< Wagalatia 2 >

1 Kisha, baada ya miaka kumi na minne, nilipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba, nikamchukua na Tito ili awe pamoja nami.
Later still, after an interval of fourteen years, I again went up to Jerusalem in company with Barnabas, taking Titus also with me.
2 Nilikwenda kwa sababu nilikuwa nimefunuliwa na Mungu, ili nikawaeleze kwa faragha wale walioonekana kuwa viongozi, ile Injili ninayoihubiri kwa watu wa Mataifa. Nilifanya hivyo kwa kuhofia kwamba nisije nikawa nilikuwa ninakimbia au nilikimbia bure.
I went up in obedience to a revelation of God's will; and I explained to them the Good News which I proclaim among the Gentiles. To the leaders of the Church this explanation was made in private, lest by any means I should be running, or should already have run, in vain.
3 Lakini hata Tito ambaye alikuwa Myunani, hakulazimika kutahiriwa.
But although my companion Titus was a Greek they did not insist upon even his being circumcised.
4 Lakini kwa sababu ya ndugu wa uongo ambao walijiingiza kwa siri katikati yetu ili kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika Kristo Yesu, wapate kututia utumwani,
Yet there was danger of this through the false brethren secretly introduced into the Church, who had stolen in to spy out the freedom which is ours in Christ Jesus, in order to rob us of it.
5 hatukukubaliana nao hata dakika moja, ili kwamba ukweli wa Injili ubaki nanyi.
But not for an hour did we give way and submit to them; in order that the Good News might continue with you in its integrity.
6 Kwa habari ya wale waliokuwa wakubaliwe kuwa viongozi (kwangu mimi sikujali vyeo vyao, maana Mungu hana upendeleo), wale watu hawakuniongezea chochote.
From those leaders I gained nothing new. Whether they were men of importance or not, matters nothing to me--God recognizes no external distinctions. To me, at any rate, the leaders imparted nothing new.
7 Badala yake walitambua kwamba nilikuwa nimekabidhiwa kazi ya kuhubiri Injili kwa watu wa Mataifa, kama vile Petro alivyokabidhiwa kuhubiri Injili kwa Wayahudi.
Indeed, when they saw that I was entrusted with the preaching of the Good News to the Gentiles as Peter had been with that to the Jews--
8 Kwa maana, Mungu aliyekuwa akitenda kazi katika huduma ya Petro kama mtume kwa Wayahudi, ndiye pia aliyekuwa anatenda kazi katika huduma yangu kama mtume kwa watu wa Mataifa.
for He who had been at work within Peter with a view to his Apostleship to the Jews had also been at work within me with a view to my Apostleship to the Gentiles--
9 Basi, Yakobo, Kefa na Yohana, walioonekana kama nguzo za kanisa, walitupa mkono wa shirika, mimi na Barnaba walipotambua ile neema niliyopewa. Wakakubali kwamba sisi twende kwa watu wa Mataifa na wao waende kwa Wayahudi.
and when they perceived the mission which was graciously entrusted to me, they (that is to say, James, Peter, and John, who were considered to be the pillars of the Church) welcomed Barnabas and me to their fellowship on the understanding that we were to go to the Gentiles and they to the Jews.
10 Walichotuomba ni kwamba tuendelee kuwakumbuka maskini, jambo ambalo ndilo nililokuwa na shauku ya kulifanya.
Only they urged that we should remember their poor--a thing which was uppermost in my own mind.
11 Lakini Petro alipofika Antiokia, mimi nilimpinga ana kwa ana kwa sababu alikuwa amekosea kwa wazi.
Now when Peter visited Antioch, I remonstrated with him to his face, because he had incurred just censure.
12 Kabla baadhi ya watu waliotoka kwa Yakobo hawajafika, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa. Lakini hao watu walipofika alianza kujiondoa na kujitenga na watu wa Mataifa kwa sababu aliwaogopa wale wa kundi la tohara.
For until certain persons came from James he had been accustomed to eat with Gentiles; but as soon as these persons came, he withdrew and separated himself for fear of the Circumcision party.
13 Pia Wayahudi wengine waliungana naye katika unafiki huu, hata Barnaba naye akapotoshwa na unafiki wao.
And along with him the other Jews also concealed their real opinions, so that even Barnabas was carried away by their lack of straightforwardness.
14 Nilipoona kwamba hawatendi sawasawa na kweli ya Injili, nilimwambia Petro mbele ya wote, “Wewe ni Myahudi, nawe unaishi kama mtu wa Mataifa na wala si kama Myahudi. Imekuwaje basi, mnawalazimisha watu wa Mataifa kufuata desturi za Kiyahudi?
As soon as I saw that they were not walking uprightly in the spirit of the Good News, I said to Peter, before them all, "If you, though you are a Jew, live as a Gentile does, and not as a Jew, how can you make the Gentiles follow Jewish customs?
15 “Sisi wenyewe ni Wayahudi kwa kuzaliwa na si watu wenye dhambi kama watu wa Mataifa,
You and I, though we are Jews by birth and not Gentile sinners,
16 bado tunajua ya kwamba mtu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria bali kwa njia ya imani katika Yesu Kristo. Hivyo sisi pia, tumemwamini Kristo Yesu ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika Kristo, wala si kwa matendo ya sheria, kwa sababu kwa kushika sheria hakuna hata mtu mmoja atakayehesabiwa haki.
know that it is not through obedience to Law that a man can be declared free from guilt, but only through faith in Jesus Christ. We have therefore believed in Christ Jesus, for the purpose of being declared free from guilt, through faith in Christ and not through obedience to Law. For through obedience to Law no human being shall be declared free from guilt.
17 “Lakini tukitafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, inakuwa dhahiri kwamba sisi ni wenye dhambi. Je, ina maana kwamba Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? La hasha!
But if while we are seeking in Christ acquittal from guilt we ourselves are convicted of sin, Christ then encourages us to sin! No, indeed.
18 Lakini ikiwa mimi ninajenga tena kile ambacho nimekwisha kukibomoa, basi ninaonyesha kwamba mimi ni mkosaji.
Why, if I am now rebuilding that structure of sin which I had demolished, I am thereby constituting myself a transgressor;
19 Kwa maana mimi kwa njia ya sheria, nimeifia sheria ili nipate kuishi kwa ajili ya Mungu.
for it is by the Law that I have died to the Law, in order that I may live to God.
20 Nimesulubiwa pamoja na Kristo, wala si mimi tena ninayeishi, bali Kristo ndiye aishiye ndani yangu. Uhai nilio nao sasa katika mwili, ninaishi kwa imani ya Mwana wa Mungu, aliyenipenda na kujitoa kwa ajili yangu.
I have been crucified with Christ, and it is no longer I that live, but Christ that lives in me; and the life which I now live in the body I live through faith in the Son of God who loved me and gave Himself up to death on my behalf.
21 Siibatilishi neema ya Mungu, kwa maana kama haki ingeweza kupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure!”
I do not nullify the grace of God; for if acquittal from guilt is obtainable through the Law, then Christ has died in vain."

< Wagalatia 2 >