< Luka 1 >

1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
Whereas many have undertaken to compose a narrative of the things, which have been fully certified among us;
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
as they delivered them to us, who were from the beginning eye-witnesses of them, and ministers of the word;
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
it seemed good to me also, having thoroughly traced them all from the very first, to write an account of them in order to thee,
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
most excellent Theophilus, that thou mayst know the certainty of the things wherein thou hast been instructed.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
There was in the days of Herod king of Judea, a certain priest named Zacharias, of the course of Abia; and his wife was of the family of Aaron, and her name was Elisabeth.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
And they were both righteous in the sight of God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
And they had no child, for Elisabeth was barren; and they were both far advanced in years.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
And it came to pass, while he was in the order of his course performing the priest's office before God,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
according to the custom of dividing the office of the priests, that it fell to his lot to burn incense, entring into the temple of the Lord:
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
and all the people were praying without at the time of offering incense.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
And there appeared to him an angel of the Lord standing on the right hand of the altar of incense.
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
And when Zacharias saw him, he was startled and struck with fear:
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
but the angel said unto him, Fear not, Zacharias; for thy prayer is heard, and thy wife Elisabeth shall bear thee a son, and thou shalt call his name John:
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
and he shall be a joy and transport to thee, yea, many shall rejoice on account of his birth; for he shall be great in the sight of the Lord,
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
and he shall drink neither wine nor any other strong liquor; and he shall be filled with the holy Spirit even from his birth;
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
and many of the children of Israel shall he convert unto the Lord their God.
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
And he shall go before Him in the spirit and power of Elias, to turn the hearts of the fathers unto the children, and the disobedient to the wisdom of the just, to prepare for the Lord a people well-disposed.
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
And Zacharias said unto the angel, Whereby shall I know this? for I am an old man, and my wife far advanced in years.
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
And the angel answering said to him, I am Gabriel, that stand in the presence of God, and I am sent to speak to thee, and to tell thee this good news:
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
and now shalt thou be dumb, and not able to speak, until the day that these things shall come to pass; because thou believedst not my words, which shall be fulfilled at their season.
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
And the people were waiting for Zacharias, and wondered at his staying so long in the temple:
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
but when he came out he could not speak to them, and they perceived that he had seen a vision in the temple; and he made signs to them, and continued speechless:
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
and as soon as the days of his ministration were accomplished, he departed to his own house.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
And after these days his wife Elisabeth conceived, and retired five months,
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
saying, the Lord hath thus dealt with me in the days wherein he looked upon me to take away my reproach among men.
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
But in the sixth month the angel Gabriel was sent by God to a city of Galilee called Nazareth,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
to a virgin who was betrothed to a man, whose name was Joseph, of the house of David; and the name of the virgin was Mary.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
And when the angel came in to the room to her, he said, Hail, thou that art highly favoured; the Lord is with thee;
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
blessed art thou among women! and when she saw him, she was confused at what he said, and pondered in her mind what sort of salutation this could be.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
And the angel said unto her, Fear not, Mary; for thou hast found favor with God:
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
and behold thou shalt conceive in thy womb, and shalt bring forth a son, and shalt call his name JESUS:
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
He shall be great, and shall be called the Son of the Most High, and the Lord God shall give Him the throne of David his father,
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
and He shall reign over the house of Jacob for ever, and of his kingdom there shall be no end. (aiōn g165)
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
Then said Mary to the angel, How can this be, since I am a virgin?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
And the angel answered and said unto her, The holy Spirit shall come upon thee, and the power of the Most High shall overshadow thee, and therefore thine holy offspring shall be called the Son of God: and lo,
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
thy cousin Elisabeth also hath conceived a son in her old age, and this is the sixth month with her that was called barren;
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
for nothing is impossible with God.
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
Then Mary said, Behold the servant of the Lord, may it be unto me according to thy word. So the angel departed from her.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
Then Mary arose and went with speed into the hill-country, to a city of Juda,
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
and came into the house of Zacharias, and saluted Elisabeth.
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
And as soon as Elisabeth heard the salutation of Mary, the child leaped in her womb, and Elisabeth was filled with the holy Spirit:
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
and she cried out with a loud voice, and said, Blessed art thou among women, and blessed is the fruit of thy womb:
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
and whence is this honor to me, that the mother of my Lord should come to me?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
for behold, as soon as the voice of thy salutation reached my ears, the child in my womb leaped for joy:
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
and blessed is she that believed; for there shall be a performance of the things that were told her from the Lord.
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
And Mary said, "My soul doth magnify the Lord, and my spirit hath rejoiced in God my Saviour;
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
for He hath regarded the low estate of his handmaid:
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
for behold, from henceforth shall all generations call me blessed:
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
for He that is mighty hath done great things for me,
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
and his name is holy, and his mercy is on them that fear Him, unto all generations.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
He hath wrought powerfully with his arm; He hath confounded those that were proud in the imagination of their heart.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
He hath cast down the mighty from their thrones, and exalted the humble.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
He hath filled the hungry with good things, and the rich He hath sent away empty.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
He hath supported Israel his servant,
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
in remembrance of his mercy (even as He promised to our fathers, to Abraham and to his seed, ) for ever." (aiōn g165)
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
And Mary stayed with her about three months, and then returned to her own house.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
Now when Elisabeth's time for her delivery was fully come, she brought forth a son:
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
and her neighbours and kindred heard that the Lord had magnified his mercy towards her, and they congratulated her;
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
and on the eighth day they came to circumcise the child: and they would have called him Zacharias, after the name of his father:
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
but his mother said, No, but he shall be called John:
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
and they said to her, There is none of thy relations of this name.
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
And they made signs to his father, what name he would have him called by.
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
And he called for a writing-tablet, and wrote upon it, His name is John: and they all wondered.
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
And his mouth was opened immediately, and his tongue loosed, and he spake and praised God.
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
And an awe fell upon all that dwelt round about them; and all these things were divulged through the whole hill-country of Judea.
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
And all that heard them, laid them up in their hearts, saying, What a child will this be? And the hand of the Lord was with him.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
And his father Zacharias was filled with the holy Spirit,
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
and prophesied, saying, "Blessed be the Lord God of Israel, for He hath visited and wrought redemption for his people,
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
and hath raised up an horn of salvation for us,
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
in the house of his servant David, as He spake by the mouth of his holy prophets from the beginning, (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
even salvation from our enemies, and from the hand of all that hate us,
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
to display his mercy towards our fathers, and to remember his holy covenant,
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
according to the oath which He sware to Abraham our father,
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
to grant unto us, that we being delivered out of the hand of our enemies, might serve Him without fear, in holiness and righteousness before Him,
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
all the days of our life.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
And thou, my child, shalt be called the prophet of the most High; for thou shalt go before the face of the Lord,
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
to make known salvation to his people,
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
in the remission of their sins, through the tender mercy of our God, whereby the day-spring hath visited us from on high,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
to enlighten them that sit in darkness and in the shadow of death, to direct our feet into the way of peace."
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
And the child grew, and became strong in spirit: and he was in the deserts till the time of his being manifested to Israel.

< Luka 1 >