< 1 Wafalme 20 >

1 Beni Hadadi mfalme wa Shamu akakusanya jeshi lake lote pamoja. Kulikuwa na wafalme thelathini na mbili wasaidizi pamoja naye, na magari na farasi. Akapanda, akaihusuru Samaria na kupigana nayo.
And Ben-Hadad king of Aram hath gathered all his force, and thirty and two kings [are] with him, and horse and chariot, and he goeth up and layeth siege against Samaria, and fighteth with it,
2 Akatuma wajumbe katika mji kwa Ahabu mfalme wa Israeli, akamwambia, “Beni Hadadi anasema hivi:
and sendeth messengers unto Ahab king of Israel, to the city,
3 Fedha zako na dhahabu zako ni zangu. Pia wake zako na watoto, wale wazuri, sasa ni wangu.”
and saith to him, 'Thus said Ben-Hadad, 'Thy silver and thy gold are mine, and thy wives and thy sons — the best — are mine.'
4 Mfalme wa Israeli akajibu akasema, “Na iwe kama unavyosema, bwana wangu, mfalme. Mimi pamoja na vile nilivyo navyo ni mali yako.”
And the king of Israel answereth and saith, 'According to thy word, my lord, O king: I [am] thine, and all that I have.'
5 Wale wajumbe wakaja tena wakasema, “Beni Hadadi anasema hivi, 'Nilituma neno kwako nikisema kwamba lazima ukabidhi kwangu fedha zako, dhahabu zako, wake zako na watoto wako.
And the messengers turn back and say, 'Thus spake Ben-Hadad, saying, Surely I sent unto thee, saying, Thy silver, and thy gold, and thy wives, and thy sons, to me thou dost give;
6 Lakini kesho nitatuma watumishi wangu kwako wakati kama huu, nao wataichunguza nyumba yako na nyumba za watumishi wako. Nao watatia mikononi mwao na kukichukua kila wakipendacho machoni mwao.'”
for if, at this time to-morrow, I send my servants unto thee then they have searched thy house, and the houses of thy servants, and it hath been, every desirable thing of thine eyes they place in their hand, and have taken away.'
7 Ndipo mfalme wa Israeli akawaita wazee wote wa nchi pamoja akawaambia, ''Hebu angalieni jinsi huyu mtu anavyotafuta matatizo. Amenitumia ujumbe kwamba anataka kuchukua wake zangu, watoto wangu, fedha na dhahabu zangu, nami sijamkatalia.”
And the king of Israel calleth to all the elders of the land, and saith, 'Know, I pray you, and see that evil this [one] is seeking, for he sent unto me for my wives, and for my sons, and for my silver, and for my gold, and I withheld not from him.'
8 Wazee wote na watu wote wakamwambia Ahabu, “Usimsikilize wala kukubaliana na matakwa yake.”
And all the elders and all the people say unto him, 'Do not hearken, nor consent.'
9 Ahabu akawaambia wajumbe wa Beni Hadadi, “Mwambieni bwana wangu mfalme kwamba, 'Ninakubaliana na kila kitu ambacho kwanza uliwatuma watumishi wako kufanya kwangu, lakini sikubaliani na matakwa yako haya ya pili.'” Wale watumishi wa Beni Hadadi wakaondoka wakampelekea mrejesho Beni Hadadi.
And he saith to the messengers of Ben-Hadad, 'Say to my lord the king, All that thou didst send for unto thy servant at the first I do, and this thing I am not able to do;' and the messengers go and take him back word.
10 Naye Beni Hadadi akatuma tena majibu yake kwa Ahabu, akaisema, “basi miungu inifanyie hivyo na zaidi, kama hata mavumbi ya Samaria yatawatosheleza watu watu wote wanaonifuata kuchukua kila mmoja angalau konzi mkononi mwake.”
And Ben-Hadad sendeth unto him, and saith, 'Thus do the gods to me, and thus do they add, if the dust of Samaria suffice for handfuls for all the people who [are] at my feet.'
11 Naye mfalme wa Israeli akamjibu akisema, “Mwabieni Beni Hadadi, 'Hakuna abebaye silaha yake, atakayejivuna kama wakati wa kuishusha.”'
And the king of Israel answereth and saith, 'Speak ye: let not him who is girding on boast himself as him who is loosing [his armour].'
12 Beni Hadadi aliusikia ujumbe huu wakati alipokuwa akinywa, yeye na wafalme walikuwa pamoja naye waliokuwa kwenye mahema yao. Beni Hadadi akayaamuru majaeshi yake, “Jipangeni katika sehemu zenu kwa ajili ya vita.” Kwa hiyo wakajiandaa kivita ili kuuvamia mji.
