< Matendo 17 >

1 Na walipopita katika miji ya Amfipoli na Apolonia, walikuja mpaka mji wa Thesalonike ambao kulikuwa na sinagogi la Wayahudi.
Après avoir passé par Amphipolis et Apollonie, ils arrivèrent à Thessalonique, où il y avait une synagogue juive.
2 Kama ilivyo kawaida ya Paulo, alienda kwao, na kwa muda wa siku tatu za Sabato alijadiliana nao juu ya maandiko.
Paul, selon sa coutume, entra chez eux; et, pendant trois sabbats, il discuta avec eux d'après les Écritures,
3 Alikuwa akiwafungulia maandiko na kuwaeleza kuwa, ilimpasa Kristo ateseke na kisha kufufuka tena kutoka kwa wafu. Aliwaambia, “Huyu Yesu ninayewaambia habari zake ndiye Kristo”
expliquant et démontrant que le Christ devait souffrir et ressusciter des morts, et disant: « Ce Jésus, que je vous annonce, est le Christ. »
4 Baadhi ya Wayahudi walishawishika na kuungana na Paulo na Sila, pamoja na Wagiriki wachamungu, akinamama wengi waongofu na kundi kubwa la watu.
Quelques-uns d'entre eux se laissèrent convaincre et se joignirent à Paul et à Silas; parmi les Grecs pieux, une grande foule, et plusieurs femmes de confiance.
5 Lakini baadhi ya Wayahudi wasioamini, waliojawa na wivu, walienda sokoni na kuwachukuwa baadhi ya watu waovu, wakakusanya umati wa watu pamoja, na kusababisha ghasia mjini, kisha wakaivamia nyumba ya Jason, wakitaka kuwakamata Paulo na Sila ilikuwaleta mbele za watu.
Mais les Juifs, qui n'étaient pas convaincus, prirent avec eux quelques méchants hommes de la place et, rassemblant une foule, mirent la ville en émoi. Assaillant la maison de Jason, ils cherchaient à les faire sortir devant le peuple.
6 Lakini walipowakosa, walimkamata Yasoni na baadhi ya ndugu wengine na kuwapeleka mbele ya maofisa wa mji, wakipiga kelele, “Hawa wanaume walioupindua ulimwengu wamefika mpaka huku pia,
Ne les ayant pas trouvés, ils traînèrent Jason et quelques frères devant les chefs de la ville, en s'écriant: « Ceux qui ont mis le monde sens dessus dessous sont aussi venus ici,
7 Wanaume hawa waliokaribishwa na Yasoni wanaihalifu sheria ya Kaisari, wanasema kuna mfalme mwingine anayeitwa Yesu”
et Jason les a reçus. Tous ceux-là agissent contrairement aux décrets de César, en disant qu'il y a un autre roi, Jésus! »
8 Umati na maofisa wa mji waliposikia mambo hayo, waliingiwa na wasiwasi.
La foule et les chefs de la ville furent troublés en entendant ces choses.
9 Baada ya kuwa wamekwisha kuchukua fedha ya thamani ya ulinzi kutoka kwa Yason na wengine, waliwaachia waende.
Après avoir pris la garantie de Jason et des autres, ils les laissèrent partir.
10 Usiku ule ndugu walimtuma Paulo na Sila Beroya. Na walipofika kule walikwenda katika sinagogi la Wayahudi.
Les frères envoyèrent aussitôt Paul et Silas, de nuit, à Béroé. Lorsqu'ils arrivèrent, ils entrèrent dans la synagogue juive.
11 Watu wale walikuwa wenye werevu mkubwa kuliko wale watu wa Thesalonike, kwa sababu walikuwa na utayari wa kulipokea neno kwa akili zao, na kuchunguza maandiko kila siku ili kuona kama maneno yaliyonenwa ndivyo yalivyo.
Or, ces gens-là étaient plus nobles que ceux de Thessalonique, en ce qu'ils recevaient la parole avec une entière disponibilité d'esprit, examinant chaque jour les Écritures pour voir si ces choses étaient vraies.
