< Matendo 5 >

1 Hivyo, mtu mmoja aliyeitwa Anania, na Safira mkewe, waliuza sehemu ya mali,
Or, un homme nommé Ananias, avec Sapphira, sa femme, vendit une propriété,
2 na akaficha sehemu ya fedha waliyouza (mke wake pia alilijua hili), na akaleta sehemu iliyobakia na kuiweka kwenye miguu ya mitume.
et en retint une partie du prix; sa femme le savait aussi, puis elle en apporta une partie et la déposa aux pieds des apôtres.
3 Lakini Petro akasema, “Anania, kwa nini shetani ameujaza moyo wako kusema uongo kwa Roho Mtakatifu na kuficha sehemu ya mali ya shamba?
Mais Pierre dit: Ananias, pourquoi Satan a-t-il rempli ton cœur pour mentir au Saint-Esprit et pour retenir une partie du prix du terrain?
4 Wakati lilipokuwa halijauzwa, halikuwa ni mali yako? Na baada ya kuuzwa, halikuwa chini ya uamuzi wako? Ilikuwaje uwaze jambo hili moyoni mwako? Hujawadanganya wanadamu, bali umemdanganya Mungu.”
Tant que tu l'as gardé, n'est-il pas resté à toi? Après sa vente, n'était-elle pas en ton pouvoir? Comment se fait-il que tu aies conçu cette chose dans ton cœur? Tu n'as pas menti aux hommes, mais à Dieu. »
5 Katika kusikia maneno haya, Anania alidondoka chini na akakata roho. Na hofu kubwa iliwajia wote waliolisikia hili.
Ananias, entendant ces paroles, tomba et mourut. Une grande crainte s'empara de tous ceux qui entendirent ces choses.
6 Vijana wakaja mbele na kumtia katika sanda, na kumpeleka nje na kumzika.
Les jeunes gens, s'étant levés, l'enveloppèrent, l'emportèrent et l'ensevelirent.
7 Baada ya masaa matatu hivi, mke wake aliingia ndani, asijue ni nini kilichokuwa kimetokea.
Environ trois heures après, sa femme, qui ne savait pas ce qui était arrivé, entra.
8 Petro akamwambia, “Niambie, kama mliuza shamba kwa thamani hiyo.” Akasema, “Ndiyo, kwa thamani hiyo.”
Pierre lui dit: « Dis-moi si tu as vendu le terrain à un tel prix. » Elle a dit: « Oui, pour tant de choses. »
9 Kisha Petro akamwambia, “Inakuwaje kwamba mmepatana kwa pamoja kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu ya wale waliomzika mme wako iko mlangoni, na watakubeba na kukupeleka nje.”
Mais Pierre lui dit: « Comment se fait-il que vous vous soyez mis d'accord pour tenter l'Esprit du Seigneur? Voici que les pieds de ceux qui ont enseveli ton mari sont à la porte, et ils vont te porter dehors. »
10 Ghafla akadondoka miguuni pa Petro, akakata roho, na wale vijana wakaja ndani wakamkuta ameshakufa. Wakambeba kumpeleka nje, na kumzika karibu na mmewe.
Elle tomba aussitôt à ses pieds et mourut. Les jeunes gens entrèrent et la trouvèrent morte; ils la portèrent dehors et l`enterrèrent près de son mari.
11 Hofu kubwa ikaja juu ya kanisa zima, na juu ya wote walioyasikia mambo haya.
Une grande crainte s'empara de toute l'assemblée et de tous ceux qui entendirent ces choses.
12 Ishara nyingi na maajabu vilikuwa vinatokea miongoni mwa watu kupitia mikono ya mitume. Walikuwa pamoja katika ukumbi wa Sulemani.
Par les mains des apôtres, beaucoup de signes et de prodiges se produisaient parmi le peuple. Ils étaient tous d'un commun accord sous le portique de Salomon.
13 Lakini, hakuna mtu mwingine tofauti aliyekuwa na ujasiri wa kuambatana nao; hata hivyo, walipewa heshima ya juu na watu.
Aucun des autres n'osait se joindre à eux, mais le peuple les honorait.
14 Na pia, waamini wengi walikuwa wakiongezeka kwa Bwana, idadi kubwa ya wanaume na wanawake,
De plus en plus de croyants se joignaient au Seigneur, des multitudes d'hommes et de femmes.
