< Yona 4 >

1 Lakini hili lilimchukiza Yona naye akakasirika.
But it displeased Jonah exceedingly, and he was angry.
2 Basi Yona akamwomba Bwana akasema, “Ee, Bwana, hiya sio yale niliyosema wakati niliporudi katika nchi yangu? Ndiyo maana nilifanya haraka na kujaribu kukimbia Tarshishi-kwa sababu nilijua kuwa wewe ni Mungu mwenye neema, mwenye huruma, si meingi wa hasira, mwingi kwa uaminifu, na hughairi maafa.
And he prayed unto the LORD, and said: 'I pray Thee, O LORD, was not this my saying, when I was yet in mine own country? Therefore I fled beforehand unto Tarshish; for I knew that Thou art a gracious God, and compassionate, long-suffering, and abundant in mercy, and repentest Thee of the evil.
3 Kwa hiyo sasa, Bwana, nakuomba, uniondoe uhai wangu, kwa maana ni bora kwangu kufa kuliko kuishi.”
Therefore now, O LORD, take, I beseech Thee, my life from me; for it is better for me to die than to live.'
4 Bwana akasema, Je, ni vema kwamba umekasirika?”
And the LORD said: 'Art thou greatly angry?'
5 Kisha Yona akaondoka mjini akaketi upande wa mashariki wa jiji. Huko alifanya makao na akaketi chini yake katika kivuli ili aweze kuona mji utakuwaje.
Then Jonah went out of the city, and sat on the east side of the city, and there made him a booth, and sat under it in the shadow, till he might see what would become of the city.
6 Bwana Mungu aliandaa mmea na kuukuza juu ya Yona ili uwe kivuli juu ya kichwa chake ili kupunguza dhiki yake. Yona alikuwa na furaha kubwa kwa sababu ya mmea.
And the LORD God prepared a gourd, and made it to come up over Jonah, that it might be a shadow over his head, to deliver him from his evil. So Jonah was exceeding glad because of the gourd.
7 Lakini Mungu aliandaa mdudu kulipopambazuka asubuhi iliyofuata. Alishambulia mmea na mmea ukapooza.
But God prepared a worm when the morning rose the next day, and it smote the gourd, that it withered.
8 Ikawa wakati jua lilipochomoza asubuhi, Mungu aliandaa upepo mkali wa mashariki. Pia, jua lilipiga kichwa cha Yona na akaanguka. Kisha Yona alitamani kufa. Akajiambia, “Ni bora kwangu kufa kuliko kuishi.”
And it came to pass, when the sun arose, that God prepared a vehement east wind; and the sun beat upon the head of Jonah, that he fainted, and requested for himself that he might die, and said: 'It is better for me to die than to live.'
9 Kisha Mungu akamwambia Yona, “Je, ni vema wewe kuwa na hasira juu ya mmea?” Yona akasema, Ni vyema kuwa nimekasirika hata kufa.
And God said to Jonah: 'Art thou greatly angry for the gourd?' And he said: 'I am greatly angry, even unto death.'
10 Bwana akasema, Umeuhurumia mmea, ambao haukuufanyia kazi wala haukukua. Uliomea katika usiku na kufa usiku.
And the LORD said: 'Thou hast had pity on the gourd, for which thou hast not laboured, neither madest it grow, which came up in a night, and perished in a night;
11 Kwa hiyo mimi, haikunipassa kuuhurumia Ninawi, mji mkuu, ambalo kuna watu zaidi ya mia na ishirini elfu ambao hawajui tofauti kati ya mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto, na pia ng'ombe wengi?
and should not I have pity on Nineveh, that great city, wherein are more than sixscore thousand persons that cannot discern between their right hand and their left hand, and also much cattle?'

< Yona 4 >