< Warumi 2 >

1 Kwa hiyo huna udhuru wowote, wewe utoaye hukumu kwa mwingine, kwa maana katika jambo lolote unalowahukumu wengine, unajihukumu wewe mwenyewe kwa sababu wewe unayehukumu unafanya mambo hayo hayo.
You are therefore without excuse, O man, whoever you are who sit in judgement upon others. For when you pass judgement on your fellow man, you condemn yourself; for you who sit in judgement upon others are guilty of the same misdeeds;
2 Basi tunajua kwamba hukumu ya Mungu dhidi ya wale wafanyao mambo kama hayo ni ya kweli.
and we know that God's judgement against those who commit such sins is in accordance with the truth.
3 Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?
And you who pronounce judgement upon those who do such things although your own conduct is the same as theirs--do you imagine that you yourself will escape unpunished when God judges?
4 Au waudharau wingi wa wema, ustahimili na uvumilivu wake, bila kujua kuwa wema wa Mungu wakuelekeza kwenye toba?
Or is it that you think slightingly of His infinite goodness, forbearance and patience, unaware that the goodness of God is gently drawing you to repentance?
5 Lakini kwa sababu ya ukaidi wenu na mioyo yenu isiyotaka kutubu, mnajiwekea akiba ya ghadhabu dhidi yenu wenyewe kwa siku ile ya ghadhabu ya Mungu, wakati hukumu yake ya haki itakapodhihirishwa.
The fact is that in the stubbornness of your impenitent heart you are treasuring up against yourself anger on the day of Anger--the day when the righteousness of God's judgements will stand revealed.
6 Kwa maana Mungu atamlipa kila mtu sawasawa na matendo yake.
To each man He will make an award corresponding to his actions;
7 Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios g166)
to those on the one hand who, by lives of persistent right-doing, are striving for glory, honour and immortality, the Life of the Ages; (aiōnios g166)
8 Lakini kwa wale watafutao mambo yao wenyewe na wale wanaokataa kweli na kuzifuata njia mbaya, kutakuwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
while on the other hand upon the self-willed who disobey the truth and obey unrighteousness will fall anger and fury, affliction and awful distress,
9 Kutakuwa na taabu na dhiki kwa kila mmoja atendaye maovu, Myahudi kwanza na mtu wa Mataifa pia,
coming upon the soul of every man and woman who deliberately does wrong--upon the Jew first, and then upon the Gentile;
10 bali utukufu, heshima na amani kwa ajili ya kila mmoja atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, kisha kwa mtu wa Mataifa.
whereas glory, honour and peace will be given to every one who does what is good and right--to the Jew first and then to the Gentile.
11 Kwa maana Mungu hana upendeleo.
For God pays no attention to this world's distinctions.
12 Watu wote waliotenda dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, nao wote wale waliotenda dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria.
For all who have sinned apart from the Law will also perish apart from the Law, and all who have sinned whilst living under the Law, will be judged by the Law.
13 Kwa maana si wale wanaoisikia sheria ambao ni wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaoitii sheria ndio watakaohesabiwa haki.
It is not those that merely hear the Law read who are righteous in the sight of God, but it is those that obey the Law who will be pronounced righteous.
14 (Naam, wakati wa watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanapofanya kwa asili mambo yatakiwayo na sheria, wao ni sheria kwa nafsi zao wenyewe, hata ingawa hawana sheria.
For when Gentiles who have no Law obey by natural instinct the commands of the Law, they, without having a Law, are a Law to themselves;
15 Wao wanaonyesha kwamba lile linalotakiwa na sheria limeandikwa kwenye mioyo yao, ambayo pia dhamiri zao zikiwashuhudia, nayo mawazo yao yenye kupingana yatawashtaki au kuwatetea.)
since they exhibit proof that a knowledge of the conduct which the Law requires is engraven on their hearts, while their consciences also bear witness to the Law, and their thoughts, as if in mutual discussion, accuse them or perhaps maintain their innocence--
16 Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.
on the day when God will judge the secrets of men's lives by Jesus Christ, as declared in the Good News as I have taught it.
17 Tazama, wewe ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea sheria na kujisifia uhusiano wako na Mungu,
And since you claim the name of Jew, and find rest and satisfaction in the Law, and make your boast in God,
18 kama unajua mapenzi ya Mungu na kukubali lililo bora kwa sababu umefundishwa na hiyo sheria,
and know the supreme will, and can test things that differ--being a man who receives instruction from the Law--
19 kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, na mwanga kwa wale walio gizani,
and have persuaded yourself that, as for you, you are a guide to the blind, a light to those who are in darkness,
20 mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una maarifa ya kweli katika hiyo sheria,
a schoolmaster for the dull and ignorant, a teacher of the young, because in the Law you possess an outline of real knowledge and an outline of the truth:
21 basi wewe, uwafundishaye wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, wewe mwenyewe waiba?
you then who teach your fellow man, do you refuse to teach yourself? You who cry out against stealing, are you yourself a thief?
22 Wewe usemaye mtu asizini, wewe mwenyewe wazini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, wafanya jambo la kumchukiza katika mahekalu?
You who forbid adultery, do you commit adultery? You who loathe idols, do you plunder their temples?
23 Wewe ujivuniaye sheria, wamwaibisha Mungu kwa kuvunja sheria?
You who make your boast in the Law, do you offend against its commands and so dishonour God?
24 Kama ilivyoandikwa, “Kwa ajili yenu ninyi, Jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa watu wa Mataifa.”
For the name of God is blasphemed among the Gentile nations because of you, as Holy Writ declares.
25 Kutahiriwa kuna thamani ikiwa unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
Circumcision does indeed profit, if you obey the Law; but if you are a Law-breaker, the fact that you have been circumcised counts for nothing.
26 Hivyo, ikiwa wale wasiotahiriwa wanatimiza mambo ambayo sheria inataka, je, kutokutahiriwa kwao hakutahesabiwa kuwa sawa na kutahiriwa?
In the same way if an uncircumcised man pays attention to the just requirements of the Law, shall not his lack of circumcision be overlooked, and,
27 Ndipo wale ambao hawakutahiriwa kimwili lakini wanaitii sheria watawahukumu ninyi, ambao ingawa mmetahiriwa na kuijua sana sheria ya Mungu iliyoandikwa, lakini mwaivunja.
although he is a Gentile by birth, if he scrupulously obeys the Law, shall he not sit in judgement upon you who, possessing, as you do, a written Law and circumcision, are yet a Law-breaker?
28 Kwa maana mtu si Myahudi kwa vile alivyo kwa nje, wala tohara ya kweli si kitu cha nje au cha kimwili.
For the true Jew is not the man who is simply a Jew outwardly, and true circumcision is not that which is outward and bodily.
29 Lakini mtu ni Myahudi alivyo ndani, nayo tohara ya kweli ni jambo la moyoni, ni la Roho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa namna hiyo hapokei sifa kutoka kwa wanadamu bali kwa Mungu.
But the true Jew is one inwardly, and true circumcision is heart-circumcision--not literal, but spiritual; and such people receive praise not from men, but from God.

< Warumi 2 >