15 kiasi kwamba hata waliwabeba wagonjwa mitaani, na kuwalaza vitandani na kwenye makochi, ili kwamba Petro akiwa anapita, kivuli chake kiweze kushuka juu yao.
On transportait même les malades dans les rues et on les couchait sur des lits et des matelas, afin que, lorsque Pierre passerait, son ombre au moins couvre quelques-uns d'entre eux.
16 Hapo pia, idadi kubwa ya watu walikuja kutoka miji iliyozunguka Yerusalem, wakiwaleta wagonjwa na wote waliopagawa na roho wachafu, na wote waliponywa.
La foule s'assemblait aussi des villes voisines de Jérusalem, amenant des malades et des personnes tourmentées par des esprits impurs; et tous étaient guéris.
17 Lakini kuhani mkuu aliinuka, na wote waliokuwa pamoja naye (ambao ni wa dhehebu la masadukayo); na walijawa na wivu
Mais le grand prêtre se leva, ainsi que tous ceux qui étaient avec lui (c'est la secte des sadducéens), et ils furent remplis de jalousie
18 wakanyosha mikono yao kuwakamata mitume na kuwaweka ndani ya gereza la jumla.
et mirent la main sur les apôtres, puis les mirent en prison publique.
19 Na wakati wa usiku malaika wa Bwana akaifungua milango ya gereza na kuwaongoza nje na kusema,
Mais un ange du Seigneur ouvrit de nuit les portes de la prison, les fit sortir et leur dit:
20 “Nendeni, mkasimame hekaluni na kuwaambia watu maneno yote ya Uzima huu.”
« Allez vous tenir debout et parlez au peuple dans le temple de toutes les paroles de cette vie. »
21 Waliposikia hili, waliingia hekaluni wakati wa kupambazuka na kufundisha. Lakini, kuhani mkuu alikuja na wote waliokuwa naye, na kuitisha baraza lote kwa pamoja, na wazee wote wa watu wa Israeli, na kuwatuma gerezani ili kuwaleta mitume.
Après avoir entendu cela, ils entrèrent dans le temple vers l'aube et enseignèrent. Mais le grand prêtre et ceux qui étaient avec lui vinrent convoquer le conseil, avec tout le sénat des enfants d'Israël, et envoyèrent à la prison pour les faire amener.
22 Lakini watumishi waliokwenda, hawakuwakuta gerezani, walirudi na kutoa taarifa,
Mais les officiers qui étaient venus ne les trouvèrent pas dans la prison. Ils revinrent et firent ce rapport:
23 “Tumekuta gereza limefungwa vizuri salama, na walinzi wamesimama langoni, lakini tulipokuwa tukifungua, hatukuona mtu ndani.”
« Nous avons trouvé la prison fermée et verrouillée, et les gardes debout devant les portes; mais quand nous les avons ouvertes, nous n'avons trouvé personne à l'intérieur! ».
24 Sasa wakati jemedari wa hekalu na makuhani wakuu waliposikia maneno haya, waliingiwa na shaka kubwa kwa ajili yao wakiwaza litakuwaje jambo hili.
Or, lorsque le grand prêtre, le commandant du temple et les chefs des prêtres entendirent ces paroles, ils furent très perplexes à leur sujet et sur ce qui pourrait en résulter.
25 Kisha mmoja akaja na kuwaambia, “Watu mliowaweka gerezani wamesimama hekaluni na wanafundisha watu.”
Quelqu'un vint leur dire: « Voici que les hommes que vous avez mis en prison sont dans le temple, debout et enseignant le peuple. »
26 Hivyo jemedari alienda pamoja na watumishi, na wakawaleta, lakini bila ya kufanya vurugu, kwa sababu waliwaogopa watu wangeweza kuwapiga kwa mawe.
Alors le capitaine alla avec les officiers et les ramena sans violence, car ils craignaient que le peuple ne les lapide.
27 Walipokwisha kuwaleta, waliwaweka mbele ya baraza. Kuhani mkuu aliwahoji
Quand ils les eurent amenés, ils les présentèrent au sanhédrin. Le grand prêtre les interrogea,
28 akisema, “Tuliwaamuru msifundishe kwa jina hili, na bado mmeijaza Yerusalemu kwa fundisho lenu, na kutamani kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
en disant: « Ne vous avons-nous pas strictement ordonné de ne pas enseigner en ce nom? Voici que vous avez rempli Jérusalem de votre enseignement, et vous avez l'intention de faire retomber sur nous le sang de cet homme. »
29 Lakini Petro na mitume wakajibu, “Lazima tumtii Mungu kuliko watu.
Mais Pierre et les apôtres répondirent: « Nous devons obéir à Dieu plutôt qu'aux hommes.
