< Wahebrania 11 >

1 Sasa imani ni hakika aliyo nayo mtu wakati atarajiapo kitu fulani kwa ujasiri. Ni hakika ya kitu ambacho bado hakijaonekana.
Or la foi est l'assurance des choses qu'on espère, la preuve de celles qu'on ne voit pas.
2 Kwa sababu hii mababu zetu walithibitika kwa imani yao.
Car c'est par là que les anciens ont obtenu l'approbation.
3 Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa amri ya Mungu, ili kwamba kile kinachoonekana hakikutengenezwa kutokana na vitu ambavyo vilikuwa vinaonekana. (aiōn g165)
Par la foi, nous comprenons que l'univers a été formé par la parole de Dieu, de sorte que ce que l'on voit n'a pas été fait à partir de choses visibles. (aiōn g165)
4 Ilikuwa kwa sababu ya imani kwamba Habili alimtolea Mungu sadaka ya kufaa kuliko alivyofanya Kaini. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba alisifiwa kuwa mwenye haki. Mungu alimsifu kwa sababu ya zawadi alizoleta. Kwa sababu hiyo, Habili bado ananena, ingawa amekufa.
Par la foi, Abel a offert à Dieu un sacrifice plus excellent que celui de Caïn, par lequel il a reçu le témoignage qu'il était juste, Dieu témoignant à l'égard de ses dons, et par lequel, bien que mort, il parle encore.
5 Ilikuwa kwa imani kwamba Enoko alichukuliwa juu na hakuona mauti. “Hakuonekana, kwa sababu Mungu alimchukua” kwa vile ilinenwa juu yake kuwa alimpendeza Mungu kabla ya kuchukuliwa juu.
C'est par la foi qu'Hénoc a été enlevé, afin qu'il ne voie pas la mort, et qu'il n'a pas été retrouvé, parce que Dieu l'a traduit. Car il lui a été rendu témoignage qu'avant sa translation il avait été bien agréable à Dieu.
6 Pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa kuwa ajaye kwa Mungu lazima aamini kwamba Mungu anaishi na kwamba huwapatia zawadi wale wamtafutao.
Sans la foi, il est impossible de lui être agréable, car celui qui s'approche de Dieu doit croire qu'il existe et qu'il est le rémunérateur de ceux qui le cherchent.
7 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Nuhu, akiwa ameonywa na Mungu kuhusiana na mambo ambayo hayakuwa yameonekana, kwa heshima ya ki Mungu alitengeneza safina kwa ajili ya kuiokoa familia yake. Kwa kufanya hivi, aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ambayo huja kupitia imani.
Par la foi, Noé, averti des choses qu'on ne voyait pas encore, et animé d'une crainte pieuse, a préparé un navire pour sauver sa maison, par lequel il a condamné le monde et est devenu héritier de la justice selon la foi.
8 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu, alipoitwa alitii na kwenda mahali ambapo alipaswa kupokea kama urithi. Alitoka bila kujua mahali gani alikuwa anakwenda.
C'est par la foi qu'Abraham, lorsqu'il fut appelé, obéit pour sortir vers le lieu qu'il devait recevoir en héritage. Il sortit, sans savoir où il allait.
9 Ilikuwa ni kwa imani kwamba aliishi katika nchi ya ahadi kama mgeni. Aliishi katika mahema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi wenzake wa ahadi ile ile.
C'est par la foi qu'il vécut comme un étranger dans la terre promise, comme dans une terre qui ne lui appartenait pas, habitant sous des tentes avec Isaac et Jacob, héritiers avec lui de la même promesse.
10 Hii ni kwa sababu alitarajia kuupata mji ambao mwenye kuubuni na mjenzi wake angelikuwa ni Mungu.
Car il attendait la cité qui a des fondements, et dont Dieu est le constructeur et l'artisan.
11 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu, na Sara mwenyewe, walipokea nguvu ya kutunga mimba ingawa walikuwa wazee sana, kwa kuwa walimuona Mungu kuwa mwaminifu, ambaye aliwaahidia mtoto wa kiume.
C'est par la foi que Sara elle-même a reçu le pouvoir de concevoir, et qu'elle a enfanté un enfant à un âge avancé, car elle a considéré comme fidèle celui qui avait promis.
12 Kwa hiyo pia kutoka kwa mtu huyu mmoja ambaye alikuwa amekaribia kufa wakazaliwa watoto wasiohesabika. Walikuwa wengi kama nyota za angani na wengi kama mbegu za mchanga katika ufukwe wa bahari.
