< Matendo 16 >

1 Paulo pia alipokuja Derbe na Lystra; na tazama, pale palikuwepo na mwanafunzi aitwaye Timotheo, ni Kijana aliyezaliwa na mama wa Kiyahudi ambaye ni muumini na baba yake ni Mgiriki.
Il arriva à Derbe et à Lystre. Et voici, il y avait là un disciple nommé Timothée, fils d'une Juive croyante, mais dont le père était Grec.
2 Watu wa Listra na Ikonia walimshudia vizuri.
Les frères qui étaient à Lystre et à Iconium rendaient sur lui un bon témoignage.
3 Paulo alimtaka ili asafiri naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwako huko kwani wote walimjua kuwa baba yake ni Mgiriki.
Paul voulut l'emmener avec lui, et il le prit et le circoncit, à cause des Juifs qui étaient dans ces contrées; car tous savaient que son père était grec.
4 Walipokuwa wakienda walipita kwenye miji na kutoa maagizo kwa makanisa ili kuyatii maagizo hayo yaliandikwa na mitume na wazee huko Yerusalemu.
Pendant qu'ils traversaient les villes, ils leur remettaient les décrets à observer, qui avaient été ordonnés par les apôtres et les anciens qui étaient à Jérusalem.
5 Hivyo makanisa yakaimarishwa katika imani na walioamini wakaongezeka kwa idadi kila siku.
Les assemblées étaient ainsi fortifiées dans la foi, et leur nombre augmentait chaque jour.
6 Paulo na mwenzake wakaenda Firigia na Galatia, kwani Roho wa Mungu aliwakataza kuhubiri neno huko kwenye jimbo la Asia.
Lorsqu'ils eurent traversé la région de la Phrygie et de la Galatie, l'Esprit Saint leur interdit d'annoncer la parole en Asie.
7 Walipokaribia Misia, walijaribu kwenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu akawakataza.
Arrivés en face de la Mysie, ils essayèrent d'aller en Bithynie, mais l'Esprit ne le leur permit pas.
8 Kwa hiyo wakapita Misia wakaja mpaka Mji wa Troa.
Passant par Mysia, ils descendirent à Troas.
9 Maono yalimtokea Paulo usiku, kulikuwa na mtu wa Makedonia amesimama, akimwita na kusema “Njoni mtusaidie huku Makedonia”.
Une vision apparut à Paul pendant la nuit. Il y avait là un homme de Macédoine, qui le suppliait et lui disait: « Passe en Macédoine et aide-nous. »
10 Paulo alipoona maono, mara tukajiandaa kwenda Makedonia, akijua kwamba Mungu alituita kwenda kuwahubiria injili.
Après avoir eu cette vision, nous cherchâmes aussitôt à nous rendre en Macédoine, concluant que le Seigneur nous avait appelés à leur annoncer la Bonne Nouvelle.
11 Hivyo tukaondoka kutoka Troa, tukaenda moja kwa moja Samothrake, na siku iliyofuata tukafika mji wa Neapoli.
Partant donc de Troas, nous fîmes route directe vers Samothrace, puis le lendemain vers Néapolis,
12 Kutoka hapo tukaenda Filipi ambao ni moja ya mji wa Makedonia, mji muhimu katika wilaya na utawala wa Kirumi na tukakaa siku kadhaa.
et de là vers Philippes, ville de Macédoine, la plus importante du district, colonie romaine. Nous séjournâmes quelques jours dans cette ville.
13 Siku ya Sabato, tulikwenda nje ya lango kwa njia ya mto, sehemu ambayo tulidhania kutakuwa na mahali pa kufanyia maombi. Tulikaa chini na kuongea na akinamama waliokuja pamoja.
Le jour du sabbat, nous nous rendîmes hors de la ville, au bord d'un fleuve, où nous pensions qu'il y avait un lieu de prière, et nous nous assîmes pour parler aux femmes qui s'étaient rassemblées.
14 Mwanamke mmoja aitwaye Lidia, muuzaji wa zambarau, kutoka katika mji wa Tiatira, mwenye kumwabudu Mungu, alitusikiliza. Bwana alimfungua moyo wake na kuweka maanani maneno yaliyosemwa na Paulo.