30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, mliyemuua, kwa kumtundika juu ya mti.
Le Dieu de nos pères a ressuscité Jésus, que vous avez tué en le pendant au bois.
31 Mungu alimtukuza katika mkono wake wa kuume, na kumfanya kuwa Mkuu na mwokozi, kutoa toba kwa Israeli, na msamaha wa dhambi.
Dieu l'a élevé par sa droite pour être Prince et Sauveur, pour donner la repentance à Israël et le pardon des péchés.
32 Sisi ni mashahidi wa mambo haya, na Roho Mtakatifu, ambaye Mungu amemtoa kwa wale wanaomtii.”
Nous sommes ses témoins de ces choses, ainsi que le Saint-Esprit, que Dieu a donné à ceux qui lui obéissent. »
33 Wajumbe wa baraza waliposikia hivi, walishikwa na hasira wakataka kuwaua mitume.
Mais eux, en entendant cela, eurent le cœur serré, et ils étaient résolus à les faire mourir.
34 Lakini pharisayo aliyeitwa Gamalieli, mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, alisimama na kuwaamuru mitume wachukuliwe nje kwa muda mfupi.
Mais quelqu'un se leva dans le sanhédrin, un pharisien nommé Gamaliel, docteur de la loi, honoré de tout le peuple, et ordonna de mettre les apôtres à l'écart pour un peu de temps.
35 Kisha akawaambia, “Wanaume wa Israeli, iweni makini sana na kile mnachopendekeza kuwafanyia watu hawa.
Il leur dit: « Hommes d'Israël, prenez garde à ces hommes, à ce que vous allez faire.
36 Kwa sababu, zamani zilizopita, Theuda aliinuka na kujidai kuwa mtu mkuu, na idadi ya watu, wapata mia nne walimfuata. Aliuawa, na wote waliokuwa wanamtii walitawanyika na kupotea.
Car, avant ces jours-ci, Theudas s'est levé, se faisant passer pour quelqu'un, et un certain nombre d'hommes, environ quatre cents, se sont joints à lui. Il fut tué, et tous ceux qui lui obéissaient furent dispersés et réduits à néant.
37 Baada ya mtu huyu, Yuda mgalilaya, aliinuka siku zile za kuandikwa sensa, akavuta watu wengi nyuma yake. Naye pia alipotea na wote waliokuwa wakimtii walitawanyika.
Après cet homme, Judas de Galilée se leva au temps de l'inscription, et il entraîna quelques personnes après lui. Lui aussi a péri, et tous ceux qui lui obéissaient ont été dispersés.
38 Sasa nawaambia, jiepusheni na watu hawa na muwaache wenyewe, kwa sababu, kama mpango huu au kazi hii ni ya watu itatupwa.
Maintenant, je vous le dis, retirez-vous de ces hommes et laissez-les tranquilles. Car si ce conseil ou cette œuvre est le fait des hommes, il sera renversé.
39 Lakini kama ni ya Mungu, hamtaweza kuwazuia; mnaweza mkajikuta hata mnashindana na Mungu.” Hivyo, walishawishika na maneno yake.
Mais si elle est de Dieu, vous ne pourrez pas la renverser, et l'on trouverait même que vous luttez contre Dieu! ».
40 Kisha, waliwaita mitume ndani na kuwachapa na kuwaamuru wasinene kwa jina la Yesu, na wakawaacha waende zao.
Ils furent d'accord avec lui. Ils convoquèrent les apôtres, les battirent, leur ordonnèrent de ne pas parler au nom de Jésus, et les relâchèrent.
41 Waliondoka mbele ya baraza wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuteseka na kutoheshimiwa kwa ajili ya Jina hilo.
Ils s'éloignèrent donc de la présence du sanhédrin, se réjouissant d'avoir été jugés dignes de subir l'opprobre pour le nom de Jésus.
42 Kwa hiyo, kila siku, ndani ya hekalu na kutoka nyumba hadi nyumba waliendelea kufundisha na kuhubiri Yesu kuwa ni Masihi.
Chaque jour, dans le temple et dans les foyers, ils ne cessaient d'enseigner et de prêcher Jésus, le Christ.

< Matendo 5 >