C'est pourquoi un seul homme a engendré autant d'enfants que les étoiles du ciel sont nombreuses, et aussi innombrables que le sable qui est au bord de la mer, et il est comme mort.
13 Hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea ahadi. Isipokuwa, wakiwa wameziona na kuzikaribisha kwa mbali, walikiri kwamba walikuwa wageni na wapitaji juu ya nchi.
Tous ceux-là sont morts dans la foi, n'ayant pas reçu les promesses, mais les ayant vues et embrassées de loin, et ayant confessé qu'ils étaient étrangers et pèlerins sur la terre.
14 Kwa wale wasemao mambo kama haya wanaweka bayana kuwa wanatafuta nchi yao wenyewe.
Car ceux qui disent de telles choses montrent clairement qu'ils cherchent un pays à eux.
15 Kwa kweli, kama wangekuwa wakiifikiria nchi ambayo kwayo walitoka, wangelikuwa na nafasi ya kurejea.
Si en effet ils avaient pensé au pays d'où ils sont partis, ils auraient eu le temps de revenir.
16 Lakini kama ilivyo, wanatamani nchi iliyo bora, ambayo, ni ya kimbingu. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa ametayarisha mji kwa ajili yao.
Mais maintenant ils désirent un pays meilleur, c'est-à-dire un pays céleste. C'est pourquoi Dieu n'a pas honte d'eux, d'être appelé leur Dieu, car il leur a préparé une cité.
17 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu baada ya kujaribiwa, alimtoa Isaka. Ndiyo, yeye ambaye alipokea kwa furaha ahadi, alimtoa mwanawe wa pekee,
Par la foi, Abraham, mis à l'épreuve, offrit Isaac. En effet, celui qui avait reçu avec joie les promesses offrait son fils unique,
18 ambaye juu yake ilinenwa, “Kutoka kwa Isaka uzao wako utaitwa.”
à qui il avait été dit: « Ta descendance sera comptée comme celle d'Isaac »,
19 IbrahImU alijua kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kumfufua Isaka kutoka katika wafu, na kwa kuzungumza kwa lugha ya maumbo, alimpokea.
concluant que Dieu est capable de ressusciter même d'entre les morts. Au sens figuré, il l'a aussi ressuscité d'entre les morts.
20 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Isaka alimbariki Yakobo na Esau kuhusu mambo yajayo.
C'est par la foi qu'Isaac a béni Jacob et Ésaü, même en ce qui concerne les choses à venir.
21 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Yakobo alipokuwa katika hali ya kufa, alimbariki kila mmoja wa watoto wa Yusufu. Yakobo akaabudu, akiegemea juu ya fimbo yake.
C'est par la foi que Jacob, à sa mort, bénit chacun des fils de Joseph et se prosterna, appuyé sur le sommet de son bâton.
22 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Yusufu wakati wake wa mwisho ulipokaribia, alinena juu ya kutoka kwa wana wa Israel Misri na akawaagiza kuchukua pamoja nao mifupa yake.
C'est par la foi que Joseph, lorsque sa fin approcha, fit mention du départ des enfants d'Israël, et donna des instructions concernant ses ossements.
23 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa, alipozaliwa, alifichwa kwa miezi mitatu na wazazi wake kwa sababu walimuona kuwa ni mtoto mchanga aliyekuwa mzuri, na hawakutishwa na amri ya mfalme.
C'est par la foi que Moïse, à sa naissance, fut caché pendant trois mois par ses parents, parce qu'ils virent qu'il était un bel enfant; et ils ne craignirent pas l'ordre du roi.
24 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa, alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mtoto wa binti Farao.
C'est par la foi que Moïse, devenu grand, refusa d'être appelé fils de la fille de Pharaon,
25 Badala yake, alichagua kushiriki mateso pamoja na watu wa Mungu badala ya kufurahia anasa za dhambi kwa kitambo.
préférant partager les mauvais traitements du peuple de Dieu plutôt que de jouir pour un temps des plaisirs du péché,
26 Alifikiri aibu ya kumfuata Kristo kuwa ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri kwa kuwa alikaza macho yake katika zawadi ya wakati wake ujao.
considérant l'opprobre du Christ comme une plus grande richesse que les trésors de l'Égypte, car il en attendait la récompense.
