< Yohana 20 >

1 Alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma, kulipokuwa kungali giza bado, Maria Magdalene alikwenda kaburini na kukuta lile jiwe limeondolewa penye ingilio.
On the first day of the week, very early, while it was still dark, Mary of Magdala came to the tomb and saw that the stone had been removed from it.
2 Hivyo akaja akikimbia kwa Simoni Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, na kusema, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na hatujui walikomweka!”
So she ran, as fast as she could, to find Simon Peter and the other disciple--the one who was dear to Jesus--and to tell them, "They have taken the Master out of the tomb, and we do not know where they have put Him."
3 Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaondoka mara kuelekea kaburini.
Peter and the other disciple started at once to go to the tomb, both of them running,
4 Wote wawili walikuwa wanakimbia, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
but the other disciple ran faster than Peter and reached it before he did.
5 Alipofika, akainama na kuchungulia mle kaburini, akaona vile vitambaa vya kitani mle ndani, lakini hakuingia.
Stooping and looking in, he saw the linen cloths lying there on the ground, but he did not go in.
6 Ndipo Simoni Petro akaja, akimfuata nyuma akaenda moja kwa moja hadi ndani ya kaburi. Naye akaona vile vitambaa vya ile sanda vikiwa pale chini
Simon Peter, however, also came, following him, and entered the tomb. There on the ground he saw the cloths;
7 na kile kitambaa kilichokuwa kichwani mwa Yesu. Kitambaa hicho kilikuwa kimekunjwa mahali pa peke yake, mbali na vile vitambaa vya kitani vya ile sanda.
and the towel, which had been placed over the face of Jesus, not lying with the cloths, but folded up and put by itself.
8 Kisha yule mwanafunzi aliyetangulia kufika kaburini naye akaingia ndani, akaona, akaamini,
Then the other disciple, who had been the first to come to the tomb, also went in and saw and was convinced.
9 (kwa kuwa mpaka wakati huo walikuwa bado hawajaelewa kutoka Maandiko kwamba ilikuwa lazima Yesu afufuke kutoka kwa wafu).
For until now they had not understood the inspired teaching, that He must rise again from among the dead.
10 Kisha hao wanafunzi wakaondoka wakarudi nyumbani kwao.
Then they went away and returned home.
11 Lakini Maria Magdalene akasimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama, kuchungulia mle kaburini,
Meanwhile Mary remained standing near the tomb, weeping aloud. She did not enter the tomb, but as she wept she stooped and looked in,
12 naye akaona malaika wawili wamevaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja upande wa kichwani na mwingine upande wa miguuni.
and saw two angels clothed in white raiment, sitting one at the head and one at the feet where the body of Jesus had been.
13 Wakamuuliza Maria, “Mwanamke, mbona unalia?” Akawaambia, “Nalia kwa kuwa wamemchukua Bwana wangu na sijui walikomweka.”
They spoke to her. "Why are you weeping?" they asked. "Because," she replied, "they have taken away my Lord, and I do not know where they have put him."
14 Baada ya kusema hayo, akageuka, akamwona Yesu amesimama, lakini hakumtambua.
While she was speaking, she turned round and saw Jesus standing there, but did not recognize Him.
15 Yesu akamwambia, “Mwanamke, mbona unalia? Unamtafuta nani?” Maria akidhani ya kuwa aliyekuwa anaongea naye ni mtunza bustani, kwa hiyo akamwambia, “Bwana, kama ni wewe umemchukua, tafadhali nionyeshe ulikomweka, nami nitamchukua.”
"Why are you weeping?" He asked; "who are you looking for?" She, supposing that He was the gardener, replied, "Sir, if you have carried him away, tell me where you have put him and I will remove him."
16 Yesu akamwita, “Maria!” Ndipo Maria akamgeukia Yesu na kusema naye kwa Kiebrania, “Rabboni!” (maana yake Mwalimu).
"Mary!" said Jesus. She turned to Him. "Rabboni!" she cried in Hebrew: the word means 'Teacher!'
