< Matendo 26 >

1 Ndipo Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujitetea.” Hivyo Paulo akawaashiria kwa mkono wake, akaanza kujitetea, akasema:
Then Agrippa said to Paul, "You have permission to speak about yourself." So Paul, with outstretched arm, proceeded to make his defence.
2 “Mfalme Agripa, najiona kuwa na heri kusimama mbele yako leo ninapojitetea kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi,
"As regards all the accusations brought against me by the Jews," he said, "I think myself fortunate, King Agrippa, in being about to defend myself to-day before you,
3 hasa kwa sababu unajua vyema desturi zote za Kiyahudi na ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na masuala ya mabishano. Kwa hiyo, nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.
who are so familiar with all the customs and speculations that prevail among the Jews; and for this reason, I pray you, give me a patient hearing.
4 “Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu nilipokuwa mtoto, kuanzia mwanzo wa maisha yangu katika nchi yangu na pia huko Yerusalemu.
"The kind of life I have lived from my youth upwards, as exemplified in my early days among my nation and in Jerusalem, is known to all the Jews.
5 Wao wamefahamu kwa muda mrefu na wanaweza kushuhudia kama wakipenda, ya kwamba kutokana na misimamo mikali sana ya dhehebu letu kwenye dini yetu, niliishi nikiwa Farisayo.
For they all know me of old--if they would but testify to the fact--how, being an adherent of the strictest sect of our religion, my life was that of a Pharisee.
6 Nami sasa ni kwa sababu ya tumaini langu katika kile ambacho Mungu aliwaahidi baba zetu, ninashtakiwa leo.
And now I stand here impeached because of my hope in the fulfilment of the promise made by God to our forefathers--
7 Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
the promise which our twelve tribes, worshipping day and night with intense devotedness, hope to have made good to them. It is on the subject of this hope, Sir, that I am accused by the Jews.
8 Kwa nini yeyote miongoni mwenu afikiri kwamba ni jambo lisilosadikika Mungu kufufua wafu?
Why is it deemed with all of you a thing past belief if God raises the dead to life?
9 “Mimi pia nilikuwa nimeshawishika kwamba imenipasa kufanya yote yale yaliyowezekana kupinga Jina la Yesu wa Nazareti.
"I myself, however, thought it a duty to do many things in hostility to the name of Jesus, the Nazarene.
10 Nami hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Kwa mamlaka ya viongozi wa makuhani, niliwatia wengi wa watakatifu gerezani na walipokuwa wakiuawa, nilipiga kura yangu kuunga mkono.
And that was how I acted in Jerusalem. Armed with authority received from the High Priests I shut up many of God's people in various prisons, and when they were about to be put to death I gave my vote against them.
11 Mara nyingi nilikwenda kutoka sinagogi moja hadi ingine nikiamuru waadhibiwe, nami nilijaribu kuwalazimisha wakufuru. Katika shauku yangu dhidi yao, hata nilikwenda miji ya kigeni ili kuwatesa.
In all the synagogues also I punished them many a time, and tried to make them blaspheme; and in my wild fury I chased them even to foreign towns.
12 “Siku moja nilipokuwa katika mojawapo ya safari hizi nikiwa ninakwenda Dameski, nilikuwa na mamlaka na agizo kutoka kwa kiongozi wa makuhani.
"While thus engaged, I was travelling one day to Damascus armed with authority and a commission from the High Priests,
13 Ilikuwa yapata adhuhuri, ee mfalme, nilipokuwa njiani, niliona nuru kutoka mbinguni kali kuliko jua, ikingʼaa kunizunguka pande zote mimi na wale niliokuwa pamoja nao.
and on the journey, at noon, Sir, I saw a light from Heaven--brighter than the brightness of the sun--shining around me and around those who were travelling with me.
14 Wote tulipokuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, mbona unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.’
We all fell to the ground; and I heard a voice which said to me in Hebrew, "'Saul, Saul, why are you persecuting Me? You are finding it painful to kick against the ox-goad.'
15 “Nikauliza, ‘Ni nani wewe, Bwana?’ “Naye Bwana akajibu, ‘Ni Mimi Yesu unayemtesa.
"'Who art Thou, Lord?' I asked. "'I am Jesus whom you are persecuting,' the Lord replied.
