< Matendo 6 >

1 Sasa katika siku hizi, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa inaongezeka, lalamiko la Wayahudi wa Kiyunani lilianza dhidi ya Waebrania, kwa sababu wajane wao walikuwa wanasahaulika katika mgao wa kila siku wa chakula.
En ces jours-là, alors que le nombre des disciples se multipliait, une plainte s'éleva des Hellènes contre les Hébreux, parce que leurs veuves étaient négligées dans le service quotidien.
2 Mitume kumi na wawili waliwaita kusanyiko lote la wanafunzi na kusema, “Siyo sahihi kwetu kuliacha neno la Mungu na kuhudumia mezani.
Les douze convoquèrent la multitude des disciples et dirent: « Il n'est pas convenable que nous abandonnions la parole de Dieu pour servir des tables.
3 Kwa hiyo, ndugu, chagueni, wanaume saba, kutoka miongoni mwenu, watu wema, waliojaa Roho na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi huduma hii.
Choisissez donc parmi vous, frères, sept hommes de bonne réputation, pleins du Saint-Esprit et de sagesse, que nous nommerons responsables de cette affaire.
4 Na sisi, tutaendelea daima katika kuomba na katika huduma ya neno.”
Mais nous continuerons à persévérer dans la prière et dans le ministère de la parole. »
5 Hotuba yao ikaupendeza mkutano wote. Hivyo, wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena, na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
Ces paroles plurent à toute la foule. Ils choisirent Étienne, homme plein de foi et du Saint-Esprit, Philippe, Prochore, Nicanor, Timon, Parménas, et Nicolas, prosélyte d'Antioche,
6 Waumini waliwaleta watu hawa mbele ya mitume, walioomba na badaye wakawawekea mikono yao.
qu'ils placèrent devant les apôtres. Après avoir prié, ils leur imposèrent les mains.
7 Hivyo, neno la Mungu lilienea; na idadi ya wanafunzi ilizidi kuongezeka huko Yesrusalem; na idadi kubwa ya makuhani wakaitii imani.
La parole de Dieu augmentait et le nombre des disciples se multipliait à Jérusalem. Une grande partie des prêtres obéissait à la foi.
8 Na Stefano, aliyejaa neema na nguvu, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa miongoni mwa watu.
Étienne, plein de foi et de puissance, faisait parmi le peuple de grands prodiges et des miracles.
9 Lakini hapo wakainuka baadhi ya watu wafuasi wa Sinagogi liitwalo Sinagogi la Mahuru, na la Wakirene na la Waeskanderia, na baadhi kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa walikuwa wakihojiana na Stefano.
Mais quelques-uns de ceux de la synagogue dite des Libertins, des Cyrénéens, des Alexandrins, des Ciliciens et des Asiatiques, se levèrent pour disputer avec Étienne.
10 Lakini, hawakuweza kushindana na hekima na Roho ambayo Stefano alikuwa akitumia katika kuzungumza.
Ils ne purent résister à la sagesse et à l'Esprit par lesquels il parlait.
11 Kisha waliwashawishi baadhi ya watu kwa siri kusema, “Tumesikia Stefano akizungumza maneno ya kufuru dhidi ya Musa na dhidi ya Mungu.”
Alors ils firent dire secrètement à des hommes: « Nous l'avons entendu prononcer des paroles blasphématoires contre Moïse et contre Dieu. »
12 Waliwashurutisha watu, wazee, na waandishi, na kumwendea Stefano, wakamkamata, na kumleta mbele ya baraza.
Ils excitèrent le peuple, les anciens et les scribes, et vinrent contre lui. Ils le saisirent, puis l'amenèrent devant le conseil,
13 waliwaleta mashahidi wa uongo, waliosema, “mtu huyu haachi kunena maneno mabaya dhidi ya eneo hili takatifu na sheria.
et établirent de faux témoins qui dirent: « Cet homme ne cesse de proférer des paroles blasphématoires contre ce lieu saint et la loi.
14 Kwani tumemsikia akisema kwamba huyu Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali hapa na kuzibadili desturi tulizokabidhiwa na Musa.”
Car nous l'avons entendu dire que ce Jésus de Nazareth détruira ce lieu et changera les coutumes que Moïse nous a transmises. »
15 Kila mmoja aliyekuwa katika baraza, akaelekeza macho yake kumwangalia Stefano, nao wakauona uso wake ulikuwa kama uso wa malaika.
Tous ceux qui siégeaient au conseil, fixant les yeux sur lui, virent son visage comme celui d'un ange.

< Matendo 6 >