< Warumi 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu,
Paul, a bondservant of Jesus Christ, called to be an Apostle, set apart to proclaim God's Good News,
2 Injili ambayo Mungu alitangulia kuiahidi kwa vinywa vya manabii wake katika Maandiko Matakatifu,
which God had already promised through His Prophets in Holy Writ, concerning His Son,
3 yaani, Injili inayomhusu Mwanawe, yeye ambaye kwa uzao wa mwili alikuwa mzao wa Daudi,
who, as regards His human descent, belonged to the posterity of David,
4 na ambaye kwa uwezo wa Roho wa utakatifu alidhihirishwa kuwa Mwana wa Mungu kwa ufufuo wake kutoka kwa wafu, yaani, Yesu Kristo, Bwana wetu.
but as regards the holiness of His Spirit was decisively proved by His Resurrection to be the Son of God--I mean concerning Jesus Christ our Lord,
5 Kwa kupitia kwake na kwa ajili ya Jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu miongoni mwa watu wa mataifa yote, waje kwenye utii utokanao na imani.
through whom we have received grace and Apostleship in His service in order to win men to obedience to the faith, among all Gentile peoples,
6 Ninyi nyote pia mko miongoni mwa watu walioitwa ili mpate kuwa mali ya Yesu Kristo.
among whom you also, called, as you have been, to belong to Jesus Christ, are numbered:
7 Kwa wote walioko Rumi wapendwao na Mungu na kuitwa kuwa watakatifu: Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
To all God's loved ones who are in Rome, called to be saints. May grace and peace be granted to you from God our Father and the Lord Jesus Christ.
8 Kwanza kabisa, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inatangazwa duniani kote.
First of all, I thank my God through Jesus Christ for what He has done for all of you; for the report of your faith is spreading through the whole world.
9 Kwa maana Mungu ninayemtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Injili ya Mwanawe, ni shahidi wangu jinsi ninavyowakumbuka
I call God to witness--to whom I render priestly and spiritual service by telling the Good News about His Son-- how unceasingly I make mention of you in His presence,
10 katika maombi yangu siku zote, nami ninaomba kwamba hatimaye sasa kwa mapenzi ya Mungu, njia ipate kufunguliwa kwa ajili yangu ili nije kwenu.
always in my prayers entreating that now, at length, if such be His will, the way may by some means be made clear for me to come to you.
11 Ninatamani sana kuwaona ili nipate kuweka juu yenu karama za rohoni ili mwe imara,
For I am longing to see you, in order to convey to you some spiritual help, so that you may be strengthened;
12 au zaidi, ninyi pamoja nami tuweze kutiana moyo katika imani sisi kwa sisi.
in other words that while I am among you we may be mutually encouraged by one another's faith, yours and mine.
13 Ndugu zangu, napenda mfahamu kwamba mara nyingi nimekusudia kuja kwenu (ingawa mpaka sasa nimezuiliwa), ili nipate kuvuna mavuno miongoni mwenu kama nilivyovuna miongoni mwa wengine ambao ni watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
And I desire you to know, brethren, that I have many a time intended to come to you--though until now I have been disappointed--in order that among you also I might gather some fruit from my labours, as I have already done among the rest of the Gentile nations.
14 Mimi ni mdeni kwa Wayunani na kwa wasio Wayunani, kwa wenye hekima na kwa wasio na hekima.
I am already under obligations alike to Greek-speaking races and to others, to cultured and to uncultured people:
15 Ndiyo sababu ninatamani sana kuihubiri Injili kwenu pia ninyi mlioko Rumi.
so that for my part I am willing and eager to proclaim the Good News to you also who are in Rome.
16 Mimi siionei haya Injili ya Kristo kwa maana ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwanza kwa Myahudi na kwa Myunani pia.
For I am not ashamed of the Good News. It is God's power which is at work for the salvation of every one who believes--the Jew first, and then the Gentile.
17 Kwa maana katika Injili haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa, haki ile iliyo kwa njia ya imani hadi imani. Kama ilivyoandikwa: “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
For in the Good News a righteousness which comes from God is being revealed, depending on faith and tending to produce faith; as the Scripture has it, "The righteous man shall live by faith."
18 Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi wote na uovu wa wanadamu ambao huipinga kweli kwa uovu wao,
For God's anger is being revealed from Heaven against all impiety and against the iniquity of men who through iniquity suppress the truth. God is angry:
19 kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.
because what may be known about Him is plain to their inmost consciousness; for He Himself has made it plain to them.