And it cometh to pass at the hearing of this word — and he is drinking, he and the kings, in the booths — that he saith unto his servants, 'Set yourselves;' and they set themselves against the city.
13 Tazama, nabii akaja kwa Ahabu mfalme wa Israeli akasema, “BWANA asema, 'Je umeliona hili jeshi kubwa? Tazama, nitaliweka katika mkono wako leo, nawe utatambua kuwa mimi ni BWANA.'”
And lo, a certain prophet hath come nigh unto Ahab king of Israel, and saith, 'Thus said Jehovah, 'Hast thou seen all this great multitude? lo, I am giving it into thy hand to-day, and thou hast known that I [am] Jehovah.'
14 Naye Ahabu akajibu, ''kwa nani? BWANA akamjibu akasema, “kwa kuwatumia viijana wanaotumikia maliwali wa wilaya.” kisha Ahabu akasema, “Ni nani atakayepewa hiyo vita?' BWANA akamwambia, “wewe.”
And Ahab saith, 'By whom?' and he saith, 'Thus said Jehovah, By the young men of the heads of the provinces;' and he saith, 'Who doth direct the battle?' and he saith, 'Thou.'
15 Ndipo Ahabu alipowataarifu wale vijna wanaowatumikia maliwali wa wilaya. Idadi yao ilikuwa 232. Baada yao aliwahesabu wanajeshi wote, jeshi lote la Israeli; idadi yao ilikuwa elfu saba.
And he inspecteth the young men of the heads of the provinces, and they are two hundred, two and thirty, and after them he hath inspecteth the whole of the people, all the sons of Israel, seven thousand,
16 Nao wakatoka wakati wa adhuhuri. Naye Beni Hadadi alikuwa akinywa na kulewa hemani mwake, yeye na wale wafalme wadogo thelathini na mbili waliokuwa wakimsaidia.
and they go out at noon, and Ben-Hadad is drinking — drunk in the booths, he and the kings, the thirty and two kings, helping him.
17 Wale maakida vijana waliokuwa wakiwasaidia maliwali wa wilaya walitangulia kwanza. Kisha Beni Hadadi alitaarifiwa na wanaskauti aliokuwa amewatuma kwamaba, “kuna watu wanakuja kutoka Samaria.”
And the young men of the heads of the provinces go out at the first, and Ben-Hadad sendeth, and they declare to him, saying, 'Men have come out of Samaria.'
18 Beni Hadadi akasema, “wawe wamekuja kwa amani au kwa vita, wakamteni wakiwa hai.”
And he saith, 'If for peace they have come out — catch them alive; and if for battle they have come out — alive catch them.'
19 Kwa hiyo wale vijvana wanaowatumikia maliwali wa wilaya wakaenda mjini na jeshi likawafuata kwa nyuma.
And these have gone out of the city — the young men of the heads of the provinces — and the force that [is] after them,
20 Kila mmoja akaua adui wake na wale washami wakakimbia. Israeli ikawashinda. Beni Hadadi mfalme wa Shamu akatoroka kwa farasi pamoja na wapanda farasi.
and smite each his man, and Aram fleeth, and Israel pursueth them, and Ben-Hadad king of Aram escapeth on a horse, and the horsemen;
21 Kisha mfalme wa Israeli akaenda akawashambulia farasi na magari, na kuwaua washami kwa mauaji makubwa.
and the king of Israel goeth out, and smiteth the horses, and the charioteers, and hath smitten among the Aramaeans a great smiting.
22 Yule nabii akaja kwa mfalme wa Israeli akamwambia, “Nenda, ukajiimarishe mwenyewe, uelewa na kupanga kile unachofanya, kwa sababu mwakani mfalme wa Shamu atapanda dhidi yako tena.”
And the prophet cometh nigh unto the king of Israel, and saith to him, 'Go, strengthen thyself, and know and see that which thou dost, for at the turn of the year the king of Aram is coming up against thee.'
23 Wale watumishi wa mfalme wa Shamu wakamwambia, “Mungu wao ni mungu wa milimani. Hiyo ndiyo sababu walikuwa na nguvu kuliko tulivyokuwa. Lakini sasa hebu tupigane nao katika nchi tambarare, na kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko wao.
And the servants of the king of Aram said unto him, 'Gods of hills [are] their gods, therefore they were stronger than we; and yet, we fight with them in the plain — are we not stronger than they?