12 Kwa hiyo wengi wao waliamini, wakiwemo wanawake wenye ushawishi mkubwa wa Kigiriki na wanaume wengi.
Plusieurs d'entre eux crurent donc, ainsi que des femmes grecques éminentes, et beaucoup d'hommes.
13 Lakini Wayahudi wa Thesalonike walipogundua kwamba Paulo anatangaza neno la Mungu huko Beroya, walienda huko na kuchochea na kisha kuanzisha ghasia kwa watu.
Mais, lorsque les Juifs de Thessalonique eurent appris que la parole de Dieu avait été annoncée par Paul à Béroé aussi, ils y vinrent aussi, agitant la foule.
14 Kwa haraka, ndugu wakampeleka Paulo kwa njia ya ziwa, lakini Sila na Timotheo wakabaki pale.
Alors les frères envoyèrent aussitôt Paul se rendre jusqu'à la mer, tandis que Silas et Timothée restaient sur place.
15 Wale ndugu waliompeleka Paulo walienda naye hadi Athene, walipomwacha Paulo huko, walipokea maagizo kutoka kwake kuwa, Sila na Timotheo waje kwake kwa haraka iwezeanavyo.
Mais ceux qui escortaient Paul le conduisirent jusqu'à Athènes. Ayant reçu l'ordre de Silas et de Timothée de venir très vite auprès de lui, ils partirent.
16 Na wakati akiwasubiri huko Athene, roho yake ilikasirishwa ndani yake kwa jinsi alivyouona mji ulivyojaa sanamu nyingi.
Pendant que Paul les attendait à Athènes, son esprit s'enflammait au-dedans de lui, lorsqu'il voyait la ville pleine d'idoles.
17 Hivyo akajadiliana katika sinagogi na wayahudi wale waliomcha Mungu na kwa wale wote aliokutana nao kila siku sokoni.
Il discutait donc dans la synagogue avec les Juifs et les personnes pieuses, et chaque jour sur la place publique avec ceux qui le rencontraient.
18 Lakini baathi ya Wanafalsafa wa Waepikureo na Wastoiko wakamkabili. Na wengine wakasema, “Ni nini anachokisema huyu mwongeaji mchanga? Wengine wakasema, “inaonekana anahubiri habari ya mungu mgeni,” kwasababu anahubiri habari ya Yesu na ufufuo.
Quelques-uns des philosophes épicuriens et stoïciens s'entretenaient aussi avec lui. Les uns disaient: « Que veut dire ce bavard? » D'autres ont dit: « Il semble prôner des divinités étrangères », car il prêchait Jésus et la résurrection.
19 Wakamchukua Paulo na kumleta Areopago, wakisema, “Twaweza kujua haya mafundisho mapya unayoyaongea?
Ils se saisirent de lui et l'amenèrent à l'Aréopage, en disant: « Pouvons-nous savoir quelle est cette nouvelle doctrine dont tu parles?
20 Kwasababu unaleta mambo mapya katika masikio yetu. Kwahivyo tunataka kujua haya mambo yana maana gani?”
Car tu fais entendre à nos oreilles des choses étranges. Nous voulons donc savoir ce que ces choses signifient. »
21 (Na watu wote wa Athene pamoja na wageni waliopo kwao, hutumia muda wao aidha katika kuongea na kusikiliza juu ya jambo jipya.)
Or, tous les Athéniens et les étrangers qui habitaient là ne passaient leur temps qu'à raconter ou à entendre quelque chose de nouveau.
22 Kwa hiyo Paulo akasimama katikati ya watu wa Areopago na kusema, “Enyi watu wa Athene, naona kuwa ninyi ni watu wa dini kwa kila namna,
Paul, debout au milieu de l'Aréopage, dit: Hommes d'Athènes, je vois que vous êtes très religieux à tous égards.
23 Kwani katika kupita kwangu na kuangalia vitu vyenu vya kuabudu, nimeona maneno yalioandikwa kwenye moja ya madhabahu yenu, ikisema “KWA MUNGU ASIYEJULIKANA”. Hivyo basi, huyo mnayemwabudu pasipokujua, ndiye ninayewajulisha ninyi.
