< Matendo 4 >

1 Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakisema na watu, makuhani, mkuu wa walinzi wa Hekalu na Masadukayo wakawajia,
While they were saying this to the people, the Priests, the Commander of the Temple Guard, and the Sadducees came upon them,
2 huku wakiwa wamekasirika sana kwa sababu mitume walikuwa wanawafundisha watu na kuhubiri kwamba kuna ufufuo wa wafu ndani ya Yesu.
highly incensed at their teaching the people and proclaiming in the case of Jesus the Resurrection from among the dead.
3 Wakawakamata Petro na Yohana na kuwatia gerezani mpaka kesho yake kwa kuwa ilikuwa jioni.
They arrested the two Apostles and lodged them in custody till the next day; for it was already evening.
4 Lakini wengi waliosikia lile neno waliamini, idadi yao ilikuwa yapata wanaume 5,000.
But many of those who had listened to their preaching believed; and the number of the adult men had now grown to be about 5,000.
5 Kesho yake, viongozi wa Kiyahudi, wazee na walimu wa sheria wakakusanyika Yerusalemu.
The next day a meeting was held in Jerusalem of their Rulers, Elders, and Scribes,
6 Walikuwepo kuhani mkuu Anasi, Kayafa, Yohana, Iskanda, na wengi wa jamaa ya kuhani mkuu.
with Annas the High Priest, Caiaphas, John, Alexander, and the other members of the high-priestly family.
7 Baada ya kuwasimamisha Petro na Yohana katikati yao, wakawauliza, “Ni kwa uwezo gani au kwa jina la nani mmefanya jambo hili?”
So they made the Apostles stand in the centre, and demanded of them, "By what power or in what name have you done this?"
8 Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akajibu, “Enyi watawala na wazee wa watu,
Then Peter was filled with the Holy Spirit, and he replied, "Rulers and Elders of the people,
9 kama leo tukihojiwa kwa habari ya mambo mema aliyotendewa yule kiwete na kuulizwa jinsi alivyoponywa,
if we to-day are under examination concerning the benefit conferred on a man helplessly lame, as to how this man has been cured;
10 ijulikane kwenu nyote na kwa watu wote wa Israeli kwamba: Ni kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulubisha lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama mbele yenu akiwa mzima kabisa.
be it known to you all, and to all the people of Israel, that through the name of Jesus the Anointed, the Nazarene, whom you crucified, but whom God has raised from among the dead-- through that name this man stands here before you in perfect health.
11 Huyu ndiye “‘jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilikataa, ambalo limekuwa jiwe kuu la pembeni.’
This Jesus is the Stone treated with contempt by you the builders, but it has been made the Cornerstone.
12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”
And in no other is the great salvation to be found; for, in fact, there is no second name under Heaven that has been given among men through which we are to be saved."
13 Wale viongozi na wazee walipoona ujasiri wa Petro na Yohana na kujua ya kuwa walikuwa watu wa kawaida, wasio na elimu, walishangaa sana, wakatambua kwamba hawa watu walikuwa na Yesu.
As they looked on Peter and John so fearlessly outspoken--and also discovered that they were illiterate persons, untrained in the schools--they were surprised; and now they recognized them as having been with Jesus.
14 Lakini kwa kuwa walikuwa wanamwona yule kiwete aliyeponywa amesimama pale pamoja nao, hawakuweza kusema lolote kuwapinga.
And seeing the man standing with them--the man who had been cured--they had no reply to make.
15 Wakawaamuru watoke nje ya Baraza la Wayahudi wakati wakisemezana jambo hilo wao kwa wao.
So they ordered them to withdraw from the Sanhedrin while they conferred among themselves.
16 Wakaulizana, “Tuwafanyie nini watu hawa? Hatuwezi kukanusha muujiza huu mkubwa walioufanya ambao ni dhahiri kwa kila mtu Yerusalemu.
"What are we to do with these men?" they asked one another; for the fact that a remarkable miracle has been performed by them is well known to every one in Jerusalem, and we cannot deny it.
17 Lakini ili kuzuia jambo hili lisiendelee kuenea zaidi kwa watu, ni lazima tuwaonye watu hawa ili wasiseme tena na mtu yeyote kwa jina la Yesu.”
But to prevent the matter spreading any further among the people, let us stop them by threats from speaking in the future in this name to any one whatever."
18 Kisha wakawaita tena ndani na kuwaamuru wasiseme wala kufundisha kamwe kwa hili jina la Yesu.
So they recalled the Apostles, and ordered them altogether to give up speaking or teaching in the name of Jesus.
19 Lakini Petro na Yohana wakajibu, “Amueni ninyi wenyewe iwapo ni haki mbele za Mungu kuwatii ninyi kuliko kumtii Mungu.