17 Yesu akamwambia, “Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’”
"Do not cling to me," said Jesus, "for I have not yet ascended to the Father. But take this message to my brethren: 'I am ascending to my Father and your Father, to my God and your God.'"
18 Kwa hiyo Maria Magdalene akaenda kuwatangazia wanafunzi wa Yesu, akisema, “Nimemwona Bwana!” Naye akawaambia kwamba Yesu alikuwa amemweleza mambo hayo yote.
Mary of Magdala came and brought word to the disciples. "I have seen the Master," she said. And she told them that He had said these things to her.
19 Ikawa jioni ya ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi wake walikuwa pamoja, milango ikiwa imefungwa kwa kuwaogopa Wayahudi. Naye Yesu aliwatokea, akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
On that same first day of the week, when it was evening and, for fear of the Jews, the doors of the house where the disciples were, were locked, Jesus came and stood in their midst, and said to them, "Peace be to you!"
20 Baada ya kusema haya, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Wanafunzi wake wakafurahi sana walipomwona Bwana.
Having said this He showed them His hands and also His side; and the disciples were filled with joy at seeing the Master.
21 Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi! Kama vile Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawatuma ninyi.”
A second time, therefore, He said to them, "Peace be to you! As the Father sent me, I also now send you."
22 Naye alipokwisha kusema haya, akawavuvia, akawaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
Having said this He breathed upon them and said, "Receive the Holy Spirit.
23 Mkimwondolea mtu yeyote dhambi zake, zitaondolewa, na yeyote msiyemwondolea dhambi zake, hazitaondolewa.”
If you remit the sins of any persons, they remain remitted to them. If you bind fast the sins of any, they remain bound."
24 Lakini Tomaso, aliyeitwa Didimasi, yaani Pacha, mmoja wa wale kumi na wawili, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja.
Thomas, one of the twelve--surnamed 'the Twin' --was not among them when Jesus came.
25 Hivyo wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Lakini yeye akawaambia, “Nisipoona zile alama za misumari mikononi mwake, na kuweka kidole changu kwenye hizo alama za misumari na mkono wangu ubavuni mwake, sitaamini.”
So the rest of the disciples told him, "We have seen the Master!" His reply was, "Unless I see in his hands the wound made by the nails and put my finger into the wound, and put my hand into his side, I will never believe it."
26 Baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwa tena pamoja ndani ya nyumba, naye Tomaso alikuwa pamoja nao. Ndipo Yesu akaja milango ikiwa imefungwa na kusimama katikati yao akasema, “Amani iwe nanyi.”
A week later the disciples were again in the house, and Thomas was with them, when Jesus came--though the doors were locked--and stood in their midst, and said, "Peace be to you."
27 Kisha akamwambia Tomaso, “Weka kidole chako hapa na uone mikono yangu, nyoosha mkono wako uguse ubavuni mwangu. Usiwe na shaka, bali uamini tu.”
Then He said to Thomas, "Bring your finger here and feel my hands; bring you hand and put it into my side; and do not be ready to disbelieve but to believe."
28 Tomaso akamwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
"My Lord and my God!" replied Thomas.
29 Yesu akamwambia, “Umeamini kwa kuwa umeniona? Wamebarikiwa wale ambao hawajaona lakini wameamini.”
"Because you have seen me," replied Jesus, "you have believed. Blessed are those who have not seen and yet have believed."
30 Yesu alifanya miujiza mingine mingi mbele za wanafunzi wake, ambayo haikuandikwa katika kitabu hiki.
There were also a great number of other signs which Jesus performed in the presence of the disciples, which are not recorded in this book.
31 Lakini haya yameandikwa ili mweze kuamini ya kuwa Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mpate uzima katika jina lake.
But these have been recorded in order that you may believe that He is the Christ, the Son of God, and that, through believing, you may have Life through His name.

< Yohana 20 >