< 1 Wafalme 18 >

1 Kwa hiyo baada ya siku nyingi neno la BWANA likamjia Eliya, katika mwaka wa tatu wa ukame, likisema, “Nenda ukajionyeshe mwenyewe kwa Ahabu nami nitainyeshea ardhi mvua.”
And the days are many, and the word of Jehovah hath been unto Elijah in the third year, saying, 'Go, appear unto Ahab, and I give rain on the face of the ground;'
2 Eliya akaenda kujionyesha mwenyewe kwa Ahabu; sasa njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.
and Elijah goeth to appear unto Ahab. And the famine is severe in Samaria,
3 Ahabu akamwita Obadia, aliyekuwa mkuu wa ikulu. Obadia alimheshimu sana BWANA,
and Ahab calleth unto Obadiah, who [is] over the house — and Obadiah hath been fearing Jehovah greatly,
4 kwa kuwa wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa BWANA, Obadia alichukua manabii mia akawaficha katika makundi ya hamsini hamsini katika pango na akawalisha kwa mikate na maji.
and it cometh to pass, in Jezebel's cutting off the prophets of Jehovah, that Obadiah taketh a hundred prophets, and hideth them, fifty men in a cave, and hath sustained them with bread and water —
5 Ahabu akamwambia Obadia, “Pita katika nchi yote na katika chemichemi zote za maji na vijito. Yamkini tunaweza kupata maji na nyasi ili tuwaokoa hawa farasi na nyumbu, ili tusiwakose wanyama wote.”
and Ahab saith unto Obadiah, 'Go through the land, unto all fountains of waters, and unto all the brooks, if so be we find hay, and keep alive horse and mule, and do not cut off any of the cattle.'
6 Kwa hiyo wakaigawa nchi kati yao ili wapite kati yake wakitafuta maji. Ahabu akaenda njia yake mwenyewe na Obadia naye akaenda njia yake.
And they apportion to themselves the land, to pass over into it; Ahab hath gone in one way by himself, and Obadiah hath gone in another way by himself;
7 Wakati Obadia akiwa njiani, akakutana na Eliya pasipo kutegemea. Obadia akamtambua na akalala kifudifudi chini. Akamwambia, “Ndiye wewe, bwana wangu Eliya?”
and Obadiah [is] in the way, and lo, Elijah — to meet him; and he discerneth him, and falleth on his face, and saith, 'Art thou he — my lord Elijah?'
8 Naye Eliya akamjibu, Ni mimi. Nenda umwambie bwana wako, 'Tazama, Eliya yuko hapa.'”
And he saith to him, 'I [am]; go, say to thy lord, Lo, Elijah.'
9 Obadia akamjibu. “Nimekoseaje, kwamba umtoe mtumishi wako katika mkono wa Ahabu ili aniue?
And he saith, 'What have I sinned, that thou art giving thy servant into the hand of Ahab — to put me to death?
10 Kama BWANA Mungu wako aishivyo, hakuna taifa wala ufalme ambapo bwana wangu hajatuma watu kukutafuta. Kila taifa au ufalme unaposema, “Eliya hayuko hapa,' Ahabu hufanya waape ni kweli hawajakuona.
Jehovah thy God liveth, if there is a nation and kingdom whither my lord hath not sent to seek thee; and they said, He is not, then he caused the kingdom and the nation to swear, that it doth not find thee;
11 Na sasa wewe unasema, 'Nenda, ukamwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa.'
and now, thou art saying, Go, say to thy lord, Lo, Elijah;
12 Mara tu baada ya kukuacha Roho wa BWANA atakuchukua na kukupeleka mahali ambapo sitapajua. Kisha nikienda na kumwambia Ahabu, na asipokuona, ataniua. Bado, mimi, mtumishi wako, nimekuwa nikimwabudu BWANA kutoka ujana wangu.
and it hath been, I go from thee, and the Spirit of Jehovah doth lift thee up, whither I know not, and I have come to declare to Ahab, and he doth not find thee, and he hath slain me; and thy servant is fearing Jehovah from my youth.