But Peter and John replied, "Judge whether it is right in God's sight to listen to you instead of listening to God.
20 Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema yale tuliyoyaona na kuyasikia.”
As for us, what we have seen and heard we cannot help speaking about."
21 Baada ya vitisho vingi, wakawaacha waende zao. Hawakuona njia yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu, kwa kuwa watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetukia.
The Court added further threats and then let them go, being quite unable to find any way of punishing them on account of the people, because all gave God the glory for the thing that had happened.
22 Kwa kuwa umri wa yule mtu aliyekuwa ameponywa kwa muujiza ulikuwa zaidi ya miaka arobaini.
For the man was over forty years of age on whom this miracle of restoration to health had been performed.
23 Punde Petro na Yohana walipoachiliwa, walirudi kwa waumini wenzao wakawaeleza waliyoambiwa na viongozi wa makuhani na wazee.
After their release the two Apostles went to their friends, and told them all that the High Priests and Elders had said.
24 Watu waliposikia hayo, wakainua sauti zao, wakamwomba Mungu kwa pamoja, wakisema, “Bwana Mwenyezi, uliyeziumba mbingu na nchi na bahari, na vitu vyote vilivyomo.
And they, upon hearing the story, all lifted up their voices to God and said, "O Sovereign Lord, it is Thou who didst make Heaven and earth and sea, and all that is in them,
25 Wewe ulisema kwa Roho Mtakatifu kupitia kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ukasema: “‘Mbona mataifa wanaghadhibika, na kabila za watu zinawaza ubatili?
and didst say through the Holy Spirit by the lips of our forefather David Thy servant, "'Why have the nations stamped and raged, and the peoples formed futile plans?
26 Wafalme wa dunia wamejipanga, na watawala wanakusanyika pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.’
The kings of the earth came near, and the rulers assembled together against the Lord and against His Anointed.'"
27 Ni kweli Herode na Pontio Pilato pamoja na watu wa Mataifa na Waisraeli, walikusanyika katika mji huu dhidi ya mwanao mtakatifu Yesu uliyemtia mafuta.
"They did indeed assemble in this city in hostility to Thy holy Servant Jesus whom Thou hadst anointed--Herod and Pontius Pilate with the Gentiles and also the tribes of Israel--
28 Wao wakafanya yale ambayo uweza wako na mapenzi yako yalikuwa yamekusudia yatokee tangu zamani.
to do all that Thy power and Thy will had predetermined should be done.
29 Sasa, Bwana angalia vitisho vyao na utuwezeshe sisi watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri mkuu.
And now, Lord, listen to their threats, and enable Thy servants to proclaim Thy Message with fearless courage,
30 Nyoosha mkono wako ili kuponya wagonjwa na kutenda ishara na miujiza kwa jina la Mwanao mtakatifu Yesu.”
whilst Thou stretchest out Thine arm to cure men, and to give signs and marvels through the name of Thy holy Servant Jesus."
31 Walipokwisha kuomba, mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.
When they had prayed, the place in which they were assembled shook, and they were, one and all, filled with the Holy Spirit, and proceeded to tell God's Message with boldness.
32 Wale walioamini wote walikuwa na moyo mmoja na nia moja. Wala hakuna hata mmoja aliyesema chochote alichokuwa nacho ni mali yake mwenyewe, lakini walishirikiana kila kitu walichokuwa nacho.
Among all those who had embraced the faith there was but one heart and soul, so that none of them claimed any of his possessions as his own, but everything they had was common property;
33 Mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwa Bwana Yesu kwa nguvu nyingi na neema ya Mungu ilikuwa juu yao wote.
while the Apostles with great force of conviction delivered their testimony as to the resurrection of the Lord Jesus; and great grace was upon them all.
34 Wala hapakuwepo mtu yeyote miongoni mwao aliyekuwa mhitaji, kwa sababu mara kwa mara wale waliokuwa na mashamba na nyumba waliviuza, wakaleta thamani ya vitu vilivyouzwa,
And, in fact, there was not a needy man among them, for all who were possessors of lands or houses sold them, and brought the money which they realised,
35 wakaiweka miguuni pa mitume, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
and gave it to the Apostles, and distribution was made to every one according to his wants.
36 Yosefu, Mlawi kutoka Kipro, ambaye mitume walimwita Barnaba (maana yake Mwana wa Faraja),
In this way Joseph, whom the Apostles gave the name of Bar-nabas--signifying 'Son of Encouragement' --a Levite, a native of Cyprus,
37 aliuza shamba alilokuwa nalo, akaleta hizo fedha alizopata na kuziweka miguuni pa mitume.
sold a farm which he had, and brought the money and gave it to the Apostles.

< Matendo 4 >