< Wahebrania 10 >

1 Kwa vile sheria ni kivuli cha mambo mema yajayo, si yale yaliyo halisi. Sheria kamwe haiwezi kuwakamilisha wale ambao wanaomkaribia Mungu kwa njia ya dhabihu zilezile ambazo makuhani waliendelea kutoa mwaka baada ya mwaka.
Car la loi, qui n'est qu'une ombre des biens à venir, et non l'image même de ces biens, ne peut jamais, avec les mêmes sacrifices qu'on offre chaque année, rendre parfaits ceux qui s'approchent.
2 Au vinginevyo dhabihu hizo zisingeweza kukoma kutolewa? Kwa kigezo hicho waabuduo, wakiwa wamesafishwa mara moja, wasingelikuwa na utambuzi zaidi wa dhambi.
Ou bien n'auraient-ils pas cessé d'être offerts, parce que les adorateurs, une fois purifiés, n'auraient plus eu conscience de leurs péchés?
3 Bali katika dhabihu hizo kuna ukumbusho wa dhambi zilizotendwa mwaka baada ya mwaka.
Mais dans ces sacrifices, il y a un rappel annuel des péchés.
4 Kwa kuwa haiwezekani kwa damu ya mafahari na mbuzi kuziondoa dhambi.
Car il est impossible que le sang des taureaux et des boucs ôte les péchés.
5 Wakati Kristo alipokuja duniani, alisema, “Hamkutamani matoleo au dhabihu, badala yake, mliandaa mwili kwa ajili yangu.
C'est pourquoi, lorsqu'il vient dans le monde, il dit, « Tu n'as pas désiré de sacrifice et d'offrande, mais tu as préparé un corps pour moi.
6 Hamkuwa na thamani katika matoleo yote ya kuteketezwa au dhabihu kwa ajili ya dhambi.
Tu n'as pas aimé les holocaustes entiers et les sacrifices pour le péché.
7 Kisha nilisema, “Ona, hapa ninayafanya mapenzi yako, Mungu, kama ilivyoandikwa kunihusu mimi katika gombo”.
Et je dis: « Voici, je suis venu (il est écrit de moi dans le rouleau du livre)". pour faire ta volonté, ô Dieu. »
8 Alisema kama ilivyo semwa hapo juu: “Hamkutamani dhabihu, matoleo, au sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya dhambi, wala hukuona furaha ndani yake” dhabihu ambazo zinatolewa kulingana na sheria.
Ayant dit auparavant: « Tu n'as pas désiré les sacrifices et les offrandes, les holocaustes entiers et les sacrifices pour le péché, et tu n'y as pas pris plaisir » (ceux qui sont offerts selon la loi),
9 Kisha alisema, “Ona, niko hapa kufanya mapenzi yako”. Ameweka pembeni taratibu zilizo za awali ili kuimarisha zile za pili.
il a dit ensuite: « Voici, je suis venu pour faire ta volonté ». Il enlève les premiers, afin d'établir les seconds,
10 Katika taratibu za pili, tumekwisha tengwa kwa Mungu kwa mapenzi yake kupitia kujitoa kwa mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa nyakati zote.
volonté par laquelle nous avons été sanctifiés par l'offrande du corps de Jésus-Christ une fois pour toutes.
11 Ni kweli, kila kuhani husimama kwa huduma siku kwa siku, akitoa dhabihu ile ile, ambayo, kwa vyovyote, kamwe isingeweza kuziondoa dhambi.
Tout prêtre, en effet, se tient chaque jour debout pour servir et offrir souvent les mêmes sacrifices, qui ne peuvent jamais ôter les péchés.
12 Lakini baada ya Kristo kutoa dhabihu mara moja kwa dhambi milele yote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu,
Mais lui, après avoir offert pour toujours un seul sacrifice pour les péchés, s'est assis à la droite de Dieu.
13 akisubiri mpaka maadui zake watiwe chini na kufanywa kiti kwa ajili ya miguu yake.
Depuis lors, il attend que ses ennemis soient devenus le marchepied de ses pieds.
14 Kwa kuwa kwa njia ya toleo moja amewakamilisha milele wale ambao wametengwa kwa Mungu.
Car, par une seule offrande, il a rendu parfaits pour toujours ceux qui sont sanctifiés.
15 Na Roho Mtakatifu pia ashuhudia kwetu. Kwa kuwa kwanza alisema,
Le Saint-Esprit nous en rend aussi témoignage, car après avoir dit,
16 “Hili ni agano nitakalofanya pamoja nao baada ya siku hizo; asema Bwana: nitaweka sheria zangu ndani ya mioyo yao, na nitaziandika katika akili zao”.
« Voici l'alliance que je conclurai avec eux. après ces jours-là », dit le Seigneur, « Je mettrai mes lois sur leur cœur, Je les écrirai aussi sur leur esprit; » puis il dit,
17 Kisha alisema, “Hawatazikumbuka tena dhambi na matendo yao mafu”.
« Je ne me souviendrai plus de leurs péchés ni de leurs iniquités. »
18 Sasa mahali palipo na msamaha kwa hawa, hakuna tena dhabihu yoyote kwa ajili ya dhambi.
Or, là où il y a rémission, il n'y a plus d'offrande pour le péché.
