< Mika 1 >

1 Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Mika Mmorashti katika siku za Yotahamu, Ahazi, na Hezekeia, mfalme wa Yuda, lile neno aliloliona kuhusiana na Samaria na Yerusalemu.
THE WORD of the LORD that came to Micah the Morashtite in the days of Jotham, Ahaz, and Hezekiah, kings of Judah, which he saw concerning Samaria and Jerusalem.
2 Sikilizeni, ninyi watu wote. Sikilizeni, dunia, na vyote vilivyomo kwenye dunia. Acheni Yahwe ashuhudiwe dhidi yenu, Bwana kutoka kwenye hekalu lake takatifu.
Hear, ye peoples, all of you; Hearken, O earth, and all that therein is; and let the Lord GOD be witness against you, the Lord from His holy temple.
3 Tazama, Yahwe anakuja kutoka mahali pake; atashuka chini na kupakanyaga mahali pa juu katika dunia.
For, behold, the LORD cometh forth out of His place, and will come down, and tread upon the high places of the earth.
4 Milima itayeyuka chini yake; mabonde yatapasuka vipande vipande kama mshumaa mbele ya moto, kama maji ambayo yamemwagika chini ya mteremko mkali.
And the mountains shall be molten under Him, and the valleys shall be cleft, as wax before the fire, as waters that are poured down a steep place.
5 Haya yote ni kwasababu ya uasi wa Yakobo, na kwasababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Je sababu ilikuwa nini kwa uasi wa Yakobo? Je ilikuwa Samaria? Je sababu ilikuwa nini kwa mahali pa juu pa Yuda? Je haiukuwa Yerusalemu?
For the transgression of Jacob is all this, and for the sins of the house of Israel. What is the transgression of Jacob? is it not Samaria? And what are the high places of Judah? are they not Jerusalem?
6 “Nitaifanya Samaria rundo la uharibifu katika shamba, kama eneo la kupandia mizabibu. Nitayavuta mawe ya jengo lake kwenda kwenye bonde; Nitaifunua misingi yake.
Therefore I will make Samaria a heap in the field, a place for the planting of vineyards; and I will pour down the stones thereof into the valley, and I will uncover the foundations thereof.
7 Sanamu zake zote za kuchonga zitapondwa vipande vipande; na zawadi zake zote zitachomwa moto. Kwa kuwa zawadi zake za ukahaba amezikusanya, na kama malipo ya ukahaba yatarudi.”
And all her graven images shall be beaten to pieces, and all her hires shall be burned with fire, and all her idols will I lay desolate; for of the hire of a harlot hath she gathered them, and unto the hire of a harlot shall they return.
8 Kwa sababu hii nitalia na kuomboleza; nitaenda peku peku na uchi; Nitaomboleza kama mbeha na kuomboleza kama bundi.
For this will I wail and howl, I will go stripped and naked; I will make a wailing like the jackals, and a mourning like the ostriches.
9 Kwa kuwa jeraha lake haliponi, kwa kuwa imefika kwa Yuda. Imefikia lango la watu wangu, hadi Yerusalemu.
For her wound is incurable; for it is come even unto Judah; it reacheth unto the gate of my people, even to Jerusalem.
10 Msiache kuwambia kuhusu katika Gathi; msilie tena. Katika Bethi Leafra nabiringisha mwenyewe kwenye mavumbi.
Tell it not in Gath, weep not at all; at Beth-le-aphrah roll thyself in the dust.
11 Piteni karibu na, makao ya Shafiri, katika uchi na aibu. Makazi ya Zaanani hayatatoka nje. Maombolezo ya Beth Ezeli, kwa ajili ya ulinzi yamechukuliwa.
Pass ye away, O inhabitant of Saphir, in nakedness and shame; the inhabitant of Zaanan is not come forth; the wailing of Beth-ezel shall take from you the standing-place thereof.
12 Kwa kuwa wakaaji wa Marothi hungoja habari njema, kwa sababu hofu, kwa sababu msiba umetoka kwa Yahwe hadi kwenye malango ya Yerusalemu.
For the inhabitant of Maroth waiteth anxiously for good; because evil is come down from the LORD unto the gate of Jerusalem.
13 Wfuungeni lijamu farasi wakokote gari la farasi, makazi ya Lakishi. Wewe Lakishi, ulikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalionekana kwako.
Bind the chariots to the swift steeds, O inhabitant of Lachish; she was the beginning of sin to the daughter of Zion; for the transgressions of Israel are found in thee.
14 Hivyo utaipa zawadi ya kuagia Moreshethi Gathi; mji wa Akzibu utawavunja moyo wafalme wa Israeli.
Therefore shalt thou give a parting gift to Moresheth-gath; the houses of Achzib shall be a deceitful thing unto the kings of Israel.
15 Tena nitaleta ushindi kwako, makazi ya Maresha; uzuri wa Israeli utakuja Adulamu.
I will yet bring unto thee, O inhabitant of Mareshah, him that shall possess thee; the glory of Israel shall come even unto Adullam.
16 Kata kipara chako na kata nywele zako kwa ajili ya watoto ambao unaowafurahisha. Fanya kipara chako mwenyewe kama tai, kwa ajili ya watoto wako watakao kwenda utumwani kutoka kwako
Make thee bald, and poll thee for the children of thy delight; enlarge thy baldness as the vulture; for they are gone into captivity from thee.

< Mika 1 >