< Ayubu 38 >

1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Тогава Господ отговори на Иова из бурята и каза:
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
Кой е тогава този, който помрачава Моя съвет С неразумни думи?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Опаши сега кръста си като мъж, И ще те попитам; и ти ми изяснявай,
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
Где беше ти, когато основах земята? Извести, ако си разумен:
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Кой определи мерките й? (ако знаеш) Или кой тегли връв за мерене по нея?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
На какво се вдълбочиха основите й? Или кой положи краеъгълния й камък,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
Когато звездите на зората пееха заедно, И всички Божии синове възклицаваха от радост?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
Или кой затвори морето с врати, Когато се устреми та излезе из матка,
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
Когато го облякох с облак И го пових с мъгла,
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
И поставих му граница от Мене, Турих лостове и врати,
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
И рекох: До тук ще дохождаш, но не по-нататък, И тук ще се спират гордите ти вълни?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
Откак започнаха дните ти заповядал ли си ти на утрото И показал на зората мястото й,
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
За да обхване краищата на земята, Така щото да се изтърсят от нея злодейците
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
Та да се преобразува тя, както глина под печат, И всичко да изпъква като че ли в облекло,
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
А от нечестивите да се отнеме виделината им, И издигнатата им мишца да се строши?
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
Проникнал ли си до изворите на морето? Или ходил ли си да изследваш бездната?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Откриха ли се на тебе вратите на смъртта? Или видял ли си сенчестите врати на смъртта?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
Схванал ли си широчината на земята? Кажи, ако си разбрал всичко това.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
Где е пътят към обиталището на светлината? И на тъмнината где е мястото й,
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
За да й заведеш до границата й, И да познаеш пътеките към дома й?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Без съмнение, ти знаеш, защото тогаз си се родил, И голямо е числото на твоите дни!
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Влизал ли си в съкровищниците за снега, Или виждал ли си съкровищниците за градушката,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
Които пазя за време на скръб, За ден на бой и на война?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
Що е пътят за мястото, гдето се разсява светлината, Или се разпръсва по земята източният вятър?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Кой е разцепил водопровод за проливните дъждове, Или път за светкавицата на гръма,
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
За да се докара дъжд върху ненаселена земя, Върху пустинята, гдето няма човек,
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
За да насити пустата и запустяла земя. И да направи нежната трева да изникне?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
Дъждът има ли баща? Или кой е родил капките на росата?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
От чия матка излиза ледът? И кой е родил небесната слана?
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
Когато водите се втвърдяват като камък, И повърхността на бездната се смръзва.
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
Ти ли връзваш връзките на Плеадите, Или развързваш въжетата на Ориона?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Извеждаш ли Мазарот на времето му? Или управляваш ли Мечката с малките й?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Познаваш ли законите на небето? Установяваш ли неговото владичество върху земята?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
Издигаш ли гласа си до облаците, За да те покрият изобилни води?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Изпращаш ли светкавици, та да излизат И да ти казват: Ето ни?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Кой е турил мъдрост в облаците? Или кой е дал разум на гъстите облаци?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Кой с мъдрост брои облаците? Или кой излива небесните мехове
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
Та да се сгъстява пръстта в куп, И буците да се слепят?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
Улавят ли лов за лъвицата? Или насищат ли охотата на лъвовите малки,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
Когато седят в рововете си, И остават в скривалищата за да причакват?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Кой приготвя за враната храната й, Когато пилетата й от нямане храна Се скитат и викат към Бога?

< Ayubu 38 >