< Luka 6 >

1 Ikawa siku moja ya Sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya nafaka, nao wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke ya nafaka, wakayafikicha kwa mikono yao na kula punje zake.
And it came to pass on the second-sabbath after the first, that as He was passing through the corn-fields, his disciples plucked the ears of corn, and rubbed them in their hands and ate them.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya mambo yasiyo halali kufanywa siku ya Sabato?”
And some of the pharisees said to them, Why do ye do that which is not lawful to do on the sabbath-days?
3 Yesu akawajibu, “Je, ninyi hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa?
And Jesus answering them said, Have ye not read what David did, when he himself was hungry and those that were with him? how he went into the house of God,
4 Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akaichukua na kuila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
and did take and eat the shew-bread, and gave also to his attendants, which it is not lawful for any to eat but the priests.
5 Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
And He said unto them, the Son of man is Lord even of the sabbath.
6 Ikawa siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia ndani ya sinagogi na akawa anafundisha. Huko palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
And it came to pass also on another sabbath, that He went into a synagogue and taught; and there was a man there, whose right hand was withered.
7 Mafarisayo na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu. Kwa hivyo wakawa wanamwangalia sana ili waone kama ataponya katika siku ya Sabato.
And the scribes and pharisees watched Him to see if He would work a cure on the sabbath: that they might find an accusation against Him.
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, hivyo akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka usimame mbele ya watu wote.” Hivyo yule mtu akainuka, akasimama mbele yao wote.
But He knew their thoughts, and said to the man that had the withered hand, Rise, and stand in the midst: and he rose up and stood forth.
9 Ndipo Yesu akawaambia wale walimu wa sheria na Mafarisayo, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya Sabato? Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
Then said Jesus unto them, I will ask you one thing, Is it lawful on the sabbath days to do good, or to do evil? to save life, or to let it be lost?
10 Akawatazama watu wote waliokuwepo, kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukaponywa kabisa.
And looking round upon them all, He said to the man, Stretch out thine hand: and he did so, and his hand was made as sound as the other.
11 Wale wakuu wakakasirika sana, wakashauriana wao kwa wao ni nini watakachomtendea Yesu.
And they were filled with confusion: and consulted together, what they might do to Jesus.
12 Ikawa katika siku hizo Yesu alikwenda mlimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.
And in those days He went out to a mountain to pray, and He continued all night in prayer to God.
13 Kulipopambazuka, akawaita wanafunzi wake, naye akachagua kumi na wawili, ambao pia aliwaita mitume:
And when it was day, He called his disciples to Him: and chose out twelve from among them, whom He also named his apostles:
14 Simoni aliyemwita Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo,
(to wit, Simon called Peter, and Andrew his brother, James and John, Philip and Bartholomew,
15 Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni aliyeitwa Zelote,
Matthew and Thomas, James the son of Alpheus, and Simon called Zelotes, and Judas the brother of James,
16 Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote ambaye alikuwa msaliti.
and Judas Iscariot, who was the traitor: )
17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali penye uwanja tambarare. Hapo palikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu kutoka sehemu zote za Uyahudi, kutoka Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
and He came down the hill with them, and stood in the plain; with the rest of his disciples, and a great multitude of people from all the parts of Judea, and from Jerusalem, and from the coast of Tyre and Sidon, who came to hear Him and to be healed of their diseases,
18 Walikuwa wamekuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu akawaponya.
even those that were tormented by impure spirits: and they were healed.
19 Watu wote walikuwa wanajitahidi kumgusa kwa sababu nguvu zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.
And all the people endeavoured to touch Him, for there went a divine virtue out of Him, and healed them all.
20 Akawatazama wanafunzi wake, akasema: “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa sababu Ufalme wa Mungu ni wenu.
And lifting up his eyes on his disciples He said, Blessed are ye though poor; for the kingdom of God is yours.
21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.
Blessed are ye that hunger now; for ye shall be satisfied. Blessed are ye that weep now; for ye shall laugh.
22 Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia, watakapowatenga na kuwatukana na kulikataa jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
Blessed are ye when men shall hate you, and reject you, and reproach you, and cast out your name as infamous on account of the Son of man.
23 “Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.
Rejoice in that day, and be exceeding glad; for behold, your reward is great in heaven: for thus did their fathers to the prophets.
24 “Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, kwa sababu mmekwisha kupokea faraja yenu.
But wo unto you that are rich; for ye have received your consolation.
25 Ole wenu ninyi mlioshiba sasa, maana mtaona njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtaomboleza na kulia.
Wo unto you that are full; for ye shall be hungry. Wo unto you that laugh now: for ye shall mourn and weep.
26 Ole wenu watu watakapowasifu, kwani ndivyo baba zao walivyowasifu manabii wa uongo.
Wo unto you when all men speak well of you; for their fathers did the same to the false prophets.
27 “Lakini nawaambia ninyi mnaonisikia: Wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia.
