< Yakobo 1 >

1 Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila kumi na mbili yaliyotawanyika, salaam.
Jacques, serviteur de Dieu et du Seigneur Jésus-Christ, aux douze tribus qui sont dans la Dispersion: Salutations.
2 Hesabuni kuwa ni furaha zaidi, ndugu zangu, mnapopita katika matatizo mbali mbali,
Réjouissez-vous, mes frères, lorsque vous tombez dans diverses tentations,
3 mkijua kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huwapa uvumilivu.
sachant que l'épreuve de votre foi produit l'endurance.
4 Acheni uvumilivu uikamilishe kazi yake, kwamba muweze kukomaa kikamilifu, bila kupungukiwa katika lolote.
Que l'endurance fasse son œuvre parfaite, afin que vous soyez parfaits et complets, ne manquant de rien.
5 Lakini kama mtu kati yenu anahitaji hekima, aiombe kutoka kwa Mungu, ambaye hutoa kwa ukarimu na pasipo kukemea kwa wote wamwombao, na atawapa hekima.
Mais si quelqu'un d'entre vous manque de sagesse, qu'il la demande à Dieu, qui donne à tous libéralement et sans reproche, et elle lui sera donnée.
6 Lakini omba kwa imani, bila shaka, kwa kuwa mwenye kutia shaka ni kama mawimbi katika bahari, huchukuliwa na upepo na kutupwa huku na huko.
Mais qu'il demande avec foi, sans douter, car celui qui doute est semblable à une vague de la mer, poussée par le vent et agitée.
7 Kwa hakika mtu huyu asifikirie kwamba atapokelewa ombi lake kutoka kwa Bwana;
Car cet homme ne doit pas penser qu'il recevra quelque chose du Seigneur.
8 mtu huyu ana nia mbili, si imara katika njia zake zote.
C'est un homme à double pensée, instable dans toutes ses voies.
9 Ndugu maskini anapaswa kujivuna katika kusimama kwake juu,
Que le frère dans l'humilité se glorifie de sa haute situation;
10 wakati huo huo ndugu tajiri katika unyenyekevu wake, kwa sababu atatoweka kama ua la kondeni katika shamba analopita.
et le riche, de ce qu'il est rendu humble, car, comme la fleur dans l'herbe, il passera.
11 Jua huchomoza na joto la kuunguza kukausha mimea, na maua huanguka na uzuri wake hufa. Vivyo hivyo watu matajiri watachakaa katikati ya kazi zao.
Car le soleil se lève avec un vent brûlant et flétrit l'herbe; la fleur qu'elle contient tombe, et la beauté de son aspect périt. Ainsi, l'homme riche se fanera aussi dans ses occupations.
12 Amebarikiwa mtu yule anayevumilia majaribu, kwa kuwa baada ya kushinda jaribu hilo, atapokea taji ya uzima, ambayo imeahidiwa kwa wale wampendao Mungu.
Heureux celui qui supporte la tentation, car, après avoir été agréé, il recevra la couronne de vie que le Seigneur a promise à ceux qui l'aiment.
13 Mtu yeyote hapaswi kusema anapojaribiwa, “Jaribu hili linatoka kwa Mungu,” kwa sababu Mungu hajaribiwi na uovu, na Mungu mwenyewe hamjaribu yeyote.
Que personne ne dise, quand il est tenté: « Je suis tenté par Dieu », car Dieu ne peut être tenté par le mal, et lui-même ne tente personne.
14 Kila mtu hujaribiwa na tamaa zake mbaya zinazomshawishi na kumvuta mbali.
Mais chacun est tenté quand il est attiré par sa propre convoitise et séduit.
15 Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.
Alors la convoitise, quand elle a conçu, engendre le péché. Et le péché, quand il est devenu adulte, produit la mort.
16 Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
Ne vous y trompez pas, mes frères bien-aimés.
17 Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika hutoka juu, hushuka chini kutoka kwa Baba wa nuru. Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo.
Tout don agréable et tout don parfait viennent d'en haut, du Père des lumières, chez qui il n'y a ni variation ni ombre portée.
18 Mungu alichagua kutupa sisi uzima kwa Neno la kweli, ili kwamba tuweze kuwa kama uzao wa kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
De sa propre volonté, il nous a engendrés par la parole de la vérité, afin que nous soyons une sorte de prémices de ses créatures.
19 Mnajua hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea wala kukasirika,
Ainsi donc, mes frères bien-aimés, que chacun soit prompt à entendre, lent à parler, et lent à se mettre en colère;
20 kwa kuwa hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu.
car la colère de l'homme ne produit pas la justice de Dieu.
21 Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote ulio mahali popote, na kwa unyenyekevu lipokeeni neno lililopandwa ndani yenu, ambalo lina uwezo wa kuokoa roho zenu.
C'est pourquoi, rejetant toute souillure et tout débordement de méchanceté, recevez avec humilité la parole implantée, qui peut sauver vos âmes.
22 Litiini neno, msilisikie tu, mkijidanganya nafsi zenu wenyewe.
Mais mettez la parole en pratique, et ne vous contentez pas d'écouter, en vous trompant vous-mêmes.
23 Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.
Car si quelqu'un écoute la parole et ne la met pas en pratique, il est semblable à un homme qui regarde son visage naturel dans un miroir;
24 Hujitathimini uso wake, na huenda zake na baada ya muda mfupi husahau anavyofanana.
car il se voit lui-même, et s'en va, et aussitôt il oublie quelle sorte d'homme il était.
25 Bali mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili, sheria ya uhuru, na kuendelea kuitii, si kwa sababu yeye ni msikilizaji anayesahau, huyu mtu atabarikiwa anapoitenda.
Mais celui qui regarde la loi parfaite de la liberté et qui persévère, n'étant pas un auditeur qui oublie, mais un exécutant, celui-là sera béni dans ce qu'il fera.
26 Ikiwa mtu yeyote atafikiri mwenyewe kuwa ni mtu wa dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, huudanganya moyo wake na dini yake ni bure.
Si quelqu'un parmi vous se croit religieux alors qu'il ne tient pas sa langue en bride, mais trompe son cœur, la religion de cet homme est sans valeur.
27 Dini iliyo safi na isiyoharibiwa mbele za Mungu wetu na Baba ni hii: kuwasaidia yatima na wajane katika mateso yao, na kujilinda wenyewe na ufisadi wa dunia.
Voici ce qu'est une religion pure et sans tache devant notre Dieu et Père: visiter les orphelins et les veuves dans leur détresse, et se garder des souillures du monde.

< Yakobo 1 >