16 Sasa inuka usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuteue uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeyaona, na yale nitakayokuonyesha.
'But rise, and stand on your feet; for I have appeared to you for the very purpose of appointing you My servant and My witness both as to the things you have already seen and as to those in which I will appear to you.
17 Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
I will save you from the Jewish people and from the Gentiles, to whom I send you to open their eyes,
18 uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
that they may turn from darkness to light and from the obedience to Satan to God, in order to receive forgiveness of sins and an inheritance among those who are sanctified through faith in Me.'
19 “Hivyo basi, Mfalme Agripa, sikuacha kuyatii yale maono yaliyotoka mbinguni,
"Therefore, King Agrippa, I was not disobedient to the heavenly vision;
20 bali niliyatangaza kwanza kwa wale wa Dameski, kisha Yerusalemu na katika vijiji vyote vya Uyahudi na pia kwa watu wa Mataifa, kwamba inawapasa kutubu na kumgeukia Mungu na kuthibitisha toba yao kwa matendo yao.
but I proceeded to preach first to the people in Damascus, and then to those in Jerusalem and in all Judaea, and to the Gentiles, that they must repent and turn to God, and live lives consistent with such repentance.
21 Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua.
"It was on this account that the Jews seized me in the Temple and tried to kill me.
22 Hadi leo nimepata msaada kutoka kwa Mungu, na hivyo nasimama hapa nikishuhudia kwa wakubwa na wadogo. Sisemi chochote zaidi ya yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia:
Having, however, obtained the help which is from God, I have stood firm until now, and have solemnly exhorted rich and poor alike, saying nothing except what the Prophets and Moses predicted as soon to happen,
23 kwamba Kristo atateswa, na kwamba yeye atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, na atatangaza nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.”
since the Christ was to be a suffering Christ, and by coming back from the dead was then to be the first to proclaim a message of light both to the Jewish people and to the Gentiles."
24 Paulo alipokuwa akifanya utetezi huu, Festo akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, wewe umerukwa na akili! Kusoma kwingi kunakufanya uwe kichaa!”
As Paul thus made his defence, Festus exclaimed in a loud voice, "You are raving mad, Paul; and great learning is driving you mad."
25 Lakini Paulo akajibu, “Mimi sijarukwa na akili, mtukufu sana Festo, bali nanena kweli nikiwa na akili zangu timamu.
"I am not mad, most noble Festus," replied Paul; "I am speaking words of sober truth.
26 Naam, Mfalme anajua kuhusu mambo haya yote, nami nasema naye kwa uhuru. Kwa sababu nina hakika kwamba hakuna hata mojawapo ya mambo haya asilolijua, kwa kuwa hayakufanyika mafichoni.
For the King, to whom I speak freely, knows about these matters. I am not to be persuaded that any detail of them has escaped his notice; for these things have not been done in a corner.
27 Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini.”
King Agrippa, do you believe the Prophets? I know that you believe them."
28 Agripa akamwambia Paulo, “Je, unanishawishi kwa haraka namna hii niwe Mkristo?”
Agrippa answered, "In brief, you are doing your best to persuade me to become a Christian."
29 Paulo akasema, “Ikiwa ni kwa haraka au la, namwomba Mungu, si wewe peke yako bali pia wale wote wanaonisikiliza leo, wawe kama mimi nilivyo, kasoro minyororo hii.”
"My prayer to God, whether briefly or at length," replied Paul, "would be that not only you but all who are my hearers to-day, might become such as I am--except these chains."
30 Baada ya kusema hayo, mfalme akainuka pamoja na mtawala na Bernike na wale waliokuwa wameketi pamoja nao.
So the King rose, and the Governor, and Bernice, and those who were sitting with them;
31 Walipokuwa wakiondoka, wakaambiana, “Mtu huyu hafanyi jambo lolote linalostahili kufa au kufungwa.”
and, having withdrawn, they talked to one another and said, "This man is doing nothing for which he deserves death or imprisonment."
32 Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeachwa huru kama hangekuwa amekata rufaa kwa Kaisari.”
And Agrippa said to Festus, "He might have been set at liberty, if he had not appealed to Caesar."

< Matendo 26 >