27 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa alitoka Misri. Hakuhofia hasira ya Mfalme, kwa kuwa alivumilia kwa kutazama kwa asiyeonekana.
C'est par la foi qu'il quitta l'Égypte, sans craindre la colère du roi, car il endurait, comme s'il voyait celui qui est invisible.
28 Ilikuwa ni kwa imani kwamba aliishika pasaka na kunyunyiza damu, ili kwamba mharibu wa mzaliwa wa kwanza asiweze kuwagusa wazaliwa wa kwanza wa kiume wa waisrael.
C'est par la foi qu'il a gardé la Pâque et l'aspersion du sang, afin que le destructeur des premiers-nés ne les touche pas.
29 Ilikuwa ni kwa imani kwamba walipita katika bahari ya shamu kama katika nchi kavu. Wakati wamisri walipojaribu kupita, walimezwa.
C'est par la foi qu'ils traversèrent la mer Rouge comme sur une terre sèche. Lorsque les Égyptiens ont essayé de le faire, ils ont été engloutis.
30 Ilikuwa ni kwa imani kwamba ukuta wa Yeriko ulianguka chini, baada ya kuuzunguka kwa siku saba.
C'est par la foi que les murs de Jéricho sont tombés après avoir été encerclés pendant sept jours.
31 Ilikuwa ni kwa imani kwamba Rahabu yule kahaba hakuangamia pamoja na wale ambao hawakuwa watiifu, kwa sababu alikuwa amewapokea wapelelezi na kuwahifadhi salama.
C'est par la foi que Rahab la prostituée n'a pas péri avec les désobéissants, ayant reçu les espions en paix.
32 Na niseme nini zaidi? Maana muda hautoshi kusimulia ya Gideoni, Barak, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samwel na za manabii,
Que dirai-je encore? Car le temps me manquerait si je parlais de Gédéon, de Barak, de Samson, de Jephté, de David, de Samuel et des prophètes -
33 ambao kupitia imani walizishinda falme, walitenda haki, na wakapokea ahadi. Walizuia vinywa vya simba,
qui, par la foi, ont soumis des royaumes, exercé la justice, obtenu des promesses, fermé la gueule des lions,
34 walizima nguvu za moto, walikwepa ncha ya upanga, waliponywa kutoka katika magonjwa, walikuwa mashujaa vitani, na walisababisha majeshi wageni kukimbia.
éteint la puissance du feu, échappé au tranchant de l'épée, se sont fortifiés à partir de leur faiblesse, sont devenus puissants à la guerre et ont mis en fuite les armées étrangères.
35 Wanawake walipokea wafu wao kwa njia ya ufufuo. Wengine waliteswa, bila kukubali kuachwa huru ili kwamba waweze kupata uzoefu wa ufufuo ulio bora zaidi.
Des femmes ont reçu leurs morts par résurrection. D'autres ont été torturés, n'acceptant pas leur délivrance, afin d'obtenir une meilleure résurrection.
36 Wengine waliteswa kwa dhihaka na kwa vichapo, naam, hata kwa vifungo na kwa kutiwa gerezani.
D'autres ont été éprouvés par la moquerie et la flagellation, et même par les liens et la prison.
37 Walipondwa mawe. Walikatwa vipande kwa misumeno. Waliuawa kwa upanga. Walikwenda kwa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi walikuwa wahitaji, wakiendelea katika maumivu na wakitendewa mabaya
Ils ont été lapidés. On les a sciés. Ils ont été tentés. Ils ont été tués par l'épée. Ils allaient et venaient, vêtus de peaux de brebis et de peaux de chèvres, dans la misère, l'affliction, les mauvais traitements,
38 (ambayo ulimwengu haukustahili kuwa nao), wakitangatanga nyikani, milimani, katika mapango na katika mashimo ya ardhini.
eux dont le monde n'était pas digne, errant dans les déserts, les montagnes, les cavernes et les trous de la terre.
39 Ingawa watu wote hawa walikubaliwa na Mungu kwa sababu ya imani yao, hawakupokea alichoahidi.
Tous ceux-là, après avoir été recommandés pour leur foi, n'ont pas reçu la promesse,
40 Mungu alitangulia kutupatia kitu kilichobora, ili kwamba bila sisi wasingeweza kukamilishwa.
Dieu ayant prévu quelque chose de meilleur à notre égard, afin que, sans nous, ils ne soient pas parfaits.

< Wahebrania 11 >