< Yohana 21 >

1 Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
After this, Jesus again showed Himself to the disciples. It was at the Lake of Tiberias. The circumstances were as follows.
2 Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
Simon Peter was with Thomas, called the Twin, Nathanael of Cana in Galilee, the sons of Zabdi, and two others of the Master's disciples.
3 Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
Simon Peter said to them, "I am going fishing." "We will go too," said they. So they set out and went on board their boat; but they caught nothing that night.
4 Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
When, however, day was now dawning, Jesus stood on the beach, though the disciples did not know that it was Jesus.
5 Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
He called to them. "Children," He said, "have you any food there?" "No," they answered.
6 Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
"Throw the net in on the right hand side," He said, "and you will find fish." So they threw the net in, and now they could scarcely drag it along for the quantity of fish.
7 Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
This made the disciple whom Jesus loved say to Peter, "It is the Master." Simon Peter therefore, when he heard the words, "It is the Master," drew on his fisherman's shirt--for he had not been wearing it--put on his girdle, and sprang into the water.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
But the rest of the disciples came in the small boat (for they were not far from land--only about a hundred yards off), dragging the net full of fish.
9 Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
As soon as they landed, they saw a charcoal fire burning there, with fish broiling on it, and bread close by.
10 Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
Jesus told them to fetch some of the fish which they had just caught.
11 Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
So Simon Peter went on board the boat and drew the net ashore full of large fish, 153 in number; and yet, although there were so many, the net had not broken.
12 Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
"Come this way and have breakfast," said Jesus. But not one of the disciples ventured to question Him as to who He was, for they felt sure that it was the Master.
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
Then Jesus came and took the bread and gave them some, and the fish in the same way.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
This was now the third occasion on which Jesus showed Himself to the disciples after He had risen from among the dead.
15 Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
When they had finished breakfast, Jesus asked Simon Peter, "Simon, son of John, do you love me more than these others do?" "Yes, Master," was his answer; "you know that you are dear to me." "Then feed my lambs," replied Jesus.
16 Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
Again a second time He asked him, "Simon, son of John, do you love me?" "Yes, Master," he said, "you know that you are dear to me." "Then be a shepherd to my sheep," He said.
17 Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
A third time Jesus put the question: "Simon, son of John, am I dear to you?" It grieved Peter that Jesus asked him the third time, "Am I dear to you?" "Master," he replied, "you know everything, you can see that you are dear to me." "Then feed my much-loved sheep," said Jesus.
18 Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
"In most solemn truth I tell you that whereas, when you were young, you used to put on your girdle and walk whichever way you chose, when you have grown old you will stretch out your arms and some one else will put a girdle round you and carry you where you have no wish to go."
19 Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
This He said to indicate the kind of death by which that disciple would bring glory to God; and after speaking thus He said to him, "Follow me."
20 Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
Peter turned round and noticed the disciple whom Jesus loved following--the one who at the supper had leaned back on His breast and had asked, "Master, who is it that is betraying you?"
21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
On seeing him, Peter asked Jesus, "And, Master, what about him?"
22 Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
"If I desire him to remain till I come," replied Jesus, "what concern is that of yours? You, yourself, must follow me."
23 Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
Hence the report spread among the brethren that that disciple would never die. Yet Jesus did not say, "He is not to die," but, "If I desire him to remain till I come, what concern is that of yours?"
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
That is the disciple who gives his testimony as to these matters, and has written this history; and we know that his testimony is true.
25 Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.
But there are also many other things which Jesus did--so vast a number indeed that if they were all described in detail, I suppose that the world itself could not contain the books that would have to be written.

< Yohana 21 >