Une femme nommée Lydie, vendeuse de pourpre, de la ville de Thyatire, qui adorait Dieu, nous écouta. Le Seigneur lui ouvrit le cœur pour qu'elle écoute ce que disait Paul.
15 Baada ya kubatizwa, yeye na nyumba yake yote, alitusihi akisema “kama mmeniona kuwa mimi ni mwaminifu katika Bwana, basi nawasihi muingie na kukaa kwangu”. Akatusihi sana.
Lorsqu'elle fut baptisée avec sa famille, elle nous supplia en disant: « Si vous m'avez jugée fidèle au Seigneur, venez dans ma maison et restez-y. » Elle nous a donc persuadés.
16 Ikawa kwamba, tulipokuwa tunaenda mahali pa kuomba, msichana mmoja aliyekuwa na pepo la utambuzi akakutana nasi. Alimletea bwana wake faida nyingi kwa kubashiri.
Comme nous allions prier, nous rencontrâmes une jeune fille douée d'un esprit de divination, qui rapportait beaucoup à ses maîtres en leur disant la bonne aventure.
17 Mwanamke huyu alimfuata Paulo pamoja na sisi, akipiga kelele na kusema “Hawa wanaume ni watumishi wa Mungu aliye Mkuu, wanaowatangazia ninyi habari ya wokovu”.
Suivant Paul et nous, elle s'écriait: « Ces hommes sont des serviteurs du Dieu Très-Haut, qui nous annoncent un chemin de salut! »
18 Alifanya hivyo kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa amekasirishwa na tendo hilo, aligeuka nyuma na kumwambia pepo, “Nakuamuru kwa Jina la Yesu umtoke ndani yake.” Naye akatoka na kumwacha mara moja.
Elle a agi ainsi pendant plusieurs jours. Mais Paul, très irrité, se retourne et dit à l'esprit: « Je t'ordonne, au nom de Jésus-Christ, de sortir d'elle. » Il sortit à l'heure même.
19 Mabwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limeondoka, waliwakamata Paulo na Sila na kuwaburuza sokoni mbele ya wenye mamlaka.
Mais, voyant que l'espoir de gain avait disparu, ses maîtres se saisirent de Paul et de Silas et les traînèrent sur la place publique devant les magistrats.
20 Walipowafikisha kwa mahakimu, walisema, “Hawa wanaume ni Wayahudi na wanasababisha ghasia kubwa katika mji wetu.
Les ayant amenés devant les magistrats, ceux-ci dirent: « Ces hommes, qui sont Juifs, agitent notre ville
21 Wanafundisha mambo ambayo siyo sheria sisi kuyapokea wala kuyafuata kama Warumi.”
et préconisent des coutumes qu'il ne nous est pas permis d'accepter ni d'observer, étant Romains. »
22 Umati ukawainukia kinyume Paulo na Sila, mahakimu wakararua nguo zao na kuwavua na kuamuru wachapwe viboko
La foule se souleva contre eux et les magistrats leur arrachèrent leurs vêtements, puis ils ordonnèrent qu'on les batte avec des verges.
23 Baada ya kuwachapa viboko vingi, waliwatupa gerezani na kumuamuru askari wa gereza kuwalinda vyema.
Après leur avoir fait subir de nombreux coups de verges, ils les jetèrent en prison, en chargeant le geôlier de les garder en sécurité.
24 Baada ya kupokea amri hiyo, askari wa gereza aliwatupa katika chumba cha ndani ya gereza na kuwafunga miguu yao kwenye sehemu alipowahifadhi.
Ayant reçu cet ordre, il les jeta dans la prison intérieure et leur fixa les pieds dans les ceps.
25 Wakati wa usiku wa manane, Paulo na Sila wakawa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwasikiliza,
Vers minuit, Paul et Silas priaient et chantaient des cantiques à Dieu, et les prisonniers les écoutaient.
26 Ghafla kukatokea tetemeko kuu na misingi ya gereza ikatikiswa, milango ya gereza ikafunguka, na minyororo ya wafungwa wote ikalegezwa.
Tout à coup, il se fit un grand tremblement de terre, en sorte que les fondements de la prison furent ébranlés; à l'instant même, toutes les portes s'ouvrirent, et les liens de chacun furent rompus.
