< 2 Wafalme 7 >

1 Elisha akasema, “Sikiliza neno la Yahwe. Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kesho mda kama huu kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kwenye lango la Samaria.””
And Elisha saith, 'Hear ye a word of Jehovah: thus said Jehovah, About this time to-morrow, a measure of fine flour [is] at a shekel, and two measures of barley at a shekel, in the gate of Samaria.'
2 Basi yule nahodha ambaye alikuwa akitegemea mkono wake amemjibu mtu wa Mungu, na kusema, “Ona, hata kama Yahwe ataweka madirisha mbinguni, je jambo hili linawezekana?” Elisha akajibu, “Ona, utaona ikitokea kwa macho yako mwenyewe, lakini hutakula chochote katika hilo.”
And the captain whom the king hath, by whose hand he hath been supported, answereth the man of God and saith, 'Lo, Jehovah is making windows in the heavens — shall this thing be?' and he saith, 'Lo, thou art seeing it with thine eyes, and thereof thou dost not eat.'
3 Basi, kulikuwa na watu wanne wenye ukoma upande wa nje wa lango la mji. Wakaambizana kila mmoja, “Kwa nini tukae hapa hadi hapo tutakapokufa?
And four men have been leprous, at the opening of the gate, and they say one unto another, 'What — we are sitting here till we have died;
4 Kama tukisema kwamba tutaenda kwenye ule mji, maana mjini kuna njaa, na tutakufa hapo. Lakini kama tukiendelea kukaa hapa, bado tutakufa. Sawa, njoni, twendeni kwenye lile jeshi la Washami. Kama wakitupa uhai, tutakuwa hai, na kama wakituua, tutakufa tu.”
if we have said, We go in to the city, then the famine [is] in the city, and we have died there; and if we have sat here, then we have died; and now, come and we fall unto the camp of Aram; if they keep us alive, we live, and if they put us to death — we have died.'
5 Hivyo wakaamka asubuhi kabla giza halijaisha kwenda kwenye kambi ya Washami; Wakati walipofika sehemu ya mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu hapo.
And they rise in the twilight, to go in unto the camp of Aram, and they come in unto the extremity of the camp of Aram, and lo, there is not a man there,
6 Kwa kuwa Bwana alikuwa ameunda jeshi la Washami kusikia sauti ya magari ya farasi, na sauti za farasi-sauti za jeshi jingine kubwa, ndipo wakaambizana kila mmoja wao, “Yule mfalme wa Israeli amekodisha wafalme wa Wahiti na Wamisri waje wapigane dhidi yetu.”
seeing Jehovah hath caused the camp of Aram to hear a noise of chariot and a noise of horse — a noise of great force, and they say one unto another, 'Lo, the king of Israel hath hired against us the kings of the Hittites, and the kings of Egypt, to come against us.'
7 Hivyo wale maaskari wakaondoka kungali giza; waliacha mahema yao, punda zao, na kambi kama ilivyokuwa, na kukimbia kwa ajili ya maisha yao.
And they rise and flee in the twilight, and forsake their tents, and their horses, and their asses — the camp as it [is] — and flee for their life.
8 Wakati wale watu wenye ukoma walipokuja sehemu ya mwisho wa kambi, wakaenda kwenye hema moja na kula na kunywa, na kubeba fedha na dhahabu na nguo, na kwenda na kuzificha. Wakarudi na kuingia kwenye hema nyingine na kubeba kutoka pale pia, na kwenda kuvificha.
And these lepers come in unto the extremity of the camp, and come in unto one tent, and eat, and drink, and lift up thence silver, and gold, and garments, and go and hide; and they turn back and go in unto another tent, and lift up thence, and go and hide.
9 Basi, wakaambizana kila mmoja, “Hatufanyi sahihi. Siku hii ni siku ya habari njema, lakini tunanyamaza kimya kuhusu hili. Kama tukisubiri mpaka kutakapopambazuka, adhabu itakuwa juu yetu. Basi, njoni, twendeni na kuwaambia nyumba ya mfalme.”
And they say one unto another, 'We are not doing right this day; a day of tidings it [is], and we are keeping silent; and — we have waited till the light of the morning, then hath punishment found us; and now, come and we go in and declare to the house of the king.'
10 Kwa hiyo wakaenda na kuwaita mabawabu wa mji. Wakawaambia, wakisema, “Tumeenda kambi ya Washami, lakini hapakuwa na mtu pale, hakuna sauti ya mtu yeyote, lakini kulikuwa na farasi wamefungwa, na punda wamefungwa, na zile hema kama zilivyokuwa.”