20 Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani, uweza wake wa milele na asili yake ya Uungu, imeonekana waziwazi, ikitambuliwa kutokana na yale aliyoyafanya ili wanadamu wasiwe na udhuru. (aïdios g126)
For, from the very creation of the world, His invisible perfections--namely His eternal power and divine nature--have been rendered intelligible and clearly visible by His works, so that these men are without excuse. (aïdios g126)
21 Kwa maana ingawa walimjua Mungu, hawakumtukuza yeye kama ndiye Mungu wala hawakumshukuru, bali fikira zao zimekuwa batili na mioyo yao ya ujinga ikatiwa giza.
For when they had come to know God, they did not give Him glory as God nor render Him thanks, but they became absorbed in useless discussions, and their senseless minds were darkened.
22 Ingawa walijidai kuwa wenye hekima, wakawa wajinga
While boasting of their wisdom they became utter fools,
23 na kubadili utukufu wa Mungu aishiye milele kwa sanamu zilizofanywa zifanane na mwanadamu ambaye hufa, na mfano wa ndege, wanyama na viumbe vitambaavyo.
and, instead of worshipping the imperishable God, they worshipped images resembling perishable man or resembling birds or beasts or reptiles.
24 Kwa hiyo, Mungu akawaacha wazifuate tamaa mbaya za mioyo yao katika uasherati, hata wakavunjiana heshima miili yao wao kwa wao.
For this reason, in accordance with their own depraved cravings, God gave them up to uncleanness, allowing them to dishonour their bodies among themselves with impurity.
25 Kwa sababu waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakaabudu na kutumikia kiumbe badala ya Muumba, ahimidiwaye milele! Amen. (aiōn g165)
For they had bartered the reality of God for what is unreal, and had offered divine honours and religious service to created things, rather than to the Creator--He who is for ever blessed. Amen. (aiōn g165)
26 Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wavunjiane heshima kwa kufuata tamaa zao za aibu. Hata wanawake wao wakabadili matumizi ya asili ya miili yao wakaitumia isivyokusudiwa.
This then is the reason why God gave them up to vile passions. For not only did the women among them exchange the natural use of their bodies for one which is contrary to nature, but the men also,
27 Vivyo hivyo wanaume pia wakiacha matumizi ya asili ya wanawake wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wakafanyiana matendo ya aibu na wanaume wengine nao wakapata katika maisha yao adhabu iliyowastahili kwa ajili ya upotovu wao.
in just the same way--neglecting that for which nature intends women--burned with passion towards one another, men practising shameful vice with men, and receiving in their own selves the reward which necessarily followed their misconduct.
28 Nao kwa kuwa hawakuona umuhimu wa kudumisha ufahamu wa Mungu, yeye akawaachilia wafuate akili za upotovu, watende mambo yale yasiyostahili kutendwa.
And just as they had refused to continue to have a full knowledge of God, so it was to utterly worthless minds that God gave them up, for them to do things which should not be done.
29 Wakiwa wamejawa na udhalimu wa kila namna, uasherati, uovu, tamaa mbaya na hila. Wamejawa na husuda, uuaji, ugomvi, udanganyifu, hadaa na nia mbaya. Wao pia ni wasengenyaji,
Their hearts overflowed with all sorts of dishonesty, mischief, greed, malice. They were full of envy and murder, and were quarrelsome, crafty, and spiteful.
30 wasingiziaji, wanaomchukia Mungu, wajeuri, wenye kiburi na majivuno, wenye hila, wasiotii wazazi wao,
They were secret backbiters, open slanderers; hateful to God, insolent, haughty, boastful; inventors of new forms of sin, disobedient to parents, destitute of common sense,
31 wajinga, wasioamini, wasio na huruma na wakatili.
faithless to their promises, without natural affection, without human pity.
32 Ingawa wanafahamu sheria ya haki ya Mungu kwamba watu wanaofanya mambo kama hayo wanastahili mauti, si kwamba wanaendelea kutenda hayo tu, bali pia wanakubaliana na wale wanaoyatenda.
In short, though knowing full well the sentence which God pronounces against actions such as theirs, as things which deserve death, they not only practise them, but even encourage and applaud others who do them.

< Warumi 1 >