27 Mlinzi wa Gereza aliamka kutoka usingizini na akaona milango yote ya gereza imefunguliwa; hivyo akachukua upanga wake maana alitaka kujiua kwa sababu alifikiri wafungwa wote walikwishatoroka,
Le geôlier, réveillé par le sommeil et voyant les portes de la prison ouvertes, tira son épée et allait se tuer, pensant que les prisonniers s'étaient échappés.
28 Lakini, Paulo akapiga kelele kwa sauti kuu, akisema “usijidhuru kwa sababu wote tuko mahali hapa”.
Mais Paul cria d'une voix forte: « Ne te fais pas de mal, car nous sommes tous ici. »
29 Mlinzi wa gereza aliomba taa ziletwe na akaingia ndani ya gereza kwa haraka, akitetemeka na kuogopa, akawaangukia Paulo na Sila,
Il demanda des lumières, entra, se jeta en tremblant devant Paul et Silas,
30 na kuwatoa nje ya gereza na kusema, “Waheshimiwa, nifanye nini ili nipate kuokoka?”
les fit sortir, et dit: « Messieurs, que dois-je faire pour être sauvé? »
31 Nao wakamwambia, “Mwamini Bwana Yesu nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.”
Ils dirent: « Crois au Seigneur Jésus-Christ, et tu seras sauvé, toi et ta famille. »
32 Walinena neno la Bwana kwake, pamoja na watu wote wa nyumbani kwake,
Ils lui annoncèrent la parole du Seigneur, ainsi qu'à tous ceux qui étaient dans sa maison.
33 Mlinzi wa gereza aliwachukua usiku ule na kuwaosha sehemu walizoumia, yeye pamoja na watu wa nyumbani mwake wakabatizwa mara.
Il les prit à l'heure même de la nuit, lava leurs plaies, et fut aussitôt baptisé, lui et toute sa famille.
34 Akawaleta Paulo na Sila nyumbani kwake na kuwatengea chakula. Naye akawa na furaha kuu pamoja na watu wa nyumbani mwake kwa sababu walimwamini Mungu.
Il les fit monter dans sa maison, leur servit à manger, et se réjouit beaucoup avec toute sa famille, parce qu'ils avaient cru en Dieu.
35 Ilipokuwa mchana, mahakimu walituma ujumbe kwa yule mlinzi wa gereza wakisema, “Waruhusu wale watu waende”,
Mais quand le jour fut venu, les magistrats envoyèrent les sergents dire: « Laissez partir ces hommes. »
36 Mlinzi wa gereza akamjulisha Paulo juu ya maneno hayo ya kuwa, “Mahakimu walituma ujumbe niruhusu mwondoke: hivyo tokeni nje na mwende kwa amani.”
Le geôlier rapporta ces paroles à Paul, en disant: « Les magistrats ont envoyé te relâcher; sors donc et va en paix. »
37 Lakini Paulo akawaambia, “Walitupiga hadharani, watu ambao ni Warumi bila kutuhukumu na waliamua kututupa gerezani; halafu sasa wanataka kututoa kwa siri? Hapana, haitawezekana, wao wenyewe waje kututoa mahali hapa”.
Mais Paul leur dit: « Ils nous ont battus publiquement sans jugement, des Romains, et ils nous ont jetés en prison! Vont-ils maintenant nous libérer secrètement? Non, très certainement, mais qu'ils viennent eux-mêmes et nous fassent sortir! ».
38 Walinzi wakawajulisha mahakimu juu ya maneno hayo, mahakimu wakaogopa sana pale walipojua kuwa Paulo na Sila ni Warumi.
Les sergents rapportèrent ces paroles aux magistrats, qui furent effrayés d'apprendre que c'étaient des Romains,
39 Mahakimu wakaja na kuwasihi watoke, na walipowatoa nje ya gereza, waliwaomba Paulo na Sila watoke nje ya mji wao.
et ils vinrent les supplier. Lorsqu'ils les eurent fait sortir, ils les prièrent de quitter la ville.
40 Kwa hiyo Paulo na Sila wakatoka nje ya gereza wakaja nyumbani kwa Lidia. Paulo na Sila walipowaona ndugu, waliwatia moyo na kisha kuondoka katika mji huo.
Ils sortirent de la prison et entrèrent dans la maison de Lydie. Après avoir vu les frères, ils les encouragèrent, puis ils partirent.

< Matendo 16 >