En effet, en passant et en observant les objets de votre culte, j'ai trouvé un autel portant cette inscription: « A UN DIEU INCONNU »; je vous annonce donc ce que vous adorez par ignorance.
24 Mungu aliyeumba dunia na kila kitu kilichoko ndani, kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hawezi kukaa katika mahekalu yaliyotengenezwa na mikono.
Le Dieu qui a fait le monde et tout ce qui s'y trouve, lui qui est le Seigneur du ciel et de la terre, n'habite pas dans des temples faits de main d'homme.
25 Na pia hatumikiwi na mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji kitu kwao, kwani yeye mwenyewe huwapa watu uzima na pumzi na vitu vingine vyote.
Il n'est pas servi par des mains d'hommes, comme s'il avait besoin de quelque chose, puisqu'il donne lui-même à tous la vie, le souffle et toutes choses.
26 Kupitia mtu mmoja, alifanya mataifa yote ya watu waishio juu ya uso wa dunia, na akawawekea nyakati na mipaka katika maeneo wanaoishi.
Il a créé d'un seul sang toutes les nations d'hommes pour qu'elles habitent sur toute la surface de la terre, en fixant les saisons et les limites de leurs habitations,
27 Kwa hiyo, wanatakiwa kumtafuta Mungu, na yamkini wamfikie na kumpata, na kwa uhakika hayupo mbali na kila mmoja wetu.
afin qu'elles cherchent le Seigneur, si peut-être elles pouvaient l'atteindre et le trouver, bien qu'il ne soit pas loin de chacun de nous.
28 Kwake tunaishi, tunatembea na kuwa na uzima wetu, kama vile mtunzi wenu mmoja wa shairi aliposema 'tu wazaliwa wake.'
Car c'est en lui que nous vivons, que nous nous mouvons et que nous avons notre existence. Comme l'ont dit certains de vos poètes: « Car nous sommes aussi sa descendance ».
29 Kwa hiyo, ikiwa sisi ni wazaliwa wa Mungu, hatupaswi kufikiri kuwa uungu ni kama dhahabu, au shaba, au mawe, sanamu iliyochongwa kwa ustadi na mawazo ya watu.
Étant donc la progéniture de Dieu, nous ne devons pas penser que la nature divine soit semblable à de l'or, de l'argent ou de la pierre, gravés par l'art et le dessein de l'homme.
30 Kwa hiyo, Mungu alinyamazia nyakati zile za ujinga, lakini sasa anaamuru watu wote kila mahali wapate kutubu.
Dieu a donc négligé les temps d'ignorance. Mais maintenant il ordonne que tous les hommes, en tout lieu, se repentent,
31 Hii ni kwa sababu ameweka siku atakayo ihukumu dunia kwa haki kwa mtu ambaye alimchagua. Mungu alitoa uhakika wa mtu huyu kwa kila mtu pale alipomfufua katoka kwa wafu.
parce qu'il a fixé un jour où il jugera le monde selon la justice, par l'homme qu'il a désigné, et dont il a donné l'assurance à tous les hommes qu'il l'a ressuscité des morts. »
32 Na watu wa Athene waliposikia habari ya kufufuliwa kwa wafu, baadhi yao wakamdhihaki Paulo, ila wengine wakasema “Tutakusikiliza tena kwa habari ya jambo hili”
Lorsqu'ils entendirent parler de la résurrection des morts, les uns se moquèrent; mais les autres dirent: « Nous voulons t'entendre encore à ce sujet. »
33 Baada ya hapo, Paulo akawaacha.
Paul se retira donc du milieu d'eux.
34 Lakini baadhi ya watu waliungana naye wakaamini, akiwemo Dionisio Mwareopago, na Mwanamke anaitwa Damari na wengine pamoja nao.
Mais quelques hommes se joignirent à lui et crurent, entre autres Denys l'Aréopagite, et une femme nommée Damaris, et d'autres avec eux.

< Matendo 17 >