13 Je, haujaambiwa, bwana wangu, nilichokifanya wakati Yezebeli alipowaua manabii wa BWANA, jinsi nilivyowaficha wale manabii mia moja wa BWANA katika makundi ya hamsini kwenye pango na kuwalisha kwa mikate na maji?
'Hath it not been declared to my lord that which I have done in Jezebel's slaying the prophets of Jehovah, that I hide of the prophets of Jehovah a hundred men, fifty by fifty in a cave, and sustained them with bread and water?
14 Na sasa unasema, 'Nenda umwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa,' kwa hiyo ataniua.”
and now thou art saying, Go, say to my lord, Lo, Elijah — and he hath slain me!'
15 Ndipo Eliya alipomjibu, “Kama vile BWANA wa majeshi aishivyo, ambaye mimi ninasimama, Kwa hakika nitajionyeshakwa Ahabu leo.”
And Elijah saith, 'Jehovah of Hosts liveth, before whom I have stood, surely to-day I appear unto him.'
16 Kwa hiyo Obadia akaenda kukutana na Ahabu, nakumwambia kile Eliya alichokuwa amemwambia. Ndipo mfalme alipoenda kukutana na Eliya.
And Obadiah goeth to meet Ahab, and declareth [it] to him, and Ahab goeth to meet Elijah,
17 Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe? Wewe mtabishaji wa Israeli!”
and it cometh to pass at Ahab's seeing Elijah, that Ahab saith unto him, 'Art thou he — the troubler of Israel?'
18 Eliya akamwambia, “Mimi sijaitabisha Israeli, Lakiini wewe na familia ya baba yako ndio watabishaji kwa kuziacha amri za BWANA na kufuata sanamu za Baali.
And he saith, 'I have not troubled Israel, but thou and the house of thy father, in your forsaking the commands of Jehovah, and thou goest after the Baalim;
19 Kwa hiyo sasa, Tuma neno na unikusanyie Israeli yote katika mlima Kameli, pamoja na manabii 450 wa Baali na wale manabii 400 wa Ashera wanaokula kwenye meza ya Yezebeli.”
and now, send, gather unto me all Israel, unto the mount of Carmel, and the prophets of Baal four hundred and fifty, and the prophets of the shrine, four hundred — eating at the table of Jezebel.'
20 Kwa hiyo Ahabu akatuma neno kwa watu wote wa Israeli na akawakusanya manabii wote kwenye mlima Kameli.
And Ahab sendeth among all the sons of Israel, and gathereth the prophets unto the mount of Carmel;
21 Eliya akaja karibu na watu wote akasema, “Mtaendelea kubadilisha mawazo yenu mpaka lini? Kama BWANA ni Mungu, mfuateni yeye, Lakini kama Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye,” Lakini watu hawakumjibu neno.
and Elijah cometh nigh unto all the people, and saith, 'Till when are ye leaping on the two branches? — if Jehovah [is] God, go after Him; and if Baal, go after him;' and the people have not answered him a word.
22 Kisha Eliya akawaambia wale watu, “Mimi, pekee yangu, ndiye niliyebaki kuwa nabii wa BWANA, lakini manabii wa Baali wako 450.
And Elijah saith unto the people, 'I — I have been left a prophet of Jehovah — by myself; and the prophets of Baal [are] four hundred and fifty men;
23 Hebu tutoleeni ng'ombe wawili. Nao wajichagulie ng'ombe mmoja na wamchinje na kumkatakata katika vipnde, na wamweke kwenye kuni, na wasitie moto chini yake. Nami nitamwandaa yule wa pili na kumweke juu ya kuni nami sitatia moto chini yake.
and let them give to us two bullocks, and they choose for themselves the one bullock, and cut it in pieces, and place [it] on the wood, and place no fire; and I — I prepare the other bullock, and have put [it] on the wood, and fire I do not place; —
24 Kisha mtaliita jina la mungu wenu, nami nitaliita jina la BWANA, na Mungu atakayejibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.” Watu wote wakajibu na kusema, “Hilo ni jambo jema.”
and ye have called in the name of your god, and I — I call in the name of Jehovah, and it hath been, the god who answereth by fire — He [is] the God.' And all the people answer and say, 'Good [is] the word.'