19 Kwa hiyo, ndugu, tunao ujasiri wa kuingia mahali patakatifu zaidi kwa damu ya Yesu.
Ayant donc, frères, la hardiesse d'entrer dans le sanctuaire par le sang de Jésus,
20 Hiyo ni njia ambayo ameifungua kwa ajili yetu kwa njia ya mwili wake, mpya na hai inayopitia kwenye pazia.
par le chemin qu'il nous a frayé, un chemin nouveau et vivant, à travers le voile, c'est-à-dire sa chair,
21 Na kwa sababu tunaye kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
et ayant un grand prêtre sur la maison de Dieu,
22 na tumkaribie na moyo wa kweli katika utimilifu wa uhakika wa imani tukiwa na mioyo iliyonyunyiziwa safi kutoka uovu wa dhamiri na kuwa na miili yetu iliyooshwa kwa maji safi.
approchons-nous avec un cœur sincère, dans la plénitude de la foi, le cœur purifié d'une mauvaise conscience et le corps lavé d'une eau pure,
23 Basi na tushikilie kwa uthabiti katika ungamo la ujasiri wa tumaini letu, bila ya kugeuka, kwa sababu Mungu aliyeahidi ni mwaminifu.
retenant sans faiblir la confession de notre espérance, car celui qui a promis est fidèle.
24 Na tuzidi kutafakari namna ya kumtia moyo kila mmoja kupenda na matendo mema.
Réfléchissons aux moyens de nous exciter les uns les autres à l'amour et aux bonnes œuvres,
25 Na tusiache kukusanyika pamoja, kama wafanyavyo wengine. Badala yake, kutiana moyo kila mmoja zaidi na zaidi, kama muonavyo siku inakaribia.
sans renoncer à nous réunir, comme c'est la coutume de quelques-uns, mais en nous exhortant les uns les autres, et cela d'autant plus que vous voyez s'approcher le Jour.
26 Kama tukifanya makusudi kuendelea kutenda dhambi baada ya kuwa tumepokea elimu ya ukweli, Dhabihu nyingine ya dhambi haisalii tena.
Car si nous péchons volontairement après avoir reçu la connaissance de la vérité, il ne reste plus de sacrifice pour les péchés,
27 Badala yake, kuna tarajio pekee la hukumu ya kutisha, na ukali wa moto ambao utawateketeza maadui wa Mungu.
mais une attente redoutable du jugement, et une ardeur de feu qui dévorera les adversaires.
28 Yeyote ambaye ameikataa sheria ya Musa hufa bila rehema mbele ya ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.
L'homme qui ne respecte pas la loi de Moïse meurt sans pitié, sur la parole de deux ou trois témoins.
29 kiwango gani zaidi cha adhabu unafikiri kinamstahiri kilammoja ambaye amemdharau mwana wa Mungu, yeyote aliyeitendea damu ya agano kama kitu kisicho kitakatifu, damu ambayo kwayo aliiweka wakfu kwa Mungu - yeyote ambaye amemtukana Roho wa neema?
De quel pire châtiment pensez-vous que sera jugé digne celui qui a foulé aux pieds le Fils de Dieu, qui a tenu pour impie le sang de l'alliance par laquelle il a été sanctifié, et qui a insulté l'Esprit de grâce?
30 Kwakuwa tunajua mmoja ambaye aliyesema, “Kisasi ni changu, nitalipa”. Na tena, “Bwana atawahukumu watu wake”.
Car nous connaissons celui qui a dit: « La vengeance m'appartient. Je rendrai la pareille, dit le Seigneur. Et encore: « Le Seigneur jugera son peuple. »
31 Ni jambo la kuogofya mtu kuangukia katika mikono ya Mungu aliye hai!
C'est une chose redoutable que de tomber entre les mains du Dieu vivant.
32 Lakini kumbuka siku zilizopita, baada ya kutiwa kwenu nuru, ni jinsi gani mliweza kuvumilia maumivu makali.
Mais rappelez-vous les jours anciens, où, après avoir été éclairés, vous avez enduré un grand combat dans les souffrances:
33 Mlikuwa mmewekwa wazi katika dhihaka ya matukano na mateso, na mlikuwa washiriki pamoja na wale waliopitia mateso kama hayo.
d'une part, en étant exposés à l'opprobre et à l'oppression, d'autre part, en devenant participants de ceux qui étaient ainsi traités.
34 Kwa kuwa mlikuwa na moyo wa huruma kwa hao waliokuwa wafungwa, na mlipokea kwa furaha adhabu ya urithi wenu, mkijua kwamba ninyi wenyewe mlikuwa na urithi bora na wa kudumu milele.
Mais vous avez eu pitié de moi dans mes chaînes et vous avez accepté avec joie le pillage de vos biens, sachant que vous avez pour vous un bien meilleur et durable dans les cieux.
35 Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, ulio na zawadi kuu.
Ne jetez donc pas votre audace, qui a une grande récompense.
36 Kwa kuwa mnahitaji uvumilivu, ili kwamba mpate kupokea ambacho Mungu amekiahidi, baada ya kuwa mmekwisha yatenda mapenzi yake.
Car il vous faut de l'endurance, afin que, ayant fait la volonté de Dieu, vous receviez la promesse.
37 Kwa kuwa baada ya kitambo kidogo, mmoja anayekuja, atakuja hakika na hatakawia.
« Dans très peu de temps, celui qui vient viendra viendra et n'attendra pas.
38 Mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Kama atarudi nyuma, sitapendezwa naye.”
Mais le juste vivra par la foi. S'il se rétracte, mon âme n'a aucun plaisir en lui. »
39 Lakini sisi si kama wale warudio nyuma kwa kuangamia. Badala yake, sisi ni baadhi ya wale tulio na imani ya kuzilinda roho zetu.
Mais nous ne sommes pas de ceux qui reculent jusqu'à la destruction, mais de ceux qui ont la foi pour le salut de l'âme.

< Wahebrania 10 >