelekea mpaka wa Ekroni, inayofikiriwa kuwa ni mali ya Wakanaani; wafalme watano wa Wafilisti, wale wafalme wa Gaza, Ashidodi, Ashikeloni, Gathi na Ekroni - miliki ya Waavi.
from the Shihor, which is before Egypt, even unto the border of Ekron northward — which is counted to the Canaanites; the five lords of the Philistines: the Gazite, and the Ashdodite, the Ashkelonite, the Gittite, and the Ekronite; also the Avvim
4 Katika upande wa kusini, kulisalia nchi yote ya Wakanaani, na Meara ambayo ni miliki ya Wasidoni, hadi Afeki, hata mpaka wa Waamori;
on the south; all the land of the Canaanites, and Mearah that belongeth to the Zidonians, unto Aphek, to the border of the Amorites;
5 nchi ya Wagebali, Lebanoni kuelekea upande wa mapambazuko ya jua, kutoka Baali- Gadi chini ya Mlima Hermoni mpaka Lebo Hamathi.
and the land of the Gebalites, and all Lebanon, toward the sunrising, from Baal-gad under mount Hermon unto the entrance of Hamath;
6 Pia, wenyeji wote wa nchi ya milima kutoka Lebanoni hadi Misrefothi - Maimu, pamoja na watu wa Sidoni. Nitawafukuza mbele ya jeshi la Israeli. Uwe na uhakika wa kuwapa Waisraeli nchi kama urithi, kama nilivyokuagiza.
all the inhabitants of the hill-country from Lebanon unto Misrephoth-maim, even all the Zidonians; them will I drive out from before the children of Israel; only allot thou it unto Israel for an inheritance, as I have commanded thee.
7 Igawanye nchi hii kama urithi kwa makabila tisa na kwa nusu ya kabila la Manase.
Now therefore divide this land for an inheritance unto the nine tribes, and the half-tribe of Manasseh.'
8 Pamoja na nusu nyingine ya kabila la Manase, Wareubeni na Wagadi wamekwisha kupokea urithi wao ambao Musa aliwapa katika upande wa mashariki wa Yordani,
With him the Reubenites and the Gadites received their inheritance, which Moses gave them, beyond the Jordan eastward, even as Moses the servant of the LORD gave them;
9 kutoka Aroeri, iliyo katika ukingo wa bonde la mto Arnoni (kujumuisha na mji ambao uko katikati ya bonde), kwa nyanda zote za Medeba hadi Diboni;
from Aroer, that is on the edge of the valley of Arnon, and the city that is in the middle of the valley, and all the table-land from Medeba unto Dibon;
10 miji yote ya Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala katika Heshiboni, hata mpaka wa Waamori,
and all the cities of Sihon king of the Amorites, who reigned in Heshbon, unto the border of the children of Ammon;
11 Gileadi na mkoa wa Wageshuri na Maakathi, mlima wote wa Hermoni, Bashani yote mpaka Saleka;
and Gilead, and the border of the Geshurites and Maacathites, and all mount Hermon, and all Bashan unto Salcah;
12 ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyetawala katika Ashitarothi na Edrei - hawa ni wale waliosalia katika Refaimu - ambao Musa aliwapiga na kuwafukuzia mbali.
all the kingdom of Og in Bashan, who reigned in Ashtaroth and in Edrei — the same was left of the remnant of the Rephaim — for these did Moses smite, and drove them out.
13 Lakini watu wa Israeli hawakuwafukuza Wageshuri wala Wamakathi. Badala yake, Wageshuri na Wamakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli hadi leo.
Nevertheless the children of Israel drove not out the Geshurites, nor the Maacathites; but Geshur and Maacath dwelt in the midst of Israel unto this day.
14 Kabila la Lawi pekee halikupewa urithi na Musa. Urithi wao ni sadaka za Yahweh, Mungu wa Israeli, zilizotolewa kwa moto, kama Mungu alivyomwagiza Musa.
Only unto the tribe of Levi he gave no inheritance; the offerings of the LORD, the God of Israel, made by fire are his inheritance, as He spoke unto him.
15 Musa aliwapa urithi kabila la Rubeni, ukoo kwa ukoo.
And Moses gave unto the tribe of the children of Reuben according to their families.
16 Miliki yao ilikuwa kutoka Aroeri, juu ya ukingo wa bonde la Mto Arnoni, na mji ulio katikati ya bonde, na nyanda zote za Medeba.