25 Kwa Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni ng'ombe mmoja kwa ajili yenu na mwe wa kwanza kumwamdaa, kwa kuwa ninyi ni wengi, Kisha liiteni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
And Elijah saith to the prophets of Baal, 'Choose for you the one bullock, and prepare first, for ye [are] the multitude, and call ye in the name of your god, and place no fire.'
26 Nao wakamchukua yule ng'ombe waliokuwa wamepewa na wakamwandaa, na ndipo walipoliita jina la Baali kuanzia asubuhi hadi adhuhuri, wakisema, “Baali, tusikie.” Lakini hapakuwepo na Sauti, na wala hakuna aliyejibu. Wakachezacheza kuizunguka madhabahu waliyotengeneza.
And they take the bullock that [one] gave to them, and prepare, and call in the name of Baal from the morning even till the noon, saying, 'O Baal, answer us!' and there is no voice, and there is none answering; and they leap on the altar that one had made.
27 Ilipofika adhuhuri Eliya akawakejeli akisema, “Mwiteni kwa nguvu! Huyo ni mungu! labda anawaza kitu, au amepumzika, au yuko safarini, au pengine amelala sharti aamshwe.”
And it cometh to pass, at noon, that Elijah playeth on them, and saith, 'Call with a loud voice, for he [is] a god, for he is meditating, or pursuing, or on a journey; it may be he is asleep, an doth awake.'
28 Kwa hiyo wakamwita kwa nguvu, wakajikatakata kama kawaida yao ilivyokuwa, kwa upanga na nyembe, mpaka damu ikawachuruzika.
And they call with a loud voice, and cut themselves, according to their ordinance, with swords and with spears, till a flowing of blood [is] on them;
29 Ikawa wakati wa adhuhuri ulipopita, na bado walikuwa wakiendelea kutabiri mpaka wakati wa jioni wa kutoa dhabihu, lakini hapakuwepo na sauti wala mtu wa kuwajibu; wala hapakuwepo na yeyote wa kujibu wala wa kuangalia.
and it cometh to pass, at the passing by of the noon, that they feign themselves prophets till the going up of the present, and there is no voice, and there is none answering, and there is none attending.
30 Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Nisogeleeni,” na watu wote wakamsogelea. Naye akatengeneza ile madhabahu ya BWANA ambayo ilikuwa imeharibika.
And Elijah saith to all the people, 'Come nigh unto me;' and all the people come nigh unto him, and he repaireth the altar of Jehovah that is broken down;
31 Eliya akachukua mawe kumi na mawili, kila jiwe moja liliwakilisha kabila moja la wana wa Yakobo - ni kupitia Yakobo kwamba neno la BWANA lilikuja, likisema, “Jina lako litakuwa Israel.”
and Elijah taketh twelve stones, according to the number of the tribes of the sons of Jacob, unto whom the word of Jehovah was, saying, 'Israel is thy name;'
32 Kwa kutumia hayo mawe aliijenga ile madhabahu kwa jina la BWANA na akachimba mfereji kuizunguka ile madhabahu kubwa kiasi cha kubeba lita kumi na tano za maji.
and he buildeth with the stones an altar, in the name of Jehovah, and maketh a trench, as about the space of two measures of seed, round about the altar.
33 Kisha akaweka kuni kwa ajili ya moto na akamkatakata yule ng'ombe katika vipande vipande na akaweka vile vipande juu ya kuni. Na akasema, “Vijazeni maji hivyo vyombo na yamwageni kwenye hiyo sadaka ya kueketezwa na juu ya hizo kuni.”
And he arrangeth the wood, and cutteth in pieces the bullock, and placeth [it] on the wood, and saith, 'Fill ye four pitchers of water, and pour on the burnt-offering, and on the wood;
34 Akasema tena fanyeni hivyo mara ya pili,” nao wakafanya kwa mara ya pili. kisha akasema, “Fanyeni mara ya tatu,” nao wakafanya kwa mara ya tatu.
and he saith, 'Do [it] a second time;' and they do [it] a second time; and he saith, 'Do [it] a third time;' and they do [it] a third time;
35 Maji yakaizunguka ile madhabahu na kuujaza ule mfereji.
and the water goeth round about the altar, and also, the trench he hath filled with water.
