< Matendo 13 >

1 Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
Or, dans l'assemblée qui était à Antioche, il y avait quelques prophètes et docteurs: Barnabas, Siméon appelé Niger, Lucius de Cyrène, Manaen, frère adoptif d'Hérode le tétrarque, et Saul.
2 Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
Comme ils servaient le Seigneur et jeûnaient, le Saint-Esprit dit: « Mettez-moi à part Barnabas et Saul, pour l'œuvre à laquelle je les ai appelés. »
3 Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
Puis, après avoir jeûné et prié, et leur avoir imposé les mains, ils les renvoyèrent.
4 Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
Ainsi, après avoir été envoyés par le Saint-Esprit, ils descendirent à Séleucie. De là, ils s'embarquèrent pour l'île de Chypre.
5 Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
Arrivés à Salamine, ils annoncèrent la parole de Dieu dans les synagogues juives. Ils avaient aussi Jean comme assistant.
6 Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
Après avoir traversé l'île jusqu'à Paphos, ils trouvèrent un sorcier, un faux prophète, un Juif qui s'appelait Bar Jésus,
7 Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
qui était avec le proconsul Sergius Paulus, un homme intelligent. Cet homme convoqua Barnabas et Saul, et chercha à entendre la parole de Dieu.
8 Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
Mais Elymas le sorcier (car c'est ainsi que s'appelle son nom selon l'interprétation) leur opposa une résistance, cherchant à détourner le proconsul de la foi.
9 Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
Mais Saul, qu'on appelle aussi Paul, rempli du Saint-Esprit, fixa les yeux sur lui
10 na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
et dit: « Fils du diable, plein de toute espèce de tromperie et de ruse, ennemi de toute justice, ne cesseras-tu pas de pervertir les voies droites du Seigneur?
11 Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
Maintenant, voici que la main du Seigneur est sur toi, et tu seras aveugle, tu ne verras pas le soleil pendant un certain temps! ». Immédiatement, un brouillard et des ténèbres se sont abattus sur lui. Il allait et venait, cherchant quelqu'un pour le conduire par la main.
12 Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
Alors le proconsul, voyant ce qui s'était passé, crut, étant étonné de l'enseignement du Seigneur.
13 Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
Paul et sa troupe partirent de Paphos et arrivèrent à Perga, en Pamphylie. Jean se sépara d'eux et retourna à Jérusalem.
14 Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
Eux, en partant de Perge, se rendirent à Antioche de Pisidie. Ils entrèrent dans la synagogue le jour du sabbat et s'assirent.
15 Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
Après la lecture de la loi et des prophètes, les chefs de la synagogue leur envoyèrent dire: « Frères, si vous avez quelque parole d'exhortation pour le peuple, parlez. »
16 Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
Paul se leva, et, faisant un geste de la main, il dit: « Hommes d'Israël, et vous qui craignez Dieu, écoutez.
17 Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
Le Dieu de ce peuple a choisi nos pères, il a exalté le peuple lorsqu'il séjournait comme étranger dans le pays d'Égypte et, le bras levé, il l'a fait sortir de ce pays.
18 Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
Pendant une période d'environ quarante ans, il les a supportés dans le désert.
19 Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
Quand il eut détruit sept nations au pays de Canaan, il leur donna leur pays en héritage pendant environ quatre cent cinquante ans.
20 Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
Après cela, il leur donna des juges jusqu'à Samuel le prophète.
21 Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
Ensuite, ils demandèrent un roi, et Dieu leur donna Saül, fils de Kish, homme de la tribu de Benjamin, pendant quarante ans.
22 Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
Après l'avoir destitué, il leur suscita David comme roi, auquel il rendit ce témoignage: « J'ai trouvé David, fils de Jessé, un homme selon mon cœur, qui fera toute ma volonté.
23 Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
C'est de la descendance de cet homme que Dieu a apporté le salut à Israël, conformément à sa promesse,
24 Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
avant sa venue, lorsque Jean avait d'abord prêché le baptême de repentance à Israël.
25 Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
Comme Jean accomplissait sa tâche, il dit: « Que supposez-vous que je sois? Je ne suis pas lui. Mais voici que quelqu'un vient après moi, et je ne suis pas digne de délier les sandales de ses pieds ».
