< Marko 16 >

1 Sabato ilipomalizika, Maria Magdalene, Maria mama yake Yakobo, na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu.
And when the sabbath was past Mary Magdalene, and Mary the mother of James, and Salome, bought spices in order to come and embalm Him:
2 Asubuhi na mapema, siku ya kwanza ya juma, mara tu baada ya kuchomoza jua, walikwenda kaburini.
and very early in the morning of the first day of the week they come to the sepulchre at sun-rising.
3 Njiani wakawa wanaulizana wao kwa wao, “Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe kutoka kwenye ingilio la kaburi?”
And they said to one another, Who will roll away the stone for us from the door of the sepulchre?
4 Lakini walipotazama, wakaona lile jiwe, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha kuvingirishwa kutoka pale penye ingilio la kaburi.
(but when they looked up, they saw that the stone was rolled away, ) for it was a very great one.
5 Walipokuwa wakiingia mle kaburini, wakamwona kijana mmoja aliyevaa joho jeupe akiwa ameketi upande wa kuume, nao wakastaajabu.
And they went into the sepulchre and saw a young man sitting on the right side, clothed in a long white robe; and they were affrighted:
6 Yule malaika akawaambia, “Msistaajabu. Mnamtafuta Yesu, Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa. Tazameni mahali walipomlaza.
but he said to them, Be not affrighted, ye seek Jesus of Nazareth, who was crucified, He is risen, He is not here, see the place where they laid Him.
7 Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake pamoja na Petro, kwamba, ‘Anawatangulia kwenda Galilaya. Huko ndiko mtamwona, kama alivyowaambia.’”
But go, tell his disciples, and Peter particularly, that He is going before you into Galilee: there ye will see Him, as He told you.
8 Hivyo wakatoka, wakakimbia kutoka mle kaburini wakiwa na hofu kuu na mshangao. Nao hawakumwambia mtu yeyote neno lolote, kwa sababu waliogopa.
And they hasted out and fled from the sepulchre; for they were seized with trembling and amazement: neither said they any thing to any one; for they were afraid.
9 (note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) Yesu alipofufuka alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma alimtokea kwanza Maria Magdalene, yule ambaye alikuwa amemtoa pepo wachafu saba.
(note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) Now Jesus being risen early on the first day of the week appeared first to Mary Magdalene, from whom He had cast out seven devils:
10 Maria akaenda, naye akawaambia wale waliokuwa wamefuatana na Yesu, waliokuwa wanaomboleza na kulia.
and she went and told those that used to be with Him, who were mourning and weeping;
11 Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria alikuwa amemwona, hawakusadiki.
but they, though they heard that He was indeed alive, and had been seen by her, did not believe it.
12 Baadaye Yesu akawatokea wawili miongoni mwa wanafunzi wake walipokuwa wakienda shambani akiwa katika sura nyingine.
After this He appeared in another form to two of them as they were walking, going into the country:
13 Nao wakarudi na kuwaambia wenzao. Lakini hawakuwasadiki wao pia.
and they went and told the rest; but they did not believe them neither.
14 Baadaye Yesu akawatokea wale wanafunzi kumi na mmoja walipokuwa wakila chakula. Akawakemea kwa kutoamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao kwa kutosadiki wale waliomwona baada yake kufufuka.
At last he appeared to the eleven as they were sitting at table, and upbraided them with their unbelief, and hardness of heart; because they did not believe those who had seen Him after He was risen.
15 Akawaambia, “Enendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
And He said unto them, Go to all the world and preach the gospel to every one:
16 Yeyote aaminiye na kubatizwa ataokoka. Lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa.
he that believeth and is baptized, shall be saved; but he that believeth not, shall be condemned.
17 Nazo ishara hizi zitafuatana na wanaoamini: Kwa Jina langu watatoa pepo wachafu; watasema kwa lugha mpya;
And these signs shall accompany them that believe; in my name shall they cast out demons, they shall speak with new tongues;
18 watashika nyoka kwa mikono yao; na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”
they shall take up serpents, and if they should drink any thing poisonous, it shall not hurt them; they shall lay hands on the sick, and they shall be well.
19 Baada ya Bwana Yesu kusema nao, alichukuliwa juu mbinguni na kuketi mkono wa kuume wa Mungu.
Now the Lord, after He had spoken to them, was taken up into heaven, and sat on the right hand of God.
20 Kisha wanafunzi wake wakatoka, wakahubiri kila mahali, naye Bwana akatenda kazi pamoja nao na kulithibitisha neno lake kwa ishara zilizofuatana nalo.]
And they went forth and preached every where, the Lord co-operating with them, and confirming the word by miracles following upon it. Amen.

< Marko 16 >