< 2 Wafalme 1 >

1 Moabu aliasi dhidi ya Israeli baada ya kifo cha Ahabu.
And Moab transgresseth against Israel after the death of Ahab,
2 Baada hapo Ahazi akaanguka chini ya dirisha lenye waya zinazikinzana kwenye chumba chake juu katika Samaria, na alikuwa amejeruhiwa. Kwa hiyo alituma wajumbe na kuwaambia, “Nendeni, muulizeni Baal Zebubu, mungu wa Ekroni, kama nitapona hili jeraha.”
and Ahaziah falleth through the lattice in his upper chamber that [is] in Samaria, and is sick, and sendeth messengers, and saith unto them, 'Go ye, inquire of Baal-Zebub god of Ekron if I recover from this sickness.'
3 Lakini malaika wa Yahwe wakamwambia Eliya Mtishbi, “Inuka, nenda ukaonane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, na uwaulize, 'Je ni kwasababu hakuna Mungu katika israeli ambaye mnayekwenda kuuliza pamoja na Zebebu, mungu wa Ekroni?
And a messenger of Jehovah hath spoken unto Elijah the Tishbite, 'Rise, go up to meet the messengers of the king of Samaria, and speak unto them, Is it because there is not a God in Israel — ye are going to inquire of Baal Zebub god of Ekron?
4 Kwa hiyo Yahwe anasema, “Hutaweza kushuka chini kutoka kwenye kitanda ambacho ulichokipanda; badala yake, utakufa hakika."”” Baada ya hapo Eliya akaondoka.
and therefore, thus said Jehovah, The bed whither thou hast gone up, thou dost not come down from it, for thou dost certainly die;' and Elijah goeth on.
5 wakati wale wajumbe waliporudi kwa Ahazia, akawaambia, “Kwa nini mmerudi?”
And the messengers turn back unto him, and he saith unto them, 'What [is] this — ye have turned back!'
6 Wakamwambia, “mtu amekuja kuonana na sisi ambaye ametuambia, 'Turudi kwa mfalme ambaye aliyewatuma, na mkamwambie, Yahwe amesema hivi: 'Je ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli mpaka mmewatuma watu kwenda kumuuliza kwa Baal Zabubu, mungu wa Ekron? Kwa hiyo hutashuka kutoka kitanda ulichokipanda; badala yake, utakufa hakika."””
And they say unto him, 'A man hath come up to meet us, and saith unto us, Go, turn back unto the king who sent you, and ye have said unto him, Thus said Jehovah, Is it because there is not a God in Israel — thou art sending to inquire of Baal-Zebub god of Ekron? therefore, the bed whither thou hast gone up, thou dost not come down from it, for thou dost certainly die.'
7 Ahazi akawaambia wajumbe wake, “'Alikuwa mtu wa aina gani, yule ambaye alikuja kuonana na ninyi na akasema haya maneno kwenu?”
And he saith unto them, 'What [is] the fashion of the man who hath come up to meet you, and speaketh unto you these words?'
8 Wakamjibu, “Alikuwa amevaa kanzu yenye manyaya na alikuwa na mkanda wa ngozi kiunanoni kwake.'” Hivyo mfalme akajibu, '“Yule alikuwa Eliya Mtishbi.”
And they say unto him, 'A man — hairy, and a girdle of skin girt about his loins;' and he saith, 'He [is] Elijah the Tishbite.'
9 Ndipo mfalme akatuma nahodha wa askari hamsini kwa Elya. Nahodha akaenda mpaka kwa Eliya ambapo alipokuwa amekaa juu ya mlima. Nahodha akamwambia Eliya, “Wewe, mtu wa Mungu, mfalme amesema, 'shuka chini.'”
And he sendeth unto him a head of fifty and his fifty, and he goeth up unto him (and lo, he is sitting on the top of the hill), and he speaketh unto him, 'O man of God, the king hath spoken, Come down.'
