< Matendo 23 >

1 Paulo akawakazia macho wale wajumbe wa baraza, akasema, “Ndugu zangu, nimetimiza wajibu wangu kwa Mungu kwa dhamiri safi kabisa hadi leo.”
Then Paul, fixing a steady gaze on the Sanhedrin, said, "Brethren, it is with a perfectly clear conscience that I have discharged my duties before God up to this day."
2 Kwa ajili ya jambo hili kuhani mkuu Anania akaamuru wale waliokuwa karibu na Paulo wampige kofi kinywani.
On hearing this the High Priest Ananias ordered those who were standing near Paul to strike him on the mouth.
3 Ndipo Paulo akamwambia, “Mungu atakupiga wewe, ewe ukuta uliopakwa chokaa! Wewe umeketi hapo ili kunihukumu kwa mujibu wa sheria, lakini wewe mwenyewe unakiuka sheria kwa kuamuru kwamba nipigwe kinyume cha sheria!”
"Before long," exclaimed Paul, "God will strike you, you white-washed wall! Are you sitting there to judge me in accordance with the Law, and do you yourself actually break the Law by ordering me to be struck?"
4 Wale watu waliokuwa wamesimama karibu na Paulo wakamwambia, “Je, wewe wathubutu kumtukana kuhani mkuu wa Mungu?”
"Do you rail at God's High Priest?" cried the men who stood by him.
5 Paulo akajibu, “Ndugu zangu, sikujua kwamba yeye alikuwa kuhani mkuu. Kwa maana imeandikwa, ‘Usimnenee mabaya kiongozi wa watu wako.’”
"I did not know, brethren," replied Paul, "that he was the High Priest; for it is written, 'Thou shalt not speak evil of a ruler of Thy people.'"
6 Paulo alipotambua ya kuwa baadhi yao walikuwa Masadukayo na wengine ni Mafarisayo, akapaza sauti kwenye baraza, “Ndugu zangu, mimi ni Farisayo, mwana Farisayo. Hapa nimeshtakiwa kuhusu tumaini langu katika ufufuo wa wafu.”
Noticing, however, that the Sanhedrin consisted partly of Sadducees and partly of Pharisees, he called out loudly among them, "Brethren, I am a Pharisee, the son of Pharisees. It is because of my hope of a resurrection of the dead that I am on my trial."
7 Aliposema haya, farakano likaanza kati ya Mafarisayo na Masadukayo na baraza lote likagawanyika.
These words of his caused an angry dispute between the Pharisees and the Sadducees, and the assembly took different sides.
8 (Kwa maana Masadukayo wanasema kwamba hakuna ufufuo, wala hakuna malaika au roho, lakini Mafarisayo wanaamini haya yote.)
For the Sadducees maintain that there is no resurrection, and neither angel nor spirit; but the Pharisees acknowledge the existence of both.
9 Kukawa na ghasia kubwa, nao baadhi ya walimu wa sheria ambao ni Mafarisayo, wakasimama wakapinga kwa nguvu wakisema, “Hatuoni kosa lolote la mtu huyu! Huenda ikawa roho au malaika amezungumza naye”
So there arose a great uproar; and some of the Scribes belonging to the sect of the Pharisees sprang to their feet and fiercely contended, saying, "We find no harm in the man. What if a spirit has spoken to him, or an angel----!"
10 Ugomvi ukawa mkubwa kiasi kwamba yule jemadari akahofu kuwa wangemrarua Paulo vipande vipande, akaamuru vikosi vya askari vishuke na kumwondoa Paulo katikati yao kwa nguvu na kumleta ndani ya ngome ya jeshi.
But when the struggle was becoming violent, the Tribune, fearing that Paul would be torn to pieces by the people, ordered the troops to go down and take him from among them by force and bring him into the barracks.
11 Usiku uliofuata, Bwana akasimama karibu naye akamwambia, “Jipe moyo! Kama vile ulivyonishuhudia hapa Yerusalemu, hivyo imekupasa kunishuhudia huko Rumi pia.”
The following night the Lord came and stood at Paul's side, and said, "Be of good courage, for as you have borne faithful witness about me in Jerusalem, so you must also bear witness in Rome."
12 Kulipopambazuka Wayahudi wakafanya shauri pamoja na kujifunga kwa kiapo kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wawe wamemuua Paulo.
Now, when daylight came, the Jews formed a conspiracy and solemnly swore not to eat or drink till they had killed Paul.
13 Waliofanya mpango huo walikuwa zaidi ya watu arobaini.
There were more than forty of them who bound themselves by this oath.
14 Wakawaendea viongozi wa makuhani na wazee na kusema, “Tumejifunga pamoja kwa kiapo kwamba hatutakula wala kunywa mpaka tuwe tumemuua Paulo.
They went to the High Priests and Elders and said to them, "We have bound ourselves under a heavy curse to take no food till we have killed Paul.
15 Hivyo basi, wewe pamoja na baraza, inawapasa mkamjulishe jemadari ili amteremshe Paulo kwenu, mjifanye kama mnataka kufanya uchunguzi wa kina zaidi wa shauri lake. Nasi tuko tayari kumuua kabla hajafika hapa.”
Now therefore you and the Sanhedrin should make representations to the Tribune for him to bring him down to you, under the impression that you intend to inquire more minutely about him; and we are prepared to assassinate him before he comes near the place."
16 Lakini mtoto wa dada yake Paulo aliposikia juu ya shauri hilo baya, alikwenda kule kwenye ngome ya askari na kumweleza Paulo.
