< Wagalatia 1 >

1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
Paul, an Apostle sent not from men nor by any man, but by Jesus Christ and by God the Father, who raised Jesus from among the dead--
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
and all the brethren who are with me: To the Churches of Galatia.
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
May grace and peace be granted to you from God the Father, and from our Lord Jesus Christ,
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
who gave Himself to suffer for our sins in order to rescue us from the present wicked age in accordance with the will of our God and Father. (aiōn g165)
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
To Him be the glory to the Ages of the Ages! Amen. (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
I marvel that you are so readily leaving Him who called you by the grace of Christ, and are adhering to a different Good News.
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
For other "Good News" there is none; but there are some persons who are troubling you, and are seeking to distort the Good News concerning Christ.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
But if even we or an angel from Heaven should bring you a Good News different from that which we have already brought you, let him be accursed.
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
What I have just said I repeat--if any one is preaching to you a Good News other than that which you originally received, let him be accursed.
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
For is it man's favour or God's that I aspire to? Or am I seeking to please men? If I were still a man-pleaser, I should not be Christ's bondservant.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
For I must tell you, brethren, that the Good News which was proclaimed by me is not such as man approves of.
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
For, in fact, it was not from man that I received or learnt it, but by a revelation from Jesus Christ.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
For you have heard of my early career in Judaism--how I furiously persecuted the Church of God, and made havoc of it;
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
and how in devotion to Judaism I outstripped many men of my own age among my people, being far more zealous than they on behalf of the traditions of my forefathers.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
But when He who set me apart even from my birth, and called me by His grace,
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
saw fit to reveal His Son within me in order that I might tell among the Gentiles the Good News concerning Him, at once I did not confer with any human being,
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
nor did I go up to Jerusalem to those who were my seniors in the Apostleship, but I went away into Arabia, and afterwards came back to Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Then, three years later, I went up to Jerusalem to inquire for Peter, and I spent a fortnight with him.
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
I saw none of the other Apostles, except James, the Lord's brother.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
In making these assertions I am speaking the truth, as in the sight of God.
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
Afterwards I visited Syria and Cilicia.
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
But to the Christian Churches in Judaea I was personally unknown.
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
They only heard it said, "He who was once our persecutor is now telling the Good News of the faith of which he formerly made havoc."
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
And they gave glory to God on my account.

< Wagalatia 1 >