< 2 Wakorintho 12 >

1 Yanipasa nijisifu, ingawa haifaidi kitu. Nitaenda kwenye maono na ufunuo kutoka kwa Bwana.
I am compelled to boast. It is not a profitable employment, but I will proceed to visions and revelations granted me by the Lord.
2 Namjua mtu mmoja katika Kristo ambaye miaka kumi na minne iliyopita alichukuliwa juu hadi mbingu ya tatu. Kama ni katika mwili au nje ya mwili, sijui, Mungu ajua.
I know a Christian man who fourteen years ago-- whether in the body I do not know, or out of the body I do not know; God knows--was caught up (this man of whom I am speaking) even to the highest Heaven.
3 Nami najua ya kwamba mtu huyu, kwamba ni katika mwili au nje ya mwili mimi sijui, lakini Mungu ajua,
And I know that this man-- whether in the body or apart from the body I do not know;
4 alinyakuliwa hadi Paradiso. Huko alisikia mambo yasiyoelezeka, mambo ambayo binadamu hana ruhusa ya kuyasimulia.
God knows--was caught up into Paradise and heard unspeakable things which no human being is permitted to repeat.
5 Nitajisifu kwa ajili ya mtu kama huyo, lakini sitajisifu kuhusu mimi mwenyewe ila mimi nitajisifia udhaifu wangu.
Of such a one I will boast; but of myself I will not boast, except in my weaknesses.
6 Hata kama ningependa kujisifu, sitakuwa mjinga, kwa maana nitakuwa nasema kweli. Lakini najizuia, ili mtu yeyote asije akaniona mimi kuwa bora zaidi kuliko ninavyoonekana katika yale ninayotenda na kusema.
If however I should choose to boast, I should not be a fool for so doing, for I should be speaking the truth. But I forbear, lest any one should be led to estimate me more highly than what his own eyes attest, or more highly than what he hears from my lips.
7 Ili kunizuia nisijivune kwa sababu ya ufunuo huu mkuu, nilipewa mwiba katika mwili wangu, mjumbe wa Shetani, ili anitese.
And judging by the stupendous grandeur of the revelations--therefore lest I should be over-elated there has been sent to me, like the agony of impalement, Satan's angel dealing blow after blow, lest I should be over-elated.
8 Kwa habari ya jambo hili nilimsihi Bwana mara tatu aniondolee mwiba huu.
As for this, three times have I besought the Lord to rid me of him;
9 Lakini aliniambia, “Neema yangu inakutosha, kwa kuwa uweza wangu hukamilika katika udhaifu.” Kwa hiyo nitajisifu kwa furaha zaidi kuhusu udhaifu wangu, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
but His reply has been, "My grace suffices for you, for power matures in weakness." Most gladly therefore will I boast of my infirmities rather than complain of them--in order that Christ's power may overshadow me.
10 Hii ndiyo sababu, kwa ajili ya Kristo, nafurahia udhaifu, katika kutukanwa, katika taabu, katika mateso na katika shida, kwa maana ninapokuwa dhaifu, ndipo nina nguvu.
In fact I take pleasure in infirmities, in the bearing of insults, in distress, in persecutions, in grievous difficulties--for Christ's sake; for when I am weak, then I am strong.
11 Nimekuwa mjinga, lakini ninyi mmenilazimisha niwe hivyo. Kwa kuwa ilinipasa kusifiwa na ninyi, kwa sababu mimi si dhalili kuliko wale “mitume walio bora,” ingawa mimi si kitu.
It is foolish of me to write all this, but you have compelled me to do so. Why, you ought to have been my vindicators; for in no respect have I been inferior to these superlatively great Apostles, even though in myself I am nothing.
12 Mambo yanayomtambulisha mtume wa kweli, yaani, ishara, miujiza na maajabu, yalifanywa miongoni mwenu kwa saburi nyingi.
The signs that characterize the true Apostle have been done among you, accompanied by unwearied fortitude, and by tokens and marvels and displays of power.
13 Je, ninyi ni kitu gani mlichopungukiwa kuliko makanisa mengine, ila tu kwamba mimi sikuwa mzigo kwenu? Nisameheni kwa kosa hili!
In what respect, therefore, have you been worse dealt with than other Churches, except that I myself never hung as a dead weight upon you? Forgive the injustice I thus did you!
14 Sasa niko tayari kuja kwenu kwa mara hii ya tatu, nami sitawalemea, kwa sababu sitahitaji chochote chenu, ila ninawahitaji ninyi, kwa kuwa hata hivyo watoto hawaweki akiba kwa ajili ya wazazi wao, bali wazazi huweka akiba kwa ajili ya watoto wao.
See, I am now for the third time prepared to visit you, but I will not be a dead weight to you. I desire not your money, but yourselves; for children ought not to put by for their parents, but parents for their children.
15 Hivyo nitafurahi kutumia kila kitu nilicho nacho kwa ajili yenu, hata mwili wangu pia. Hata ingawa inaonekana ninavyozidi kuwapenda, ndivyo upendo wenu kwangu unavyopungua.
And as for me, most gladly will I spend all I have and be utterly spent for your salvation.
16 Iwe iwavyo, kwa vyovyote vile mimi sikuwalemea. Lakini kwa mimi kuwa mwerevu naliwapata.
If I love you so intensely, am I the less to be loved? Be that as it may: I was not a burden to you. But being by no means scrupulous, I entrapped you, they say!
17 Je, nilijipatia faida kwa kumtumia mtu yeyote niliyemtuma kwenu?
Have I gained any selfish advantage over you through any one of the messengers I have sent to you?
18 Nilimshawishi Tito aje kwenu, nami nilimtuma pamoja na ndugu yetu. Je, Tito aliwatumia ninyi ili kujipatia faida? Je, hatuenendi kwa roho moja, na hatuchukui hatua zile zile?
I begged Titus to visit you, and sent our other brother with him. Did Titus gain any selfish advantage over you? Were not he and I guided by one and the same Spirit, and did we not walk in the same steps?
19 Je, mmekuwa mkifikiri kwamba sisi tunajaribu kujitetea mbele yenu? Sisi tumekuwa tukinena mbele za Mungu kama wale walio katika Kristo. Na chochote tufanyacho, ndugu wapendwa, ni kwa ajili ya kuwatia nguvu.
You are imagining, all this time, that we are making our defense at your bar. In reality it is as in God's presence and in communion with Christ that we speak; but, dear friends, it is all with a view to your progress in goodness.
20 Kwa kuwa nina hofu ya kwamba nitakapokuja naweza kuwakuta nisivyotaka, nanyi mkanikuta msivyotaka. Nina hofu kwamba panaweza kuwa na ugomvi, wivu, ghadhabu, fitina, masingizio, masengenyo, majivuno na machafuko.
For I am afraid that perhaps when I come I may not find you to be what I desire, and that you may find me to be what you do not desire; that perhaps there may be contention, jealousy, bitter feeling, party spirit, ill-natured talk, backbiting, undue eulogy, unrest;
21 Nina hofu kwamba nitakapokuja tena kwenu, Mungu wangu atanidhili mbele yenu, nami nitasikitishwa na wengi waliotenda dhambi mbeleni, na wala hawajatubu kwa uchafu wao, uasherati, na ufisadi walioushiriki.
and that upon re-visiting you I may be humbled by my God in your presence, and may have to mourn over many whose hearts still cling to their old sins, and who have not repented of the impurity, fornication, and gross sensuality, of which they have been guilty.

< 2 Wakorintho 12 >