But Paul's sister's son heard of the intended attack upon him. So he came and went into the barracks and told Paul about it;
17 Ndipo Paulo akamwita mmoja wa viongozi wa askari, akamwambia, “Mpeleke huyu kijana kwa jemadari, analo jambo la kumweleza.”
and Paul called one of the Captains and said, "Take this young man to the Tribune, for he has information to give him."
18 Hivyo yule kiongozi wa askari akampeleka yule kijana kwa jemadari, akamwambia, “Paulo yule mfungwa aliniita na kuniomba nimlete huyu kijana kwako, kwa sababu ana neno la kukueleza.”
So he took him and brought him to the Tribune, and said, "Paul, the prisoner, called me to him and begged me to bring this youth to you, because he has something to say to you."
19 Yule jemadari akamshika yule kijana mkono, akampeleka kando na kumuuliza, “Unataka kuniambia nini?”
Then the Tribune, taking him by the arm, withdrew out of the hearing of others and asked him, "What have you to tell me?"
20 Yule kijana akasema, “Wayahudi wamekubaliana wakuombe umpeleke Paulo kwenye baraza lao kesho kwa kisingizio kwamba wanataka kufanya uchunguzi wa kina wa shauri lake.
"The Jews," he replied, "have agreed to request you to bring Paul down to the Sanhedrin to-morrow for the purpose of making yourself more accurately acquainted with the case.
21 Lakini usishawishiwe nao kwa maana zaidi ya watu arobaini wanamvizia. Wamejifunga kwa kiapo kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wawe wamemuua Paulo. Sasa wako tayari, wanangoja idhini yako kwa ajili ya ombi lao.”
I beg you not to comply; for more than forty men among them are lying in wait for him, who have solemnly vowed that they will neither eat nor drink till they have assassinated him; and even now they are ready, in anticipation of receiving that promise of you."
22 Yule jemadari akamruhusu yule kijana aende na akamwonya, akisema, “Usimwambie mtu yeyote kwamba umenieleza habari hizi.”
So the Tribune sent the youth home, cautioning him. "Do not let any one know that you have given me this information," he said.
23 Kisha yule jemadari akawaita viongozi wake wawili wa askari akawaambia, “Jiandaeni kuondoka saa tatu usiku huu kuelekea Kaisaria pamoja na askari 200, wapanda farasi sabini na watu 200 wenye mikuki.
Then, calling to him two of the Captains, he gave his orders. "Get ready two hundred men," he said, "to march to Caesarea, with seventy cavalry and two hundred light infantry, starting at nine o'clock to-night."
24 Pia tayarisheni na farasi watakaotumiwa na Paulo, mkampeleke salama kwa mtawala Feliksi.”
He further told them to provide horses to mount Paul on, so as to bring him safely to Felix the Governor.
25 Kisha akaandika barua kwa Feliksi kama ifuatavyo:
He also wrote a letter of which these were the contents:
26 Klaudio Lisia, Kwa Mtawala, Mtukufu Feliksi: Salamu.
"Claudius Lysias to his Excellency, Felix the Governor: all good wishes.
27 Mtu huyu alikamatwa na Wayahudi wakakaribia kumuua, lakini nikaja na vikosi vyangu vya askari nikamwokoa, kwa kuwa nilipata habari kwamba yeye ni raiya wa Rumi.
This man Paul had been seized by the Jews, and they were on the point of killing him, when I came upon them with the troops and rescued him, for I had been informed that he was a Roman citizen.
28 Nilitaka kujua kwa nini walikuwa wanamshutumu, hivyo nikamleta mbele ya baraza lao.
And, wishing to know with certainty the offense of which they were accusing him, I brought him down into their Sanhedrin,
29 Ndipo nikaona kuwa alikuwa anashutumiwa kwa mambo yanayohusu sheria yao, lakini hakuwa ameshtakiwa kwa jambo lolote linalostahili kifo au kifungo.
and I discovered that the charge had to do with questions of their Law, but that he was accused of nothing for which he deserves death or imprisonment.
30 Nilipoarifiwa kuwa kulikuwa na shauri baya dhidi ya mtu huyu, nilimtuma kwako mara moja. Niliwaagiza washtaki wake pia waeleze mashtaka yao dhidi yake mbele yako.
But now that I have received information of an intended attack upon him, I immediately send him to you, directing his accusers also to state before you the case they have against him."
31 Hivyo askari, kwa kufuata maelekezo waliyopewa, wakamchukua Paulo wakati wa usiku na kumleta mpaka Antipatri.
So, in obedience to their orders, the soldiers took Paul and brought him by night as far as Antipatris.
32 Kesho yake wakawaacha wale wapanda farasi waendelee na safari wakiwa na Paulo, wao wakarudi kwenye ngome ya askari.
The next day the infantry returned to the barracks, leaving the cavalry to proceed with him;
33 Askari walipofika Kaisaria, walimpa mtawala ile barua, na kumkabidhi Paulo kwake.
and, the cavalry having reached Caesarea and delivered the letter to the Governor, they brought Paul also to him.
34 Mtawala alipokwisha kuisoma ile barua alimuuliza Paulo alikuwa mtu wa jimbo gani. Alipojua kuwa anatoka Kilikia,
Felix, after reading the letter, inquired from what province he was; and being told "from Cilicia,"
35 alisema, “Nitasikiliza shauri lako washtaki wako watakapofika hapa.” Kisha akaamuru Paulo awekwe chini ya ulinzi kwenye jumba la kifalme la Herode.
he said, "I will hear all you have to say, when your accusers also have come." And he ordered him to be detained in custody in Herod's Palace.

< Matendo 23 >