And they come in, and call unto the gatekeeper of the city, and declare for themselves, saying, 'We have come in unto the camp of Aram, and lo, there is not there a man, or sound of man, but the bound horse, and the bound ass, and tents as they [are].'
11 Ndipo mabawabu wakatoa habari, ndipo wakaambiwa ndani ya nyumba ya mfalme.
and he calleth the gatekeepers, and they declare to the house of the king within.
12 Basi yule mfalme akainuka usiku nakusema kwa watumishi wake, “Nitawaambia sasa kile ambacho Washami walichotufanyia. Wanajua kwamba tunanjaa, hivyo wameondoka kwenye kambi kwenda kujificha kwenye mashamba. Wanasema, 'Wakati watakapotoka mjini, tutawakamata wakiwa hai, na kuingia mjini.”
And the king riseth by night, and saith unto his servants, 'Let me declare, I pray you, to you that which the Aramaeans have done to us; they have known that we are famished, and they are gone out from the camp to be hidden in the field, saying, When they come out from the city, then we catch them alive, and unto the city we enter.'
13 Mmoja wa wale watumishi wa mfalme akajibu na kusema, “Nakuomba, ngoja baadhi ya watu wachukue farasi watano wale waliosalia, ambao wamebaki kwenye mji. Wako kama mkutano wote wa Israeli waliobaki-wengi wamekufa; ngoja tuwatume na tuone.”
And one of his servants answereth and saith, 'Then let them take, I pray thee, five of the horses that are left, that have been left in it — lo, they [are] as all the multitude of Israel who have been left in it; lo, they are as all the multitude of Israel who have been consumed — and we send and see.'
14 Hivyo wakachukua magari mawili ya farasi pamoja na farasi, na mfalme akawatuma baada ya jeshi la Washami, akisema, “Enendeni mkaone.”
And they take two chariot-horses, and the king sendeth after the camp of Aram, saying, 'Go, and see.'
15 Wakawafuata kwenda Yordani, na barabara zote zilikuwa zimejaa na vifaa ambavyo Washami walivitupa wapate kukimbia haraka. Kwa hiyo wale wajumbe wakarudi na kumwambia mfalme.
And they go after them unto the Jordan, and lo, all the way is full of garments and vessels that the Aramaeans have cast away in their haste, and the messengers turn back and declare to the king.
16 Wale watu wakatoka nje na wakaziteka nyara zile kambi za Washami. Hivyo kipimo cha unga mzuri uliuzwa kwa shekeli moja, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli moja, kama vile ambavyo neno la Yahwe lilivyosema.
And the people go out and spoil the camp of Aram, and there is a measure of fine flour at a shekel, and two measures of barley at a shekel, according to the word of Jehovah.
17 Naye mfalme alimwagiza yule nahodha ambaye alitegemea mkono wake kuwa mkuu wa lango, na watu wakamkanyaga chini langoni. Alikufa kama mtu wa Mungu alivyosema, ambaye ameongea wakati yule mfalme alipomshukia.
And the king hath appointed the captain, by whose hand he is supported, over the gate, and the people tread him down in the gate, and he dieth, as the man of God spake, which he spake in the coming down of the king unto him,
18 Basi ikatokea kama yule mtu wa Mungu alivyosema kwa mfalme akisema, “Mda kama huu kwenye lango la Samaria, vipimo viwili vya shayiri vitapatikana kwa shekeli, na kipimo cha unga mzuri kwa shekeli.”
yea, it cometh to pass, according to the speaking of the man of God unto the king, saying, 'Two measures of barley at a shekel, and a measure of fine flour at a shekel are, at this time to-morrow, in the gate of Samaria;'
19 Yule nahodha alimjibu yule mtu wa Mungu na kusema, “Tazama, hata kama Yahwe angefanya madirisha mbinguni, je hiki kitu kingeweza kutokea” Elisha akasema, “Tazama, utaona kikitokea kwa macho yako mwenyewe, lakini hutakula chochote katika hicho.”
and the captain answereth the man of God, and saith, 'And lo, Jehovah is making windows in the heavens — it is according to this word?' and he saith, 'Lo, thou art seeing with thine eyes, and thereof thou dost not eat;'
20 Hivyo ndivyo haswa kilichompata, kwa kuwa watu wakamkanyaga kwenye lango, na kufa.
and it cometh to him so, and the people tread him down in the gate, and he dieth.

< 2 Wafalme 7 >