And their border was from Aroer, that is on the edge of the valley of Arnon, and the city that is in the middle of the valley, and all the table-land by Medeba;
17 Wareubeni walipata pia Heshiboni, na miji yake yote zilizo katika uwanda, Diboni, na Bamathi Baali, na Bethi Baalimeoni,
Heshbon, and all her cities that are in the table-land; Dibon, and Bamoth-baal, and Beth-baal-meon;
18 na Yahazi, na Kedemothi, na Mefaathi,
and Jahaz, and Kedemoth, and Mephaath;
19 na Kiriathaimu, na Sibuma, na Zerethishahari juu ya kilima cha bonde.
and Kiriathaim, and Sibmah, and Zerethshahar in the mount of the valley;
20 Wareubeni walipata pia Bethi Peori, miteremko ya Pisiga, Bethi Yeshimothi,
and Beth-peor, and the slopes of Pisgah, and Beth-jeshimoth;
21 miji yote ya uwanda, na ufalme wote wa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa ametawala katika Heshiboni, ambaye Musa alikuwa amemshinda pamoja na viongozi wa Midiani, Evi, Rekemu, Zuri, Huri na Reba, wana wa mfalme wa Sihoni, ambao walikuwa wameishi katika nchi.
and all the cities of the table-land, and all the kingdom of Sihon king of the Amorites, who reigned in Heshbon, whom Moses smote with the chiefs of Midian, Evi, and Rekem, and Zur, and Hur, and Reba, the princes of Sihon, that dwelt in the land.
22 Pia, watu wa Israeli walimwua kwa upanga Baalam mwana wa Beori, ambaye alifanya mambo ya uaguzi, miongoni mwa wale waliowaua.
Balaam also the son of Beor, the soothsayer, did the children of Israel slay with the sword among the rest of their slain.
23 Mpaka wa kabila la Rubeni ni Mto Yordani; huu ndio mpaka wao. Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Rubeni, uliotolewa kwa kila ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
And as for the border of the children of Reuben, the Jordan was their border. This was the inheritance of the children of Reuben according to their families, the cities and the villages thereof.
24 Hiki ndicho Musa alilipa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
And Moses gave unto the tribe of Gad, unto the children of Gad, according to their families.
25 Himaya yao ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni, hadi Aroeri, iliyo mashariki mwa Raba,
And their border was Jazer, and all the cities of Gilead, and half the land of the children of Ammon, unto Aroer that is before Rabbah;
26 kutoka Heshiboni hadi Ramathi - Mizipe na Betonimu, kutoka Mahanaimu mpaka himaya ya Debiri.
and from Heshbon unto Ramath-mizpeh, and Betonim; and from Mahanaim unto the border of Lidbir;
27 Katika bonde, Musa aliwapa Bethi -Haramu, Bethi - Nimra, Sukothi, na Zafoni, ufalme uliobakia wa Sihoni mfalme wa Heshiboni, pamoja na Yordani kama mpaka, katika sehemu za chini za mwisho wa Bahari ya Kinerethi, upande wa mashariki ng'ambo ya Yordani.
and in the valley, Beth-haram, and Beth-nimrah, and Succoth, and Zaphon, the rest of the kingdom of Sihon king of Heshbon, the Jordan being the border thereof, unto the uttermost part of the sea of Chinnereth beyond the Jordan eastward.
28 Huu ni urithi wa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
This is the inheritance of the children of Gad according to their families, the cities and the villages thereof.
29 Musa aliwapa urithi nusu ya kabila la Manase. Urithi uligawiwa kwa nusu ya kabila la watu wa Manase kutokana na kabila zao.
And Moses gave inheritance unto the half-tribe of Manasseh; and it was for the half-tribe of the children of Manasseh according to their families.
30 Miliki yao ilikuwa kutoka Mahanaimu, Bashani yote, ufalme wote wa mfalme Ogu wa Bashani, na miji yote ya Yairi, iliyo katika Bashani, miji sitini;
And their border was from Mahanaim, all Bashan, all the kingdom of Og king of Bashan, and all the villages of Jair, which are in Bashan, threescore cities;
31 nusu ya Gileadi, na Ashitarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Miji hii iligawanywa kwa ukoo wa Makiri mwana wa Manase -nusu ya watu wa Makiri, walipewa kwa kila familia zao.
and half Gilead, and Ashtaroth, and Edrei, the cities of the kingdom of Og in Bashan, were for the children of Machir the son of Manasseh, even for the half of the children of Machir according to their families.
32 Huu ndio urithi ambao Musa aliowagawia katika nyanda za Moabu, ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
These are the inheritances which Moses distributed in the plains of Moab, beyond the Jordan at Jericho, eastward.
33 Musa hakulipa urithi kabila la Lawi. kwa kuwa Yahweh, Mungu wa israeli, ni urithi wao, kama vile alivyowaambia.
But unto the tribe of Levi Moses gave no inheritance; the LORD, the God of Israel, is their inheritance, as He spoke unto them.

< Yoshua 13 >