< Yona 3 >

1 Neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili, akisema,
And the word of the LORD came unto Jonah the second time, saying:
2 “Ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa, na uhubiri ujumbe ule ambao nitakuagiza.”
'Arise, go unto Nineveh, that great city, and make unto it the proclamation that I bid thee.'
3 Basi Yona akaondoka akaenda Niniawi kwa kutii neno la Bwana. Sasa Ninawi ilikuwa mji mkubwa sana, ilikuwa safari ya siku tatu.
So Jonah arose, and went unto Nineveh, according to the word of the LORD. Now Nineveh was an exceeding great city, of three days' journey.
4 Yona akaanza kuingia ndani ya mji, na baada ya safari ya siku, akapaza sauti, akasema, “Katika siku arobaini Ninawi itaangamizwa.”
And Jonah began to enter into the city a day's journey, and he proclaimed, and said: 'Yet forty days, and Nineveh shall be overthrown.'
5 Watu wa Ninawi walimwamini Mungu na wakatangaza kufunga. Wote hwakavaa nguo za magunia, kutoka aliyemkubwa hata mdogo.
And the people of Nineveh believed God; and they proclaimed a fast, and put on sackcloth, from the greatest of them even to the least of them.
6 Mapema habari zilimfikia mfalme wa Ninawi. Akasimama kutoka kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika magunia, akaketi katika majivu.
And the tidings reached the king of Nineveh, and he arose from his throne, and laid his robe from him, and covered him with sackcloth, and sat in ashes.
7 Alitoa tangazo ambalo lilsemalo, “katika mji wa Ninawi, kwa mamlaka ya mfalme na wakuu wake, msiruhusu mtu wala mnyama, ng'ombe wala kundi, asionje kitu chochote. Wao wasile wala kunywe maji.
And he caused it to be proclaimed and published through Nineveh by the decree of the king and his nobles, saying: 'Let neither man nor beast, herd nor flock, taste any thing; let them not feed, nor drink water;
8 Lakini watu na wanyama wawe wamefunikwa kwa magunia na walie kwa sauti kubwa kwa Mungu. Kila mtu ageuke na kuacha njia yake mbaya na kutoka katika udhalimu uliyopo mikononi mwake.
but let them be covered with sackcloth, both man and beast, and let them cry mightily unto God; yea, let them turn every one from his evil way, and from the violence that is in their hands.
9 Nani anajua? Mungu anaweza kurejea na kubadili mawazo yake na kuacha ghadhabu yake kali ili tusiangamie.”
Who knoweth whether God will not turn and repent, and turn away from His fierce anger, that we perish not?'
10 Mungu akaona yale waliyoyafanya, wakaziacha njia zao mbaya. Kwa hiyo Mungu alibadili mawazo yake juu ya adhabu aliyowaambia angewafanyia, nae hakufanya hivyo.
And God saw their works, that they turned from their evil way; and God repented of the evil, which He said He would do unto them; and He did it not.

< Yona 3 >