24 Na ufanye hivi: waondoe wafalme; mwondoe kila mmoja mahali pake ukaweke majemedari mahali pao.
'And this thing do thou: turn aside the kings each out of his place, and set captains in their stead;
25 Kisha ujihesabie jeshi kama lile jeshi ulilopoteza, farasi kwa farasi na gari kwa gari, nasi tutapigana nao katika nchi tambarare. Kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko walivyo.” Kwa hiyo Beni Hadadi akausikiliza ushauri huo naye akafanya kama alivyoshauriwa.
and thou, number to thee a force as the force that is fallen from thee, and horse for horse, and chariot for chariot, and we fight with them in the plain; are we not stronger than they?' and he hearkeneth to their voice, and doth so.
26 Baada ya mwanzo wa mwaka mpya, Beni Hadadi akawahesabu Washami na akapanda Afeki kupigana na Israeli.
And it cometh to pass at the turn of the year, that Ben-Hadad inspecteth the Aramaeans, and goeth up to Aphek, to battle with Israel,
27 Watu wa Israeli walikuwa wamehesabiwa na walikuwa wamejipanga kupigana nao. Watu wa Israeli wakafanya kambi mbele yao kama makundi mawili madogo ya mbuzi, lakini Washami wakaujaza upande wa nchi.
and the sons of Israel have been inspected, and supported, and go to meet them, and the sons of Israel encamp before them, like two flocks of goats, and the Aramaeans have filled the land.
28 Ndipo mtu wa Mungu akaja karibu akaongea mfalme wa Israeli akamwambia, “BWANA anasema: 'Kwa kuwa Washami wamesema kuwa BWANA ni mungu wa milima, na wala si mungu wa mabondeni, nitaliweka hili jeshi kubwa mkononi mwako, nawe utajua kuwa mimi ni BWANA.'”
And there cometh nigh a man of God, and speaketh unto the king of Israel, and saith, 'Thus said Jehovah, Because that the Aramaeans have said, God of hills [is] Jehovah, and He [is] not God of valleys — I have given the whole of this great multitude into thy hand, and ye have known that I [am] Jehovah.'
29 Kwa hiyo majeshi yakaweka kambi yakikabiliana kwa muda wa siku saba. Kisha siku ya saba vita vikaanza. Watu wa Israeli wakawaua Washami 100, 000 wanajeshi wa ardhini kwa siku moja.
And they encamp one over-against another seven days, and it cometh to pass on the seventh day, that the battle draweth near, and the sons of Israel smite Aram — a hundred thousand footmen in one day.
30 Waliobaki wakakimbilia Afeki, mjini, na ule ukuta ukaanguka juu ya watu ishiriinina saba elfu waliobaki. Naye Beni Hadadi akakimbilia mjini. akaingia kwenye chumba cha ndani.
And those left flee to Aphek, unto the city, and the wall falleth on twenty and seven chief men who are left, and Ben-Hadad hath fled, and cometh in unto the city, into the innermost part.
31 Wale watumishi wa Beni Hadadi wakamwambia, “Tazama sasa, tumesikia kwamba wale wafalme wa nyumba ya Israeli ni wenye rehema. Tafadhali hebu tuvaeni magaunia viunoni mwetu na kamba vichwani mwetu, na twendeni kwa mfalme wa Israeli. Labda atakuokoa roho yako.”
And his servants say unto him, 'Lo, we pray thee, we have heard that the kings of the house of Israel — that they are kind kings; let us put, we pray thee, sackcloth on our loins, and ropes on our heads, and we go out unto the king of Israel; it may be he doth keep thee alive.'
32 Kwa hiyo wakavaa magunia viunoni mwao na kujifunga kamba vichwani mwao na kisha wakaenda kwa mfalme wa Israeli wakamwambia, “Mtumishi wako Beni Hadadi, anasema, 'tafadhali niachie uhai wangu.” Ahabu akawaambia, “Je, bado yuko hai? Yeye ni ndugu yangu.”
And they gird sackcloth on their loins, and ropes [are] on their heads, and they come in unto the king of Israel, and say, 'Thy servant Ben-Hadad hath said, Let me live, I pray thee;' and he saith, 'Is he yet alive? he [is] my brother.'
33 Sasa wale watu walikuwa wakisikiliza ishara yeyote kutoka kwa Ahabu, kwa hiyo wakamjibu haraka, “Ndiyo ndugu yako Beni Hadadi bado yuko hai.” Ahabu akawaambia, “Nendeni mkamlete.” Ndipo Beni Hadadi alipokuja kwake, na Ahabu akamwacha aje kwenye gari lake.