But I say unto you my hearers, Love your enemies, do good to them that hate you,
28 Wabarikini wale wanaowalaani, waombeeni wale wanaowatendea mabaya.
bless them that curse you, and pray for them that abuse you;
29 Kama mtu akikupiga shavu moja, mgeuzie na la pili pia. Mtu akikunyangʼanya koti lako, usimzuie kuchukua joho pia.
to him that smiteth thee on the one cheek, offer also the other; and let him that taketh away thy cloke, have thy coat too rather than strive with him:
30 Mpe kila akuombaye, na kama mtu akichukua mali yako usitake akurudishie.
give to him that asketh thee, and from him that taketh thy goods on loan demand nothing.
31 Watendeeni wengine kama ambavyo mngetaka wawatendee ninyi.
And as ye would that men should do to you, do ye also to them in like manner.
32 “Kama mkiwapenda tu wale wanaowapenda, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwapenda wale wawapendao.
If ye love only them that love you, what thanks are due to you? for even the wicked love those that love them:
33 Tena mkiwatendea mema wale tu wanaowatendea ninyi mema, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ hufanya vivyo hivyo.
and if ye do good offices to them that do good to you, what thanks are due to you? for even wicked men do the same.
34 Tena mnapowakopesha wale tu mnaotegemea wawalipe, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwakopesha ‘wenye dhambi’ wenzao wakitarajia kulipwa mali yao yote.
And if ye lend to those from whom ye expect to receive, what thanks are due to you? for sinners also lend to sinners that they may receive an equivalent.
35 Lakini wapendeni adui zenu, watendeeni mema, wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo thawabu yenu itakapokuwa kubwa, nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu Sana, kwa sababu yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na kwa wale waovu.
But do ye love your enemies, and do good, and lend, expecting nothing from it: and your reward shall be great, and ye shall be the sons of the most High; for He is kind even to the ungrateful and the wicked:
36 Kuweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
be ye therefore merciful as your heavenly Father also is merciful.
37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa. Msilaumu, nanyi hamtalaumiwa. Sameheni, nanyi mtasamehewa.
Judge not, and ye shall not be judged: condemn not, and ye shall not be condemned: forgive, and ye shall be forgiven:
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”
give, and it shall be given unto you; good measure, pressed and shaken down and running over, shall they give into your bosom: for by the same measure, which ye measure with, shall it be measured back again to you.
39 Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu aweza kumwongoza kipofu? Je, wote wawili hawatatumbukia shimoni?
And He said to them by way of parable, Can a blind man guide a blind man? will they not both fall into a ditch?
40 Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu wake, ila yule aliyehitimu aweza kuwa kama mwalimu wake.
the learner is not above his teacher, tho' every complete scholar will become as learned as his master.
41 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
But why dost thou look at the chaff in thy brother's eye, and takest no notice of the beam that is in thine own?
42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, acha nitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako? Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
or how canst thou say to thy brother, Brother let me take out the splinter that is in thine eye, when thou thyself seest not the beam that is in thine own eye? Thou hypocrite, first take out the beam from thine own eye, and then thou wilt see distinctly how to take out the chaff that is in thy brother's eye.
43 “Hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
For that is not a good tree which produceth bad fruit, nor is the tree bad, which produceth good fruit:
44 Kila mti hujulikana kwa matunda yake. Kwa maana watu hawachumi tini kwenye miiba, wala zabibu kwenye michongoma.
for every tree is known by it's fruit; for men do not gather figs from thorns, nor grapes from a bramble.
45 Vivyo hivyo mtu mwema hutoa mambo mema kutoka kwenye hazina ya moyo wake, naye mtu mwovu hutoa mambo maovu kutoka kwenye hazina ya moyo wake. Kwa kuwa mtu hunena kwa kinywa chake yale yaliyoujaza moyo wake.
A good man, out of the good treasure of his heart, bringeth forth that which is good; and an evil man, out of the evil treasure of his heart, bringeth forth that which is evil: for out of the abundance of the heart his mouth speaketh.
46 “Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamfanyi ninayowaambia?
But why do ye call me, Lord, Lord, and do not practise what I teach you?
47 Nitawaonyesha jinsi alivyo mtu yule anayekuja kwangu na kusikia maneno yangu na kuyatenda.
Whosoever cometh unto me, and heareth my instructions, and observeth them, I will shew you to whom he is like:
48 Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba, akachimba chini sana, na kuweka msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipokuja, maji ya ghafula yaliipiga ile nyumba, lakini haikutikisika, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
he is like a man who in building an house digged deep, and laid the foundation upon a rock; and when a flood came, the torrent beat violently against that house, but could not shake it, for it was founded upon a rock.
49 Lakini yeye anayesikia maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ikaanguka mara na kubomoka kabisa.”
But he that heareth and observeth not, is like a man that built an house upon the ground without any foundation, which the flood beat violently upon, and immediately it fell down, and the ruin of that house was great.

< Luka 6 >