36 Ikawa wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea na akasema, “BWANA, Mungu wa Abrahamu, na wa Isaka, na wa Israeli, na ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu wa Israeli, na kwamba mimi ni mtumishi wako, na kwamba nimeyafanya mambo haya yote kwa jina lako.
And it cometh to pass, at the going up of the [evening -]present, that Elijah the prophet cometh nigh and saith, 'Jehovah, God of Abraham, Isaac, and Israel, to-day let it be known that Thou [art] God in Israel, and I Thy servant, that by Thy word I have done the whole of these things;
37 Nisikie, BWANA, nisike, ili hawa watu wajue kuwa wewe, BWANA, ndiye Mungu, na kwamba umeirudisha mioyo yao kwako tena.”
answer me, O Jehovah, answer me, and this people doth know that Thou [art] Jehovah God; and Thou hast turned their heart backward.'
38 Ndipo moto wa BWANA ukashuka ukairamba ile sadaka, pamoja na zile kuni, mawe na mavumbi, na kuyaramba yale maji yaliyokuwa kwenye ule mfereji.
And there falleth a fire of Jehovah, and consumeth the burnt-offering, and the wood, and the stones, and the dust, and the water that [is] in the trench it hath licked up.
39 watu wote walipoona haya, wakalala kifudifudi chini wakasema, “BWANA, ndiye Mungu! BWANA ndiye Mungu!
And all the people see, and fall on their faces, and say, 'Jehovah, He [is] the God, Jehovah, He [is] the God.'
40 Kwa hiyo Eliya akawaambia, “Wakamateni manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja wao atoroke.” Kwa hiyo wakawakamata, na Eliya akawaleta manabii wa Baali chini kwenye kijito cha Kishoni na akawaua huko.
And Elijah saith to them, 'Catch ye the prophets of Baal; let not a man escape of them;' and they catch them, and Elijah bringeth them down unto the stream Kishon, and doth slaughter them there.
41 Eliya akamwambia Ahabu, “Inuka, ule na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.”
And Elijah saith to Ahab, 'Go up, eat and drink, because of the sound of the noise of the shower.'
42 Kwa hiyo Ahabu akaenda akala na knywa. Kisha Eliya akaenda juu ya mlima Kameli, akasudu chini na akaweka uso wake katikati ya magoti.
And Ahab goeth up to eat, and to drink, and Elijah hath gone up unto the top of Carmel, and he stretcheth himself out on the earth, and he placeth his face between his knees,
43 Akamwambia mtumishi wake, “Nenda sasa, utazame upande wa bahari.” mtumishi wake akaenda na akasema, “Hakuna kitu,” Eliya akamwambia, “Nenda tena, mpaka mara saba.”
and saith unto his young man, 'Go up, I pray thee, look attentively the way of the sea;' and he goeth up and looketh attentively, and saith, 'There is nothing;' and he saith, 'Turn back,' seven times.
44 Ile mara ya saba mtumishi wake akasema, “Tazama, kuna wingu linapanda kutoka baharini, ni dogo kama mkono wa mtu.” Eliya akamjibu, Nenda ukamwambie Ahabu, 'Andaa gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.'”
And it cometh to pass, at the seventh, that he saith, 'Lo, a little thickness as the palm of a man is coming up out of the sea.' And he saith, 'Go up, say unto Ahab, 'Bind — and go down, and the shower doth not restrain thee.'
45 Ikatokea baada ya muda mfupi mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, na kulikuwa na mvua kubwa. Ahabu akapanda gari akaenda zake Yezreeli,
And it cometh to pass, in the meantime, that the heavens have become black — thick clouds and wind — and the shower is great; and Ahab rideth, and goeth to Jezreel,
46 lakini mkono wa BWANA ulikuwa juu ya Eliya. Akalikaza vazi lake kwa mshipi wake na akakimbia mbele ya Ahabu kwenye lango la Yezreeli.
and the hand of Jehovah hath been on Elijah, and he girdeth up his loins, and runneth before Ahab, till thine entering Jezreel.

< 1 Wafalme 18 >