And the men observe diligently, and hasten, and catch it from him, and say, 'Thy brother Ben-Hadad;' and he saith, 'Go ye in, bring him;' and Ben-Hadad cometh out unto him, and he causeth him to come up on the chariot.
34 Beni Hadadi akamwambia Ahabu, “Nitakurudishia miji yako ambayo baba yangu alichukua toka kwa baba yako, na unaweza kutengeneza masoko kwa ajili yako Dameski, kama baba yangu alivyofanya kule Samaria.” Ahabu akajibu, “Nitakuacha uende kwa agano hili.” Kwa hiyo Ahabu akafanya agano naye kisha akamwacha aende.
And he saith unto him, 'The cities that my father took from thy father, I give back, and streets thou dost make for thee in Damascus, as my father did in Samaria;' — 'and I, with a covenant, send thee away;' and he maketh with him a covenant, and sendeth him away.
35 Mtu mmoja, mmoja wana wa wana wa manabii, akamwambia mmoja wa wale manabii wenzake kwa neno la BWANA, “Tafadhali nipige.” Lakini yule mtu akakataa kumpiga.
And a certain man of the sons of the prophets said unto his neighbour by the word of Jehovah, 'Smite me, I pray thee;' and the man refuseth to smite him,
36 Kisha yule nabii akamwambia nabii mwenzake, “Kwa sababu umekataa kutii sauti ya BWANA, mara tu utakaponiacha, simba atakuua.” na mara tu baad ya yule mtu kumwacha, simba akamkuta na kumwua.
and he saith to him, 'Because that thou hast not hearkened to the voice of Jehovah, lo, thou art going from me, and the lion hath smitten thee;' and he goeth from him, and the lion findeth him, and smiteth him.
37 Kisha yule nabii akamkuta mtu mwingine akamwambia, “Tafadhali nipige.”Yule mtu akampiga na kumwumiza.
And he findeth another man, and saith, 'Smite me, I pray thee;' and the man smiteth him, smiting and wounding,
38 Kisha yule nabii akaondoka akaenda kumsubiri yule mfalme barabarani; naye alikuwa amejibadilisha kwa kilemba machoni pake.
and the prophet goeth and standeth for the king on the way, and disguiseth himself with ashes on his eyes.
39 Ikawa mfalme alipokuwa akipita, Yule nabii akamwita mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako alienda katikati ya pigano, na askari akasimama akamleta adui kwangu akasema, 'Mwangalie mtu huyu. Na ikiwa kwa vyovyote atatoroka, basi maisha yako yatatolewa kwa ajili ya maisha yake vinginevyo utalipa kilo thelathini za fedha.
And it cometh to pass — the king is passing by — that he hath cried unto the king, and saith, 'Thy servant went out into the midst of the battle, and lo, a man hath turned aside and bringeth in unto me a man, and saith, Keep this man; if he be at all missing, then hath thy life been for his life, or a talent of silver thou dost weigh out;
40 Lakini kwa kuwa mtumishi wako alikuwa na mambo mengi akienda huku na kule, yule askari adui akatoroka.” Basi mfalme wa Israeli akamwambia, Hivyo ndivyo itakavyokuwa hukukmu yako - umejihukumu mwenyewe.”
and it cometh to pass, thy servant is working hither and thither, and he is not!' and the king of Israel saith unto him, Right [is] thy judgment; thou hast determined [it].'
41 Ndipo yule nabii alipoondoa haraka kile kilemba machoni pake, na mfalme wa Israeli alipotambua kuwa huyo alikuwa mmoja wa manabii.
And he hasteth and turneth aside the ashes from off his eyes, and the king of Israel discerneth him, that he [is] of the prophets,
42 Yule nabii akamwambia mfalme, “BWANA anasema, 'Kwa sababu umemwachia aende mtu yule niliyekuwa nimemhukumu kifo, maisha yako yatachukua nafasi ya maisha yake.'”
and he saith unto him, 'Thus said Jehovah, Because thou hast sent away the man I devoted, out of [thy] hand, even thy life hath been for his life, and thy people for his people;'
43 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akaenda nyumbani kwake akiwa na moyo mzito na mwenye hasira, akafika Samaria.
and the king of Israel goeth unto his house, sulky and wroth, and cometh in to Samaria.

< 1 Wafalme 20 >