10 Eliya akajibu na kusema kwa nahodha, “Kama mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke chini kutoka mbinguni na kukula wewe na watu wako hamsini.” Kisha moto ukashuka chini kutoka mbinguni na kumla yeye na watu wake hamsini.
And Elijah answereth and speaketh unto the head of the fifty, 'And if I [am] a man of God, fire doth come down from the heavens, and consume thee and thy fifty;' and fire cometh down from the heavens, and consumeth him and his fifty.
11 Tena Mfalme Ahazi akamtuma nahodha mwingine pamoja na maaskari wengine hamsini. Huyu nahodha pia akasema kwa Eliya, “Wewe, mtu wa Mungu, mfalme anasema, teremka chini haraka.”'
And he turneth and sendeth unto him another head of fifty and his fifty, and he answereth and speaketh unto him, 'O man of God, thus said the king, Haste, come down.'
12 Eliya akajibu na kuwaambia, “Kama mimi ni mtu wa Mungu, ngoja moto ushuke kutoka mbinguni na ukule wewe na watu wako hamsini.” Moto wa Mungu ukashuka chini tena kutoka mbinguni na kumla yeye na watu wake hamsini.
And Elijah answereth and speaketh unto them, 'If I [am] a man of God, fire doth come down from the heavens, and consume thee and thy fifty;' and fire of God cometh down from the heavens, and consumeth him and his fifty.
13 Bado tena mfalme alituma kundi la tatu la wapiganaji hamsini. Huyu nahodha akaenda, akaanguka mbele ya miguu ya Eliya, na kumsihi na kumwambia, “Wewe, mtu wa Mungu, Nakuomba, acha uzima wangu na uzima wa hawa watumishi wako hamsini uwe na thamani machoni kwako.
And he turneth and sendeth a third head of fifty and his fifty, and the third head of fifty goeth up, and cometh in, and boweth on his knees over-against Elijah, and maketh supplication unto him, and speaketh unto him, 'O man of God, let be precious, I pray thee, my soul and the soul of thy servants — these fifty — in thine eyes.
14 Ndipo, moto ukashuka chini kutoka mbinguni na kuwala wale manahodha wawili wa kwanza pamoja na watu wao, bali sasa acha uzima wangu uwe na thamani machoni kwako.”
Lo, come down hath fire from the heavens, and consumeth the two heads of the former fifties and their fifties; and, now, let my soul be precious in thine eyes.'
15 Malaika wa Yahwe akamwambia Eliya, “'Nenda chini pamoja naye. Usimwogope.”' Hivyo Eliya akainuka na kwenda chini pamoja naye kwenda kwa mfalme.
And a messenger of Jehovah speaketh unto Elijah, 'Go down with him, be not afraid of him;' and he riseth and goeth down with him unto the king,
16 Baadye Eliya akamwambia Ahazia, '“Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, Umewatuma wajumbe kuzungumza pamoja na Baal-Zebubu, mungu wa Ekron. Je ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ambaye unayeweza kumuuliza habari? Kwa hiyo sasa, hutaweza kushuka chini kutoka kwenye kitanda ulichokipanda; utakufa hakika.'”
and speaketh unto him, 'Thus said Jehovah, Because that thou hast sent messengers to inquire of Baal-Zebub god of Ekron — is it because there is not a God in Israel to inquire of His word? therefore, the bed whither thou hast gone up — thou dost not come down from it, for thou dost certainly die.'
17 Hivyo Mfalme Ahazia alikufa kulingana na neno la Yahwe ambalo Eliya alilisema. Yoramu alianza kutawala katika eneo lake, katika mwaka wa pili Yoramu mwana wa Yohoshafati mfalme wa Yuda, kwa sababu Ahazia hakuwa na mtoto.
And he dieth, according to the word of Jehovah that Elijah spake, and Jehoram reigneth in his stead, in the second year of Jehoram son of Jehoshaphat king of Judah, for he had no son.
18 Kama mambo mengine yanayomuhusu Ahazia, je hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
And the rest of the matters of Ahaziah that he did, are they not written on the book of the Chronicles of the kings of Israel?

< 2 Wafalme 1 >