< 2 Wakorintho 13 >

1 Hii ndiyo mara ya tatu mimi kuja kwenu. “Shtaka lolote lazima lithibitishwe na mashahidi wawili au watatu.”
This intended visit of mine is my third visit to you. "On the evidence of two or three witnesses every charge shall be sustained."
2 Nimekwisha kuwaonya nilipokuwa pamoja nanyi mara ya pili. Sasa narudia wakati sipo, kwamba nikija tena sitawahurumia wale waliokuwa wametenda dhambi hapo awali na wengine wote,
Those who cling to their old sins, and indeed all of you, I have forewarned and still forewarn (as I did on my second visit when present, so I do now, though absent) that, when I come again, I shall not spare you;
3 kwa kuwa mnadai uthibitisho kwamba Kristo anazungumza kwa kunitumia mimi. Yeye si dhaifu katika kushughulika nanyi, bali ana nguvu kati yenu.
since you want a practical proof of the fact that Christ speaks by my lips--He who is not feeble towards you, but powerful among you.
4 Kwa kuwa alisulubiwa katika udhaifu, lakini anaishi kwa nguvu za Mungu. Vivyo hivyo, sisi tu dhaifu kupitia kwake, lakini katika kuwashughulikia ninyi tutaishi pamoja naye kwa nguvu za Mungu.
For though it is true that He was crucified through weakness, yet He now lives through the power of God. We also are weak, sharing His weakness, but with Him we shall be full of life to deal with you through the power of God.
5 Jichunguzeni wenyewe mwone kama mnaishi katika imani. Jipimeni wenyewe. Je, hamtambui ya kuwa Yesu Kristo yumo ndani yenu? Kama sivyo, basi, mmeshindwa kufikia kipimo hicho!
Test yourselves to discover whether you are true believers: put your own selves under examination. Or do you not know that Jesus Christ is within you, unless you are insincere?
6 Natumaini mtaona kuwa sisi hatukushindwa.
But I trust that you will recognize that we are not insincere.
7 Lakini tunamwomba Mungu msije mkatenda kosa lolote, si ili sisi tuonekane kuwa tumeshinda hilo jaribio, bali ili ninyi mtende lililo haki, hata kama tutaonekana kuwa tumeshindwa.
And our prayer to God is that you may do nothing wrong; not in order that our sincerity may be demonstrated, but that you may do what is right, even though our sincerity may seem to be doubtful.
8 Kwa maana hatuwezi kufanya lolote kinyume na kweli, bali kuithibitisha kweli tu.
For we have no power against the truth, but only for the furtherance of the truth;
9 Tunafurahi wakati wowote sisi tunapokuwa dhaifu, lakini ninyi mkawa na nguvu. Nayo maombi yetu ni kwamba mpate kuwa wakamilifu.
and it is a joy to us when we are powerless, but you are strong. This we also pray for--the perfecting of your characters.
10 Hii ndiyo sababu nawaandikia mambo haya wakati sipo, ili nikija nisiwe mkali katika kutumia mamlaka yangu, mamlaka Bwana aliyonipa ya kuwajenga ninyi wala si ya kuwabomoa.
For this reason I write thus while absent, that when present I may not have to act severely in the exercise of the authority which the Lord has given me for building up, and not for pulling down.
11 Hatimaye, ndugu zangu, kwaherini. Kuweni wakamilifu, mkafarijike, kuweni wa nia moja, kaeni kwa amani. Naye Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.
Finally, brethren, be joyful, secure perfection of character, take courage, be of one mind, live in peace. And then God who gives love and peace will be with you.
12 Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu.
Salute one another with a holy kiss.
13 Watakatifu wote wanawasalimu.
All God's people here send greetings to you.
14 Neema ya Bwana Yesu Kristo, na upendo wa Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote. Amen.
May the grace of the Lord Jesus Christ, the love of God, and the fellowship of the Holy Spirit, be with you all.

< 2 Wakorintho 13 >