< Yohana 13 >

1 Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.
Now just before the Feast of the Passover this incident took place. Jesus knew that the time had come for Him to leave this world and go to the Father; and having loved His own who were in the world, He loved them to the end.
2 Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu.
While supper was proceeding, the Devil having by this time suggested to Judas Iscariot, the son of Simon, the thought of betraying Him, Jesus,
3 Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
although He knew that the Father had put everything into His hands, and that He had come forth from God and was now going to God,
4 hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
rose from the table, threw off His upper garments, and took a towel and tied it round Him.
5 Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
Then He poured water into a basin, and proceeded to wash the feet of the disciples and to wipe them with the towel which He had put round Him.
6 Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
When He came to Simon Peter, Peter objected. "Master," he said, "are you going to wash my feet?"
7 Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
"What I am doing," answered Jesus, "for the present you do not know, but afterwards you shall know."
8 Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn g165)
"Never, while the world lasts," said Peter, "shall you wash my feet." "If I do not wash you," replied Jesus, "you have no share with me." (aiōn g165)
9 Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
"Master," said Peter, "wash not only my feet, but also my hands and my head."
10 Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
"Any one who has lately bathed," said Jesus, "does not need to wash more than his feet, but is clean all over. And you my disciples are clean, and yet this is not true of all of you."
11 Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
For He knew who was betraying Him, and that was why He said, "You are not all of you clean."
12 Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
So after He had washed their feet, put on His garments again, and returned to the table, He said to them, "Do you understand what I have done to you?
13 Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
You call me 'The Rabbi' and 'The Master,' and rightly so, for such I am.
14 Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
If I then, your Master and Rabbi, have washed your feet, it is also your duty to wash one another's feet.
15 Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
For I have set you an example in order that you may do what I have done to you.
16 Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
In most solemn truth I tell you that a servant is not superior to his master, nor is a messenger superior to him who sent him.
17 Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.
If you know all this, blessed are you if you act accordingly.
18 “Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
I am not speaking of all of you. I know whom I have chosen, but things are as they are in order that the Scripture may be fulfilled, which says, 'He who eats my bread has lifted up his heel against me.'
19 “Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
From this time forward I tell you things before they happen, in order that when they do happen you may believe that I am He.
20 Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
In most solemn truth I tell you that he who receives whoever I send receives me, and that he who receives me receives Him who sent me."
21 Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
After speaking thus Jesus was troubled in spirit and said with deep earnestness, "In most solemn truth I tell you that one of you will betray me."
22 Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
The disciples began looking at one another, at a loss to know to which of them He was referring.
23 Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu.
There was at table one of His disciples--the one Jesus loved-- reclining with his head on Jesus's bosom.
24 Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
Making a sign therefore to him, Simon Peter said, "Tell us to whom he is referring."
25 Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
So he, having his head on Jesus's bosom, leaned back and asked, "Master, who is it?"
26 Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
"It is the one," answered Jesus, "for whom I shall dip this piece of bread and to whom I shall give it." Accordingly He dipped the piece of bread, and took it and gave it to Judas, the son of the Iscariot Simon.
27 Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.”
Then, after Judas had received the piece of bread, Satan entered into him. "Lose no time about it," said Jesus to him.
28 Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo.
But why He said this no one else at the table understood.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote.
Some, however, supposed that because Judas had the money-box Jesus meant, "Buy what we require for the Festival," or that he should give something to the poor.
30 Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
So Judas took the piece of bread and immediately went out. And it was night.
31 Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
So when he was gone out, Jesus said, "Now is the Son of Man glorified, and God is glorified in Him.
32 Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.
Moreover God will glorify Him in Himself, and will glorify Him without delay.
33 “Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.
Dear children, I am still with you a little longer. You will seek me, but, as I said to the Jews, 'Where I am going you cannot come,' so for the present I say to you.
34 “Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
A new commandment I give you, to love one another; that as I have loved you, you also may love one another.
35 Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
It is by this that every one will know that you are my disciples--if you love one another."
36 Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
"Master," inquired Simon Peter, "where are you going?" "Where I am going," replied Jesus, "you cannot be my follower now, but you shall be later."
37 Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
"Master," asked Peter again, "why cannot I follow you now? I will lay down my life on your behalf.
38 Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
"You say you will lay down your life on my behalf!" said Jesus; "in most solemn truth I tell you that the cock will not crow before you have three times disowned me."

< Yohana 13 >