26 Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
« Frères, enfants de la souche d'Abraham, et ceux d'entre vous qui craignent Dieu, la parole de ce salut vous est adressée.
27 Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
Car les habitants de Jérusalem et leurs chefs, parce qu'ils ne l'ont pas connu, ni les voix des prophètes qu'on lit chaque sabbat, les ont accomplies en le condamnant.
28 Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
Bien qu'ils ne trouvassent aucune cause de mort, ils demandaient encore à Pilate de le faire mourir.
29 Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
Lorsqu'ils eurent accompli tout ce qui était écrit sur lui, ils le descendirent du bois et le déposèrent dans un sépulcre.
30 Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
Mais Dieu l'a ressuscité des morts,
31 Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
et il a été vu pendant plusieurs jours par ceux qui étaient montés avec lui de la Galilée à Jérusalem, et qui sont ses témoins auprès du peuple.
32 Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
Nous vous annonçons la bonne nouvelle de la promesse faite aux pères,
33 Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
que Dieu a accomplie pour nous, leurs enfants, en ressuscitant Jésus. Comme il est aussi écrit dans le deuxième psaume, « Tu es mon fils. Aujourd'hui, je suis devenu votre père.
34 Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
« En ce qui concerne le fait qu'il l'a ressuscité d'entre les morts, pour qu'il ne retourne plus à la corruption, il a parlé ainsi: 'Je te donnerai les bénédictions saintes et sûres de David'.
35 Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
C'est pourquoi il dit aussi dans un autre psaume: « Tu ne permettras pas que ton Saint voie la corruption.
36 Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
Car David, après avoir, dans sa génération, servi le conseil de Dieu, s'est endormi, a été couché avec ses pères et a vu la décadence.
37 Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
Mais celui que Dieu a élevé n'a pas vu la décadence.
38 Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
Sachez donc, frères, que par cet homme vous est annoncée la rémission des péchés;
39 Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
et que par lui quiconque croit est justifié de toutes les choses dont vous ne pouviez être justifiés par la loi de Moïse.
40 Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
Prenez donc garde que ne vienne sur vous ce qui est annoncé par les prophètes:
41 'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
« Voyez, moqueurs! S'émerveiller et périr, car je fais une œuvre dans vos jours, un ouvrage que vous ne croirez nullement, si on vous le déclare. »
42 Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
Les Juifs étant sortis de la synagogue, les païens demandèrent que ces paroles leur fussent annoncées le sabbat suivant.
43 Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
A la fin de la synagogue, beaucoup de Juifs et de prosélytes pieux suivirent Paul et Barnabas, qui, leur parlant, les exhortèrent à persévérer dans la grâce de Dieu.
44 Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
Le sabbat suivant, presque toute la ville était rassemblée pour entendre la parole de Dieu.
45 Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
Mais les Juifs, voyant la foule, furent remplis de jalousie, contredirent les paroles de Paul et blasphémèrent.
46 Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios g166)
Paul et Barnabé prirent la parole avec audace et dirent: « Il fallait que la parole de Dieu vous soit d'abord annoncée. Puisque vous l'avez repoussée de vous-mêmes et que vous vous jugez indignes de la vie éternelle, voici que nous nous tournons vers les païens. (aiōnios g166)
47 Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
Car c'est ainsi que le Seigneur nous l'a ordonné, en disant, Je t'ai mis en lumière pour les païens, afin que tu apportes le salut aux extrémités de la terre. »
48 Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios g166)
Les païens, ayant entendu cela, se réjouirent et glorifièrent la parole de Dieu. Tous ceux qui étaient destinés à la vie éternelle crurent. (aiōnios g166)
49 Neno la Bwana lilienea nchi yote.
La parole du Seigneur se répandit dans toute la région.
50 Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
Mais les Juifs, soulevant les femmes pieuses et les notables, ainsi que les principaux hommes de la ville, excitèrent une persécution contre Paul et Barnabas, et les chassèrent de leur territoire.
51 Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
Mais ils secouèrent contre eux la poussière de leurs pieds, et arrivèrent à Iconium.
52 Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.
Les disciples furent remplis de joie et du Saint-Esprit.

< Matendo 13 >