< 1 Petro 1 >

1 Petro, mtume wa Yesu Kristo: Kwa wateule wa Mungu, wageni katika ulimwengu, waliotawanyika kote katika Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia.
Peter, an Apostle of Jesus Christ: To God's own people scattered over the earth, who are living as foreigners in Pontus, Galatia, Cappadocia, Roman Asia, and Bithynia,
2 Ni ninyi ambao mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba kulingana na alivyotangulia kuwajua, kupitia kwa kazi ya utakaso wa Roho, katika utiifu kwa Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake: Neema na amani ziwe kwenu kwa wingi.
chosen in accordance with the foreknowledge of God the Father, through the sanctifying work of the Spirit, with a view to their obedience and to their being sprinkled with the blood of Jesus Christ. May more and more grace and peace be granted to you.
3 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema zake kuu ametuzaa sisi mara ya pili katika tumaini lenye uzima kupitia kwa kufufuka kwa Yesu Kristo kutoka kwa wafu,
Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, who in His great mercy has begotten us anew to an ever-living hope through the resurrection of Jesus Christ from the dead,
4 ili tuupate urithi usioharibika, usio na uchafu, ule usionyauka: uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu,
to an inheritance imperishable, undefiled and unfading, which has been reserved in Heaven for you,
5 ninyi ambao mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani, hadi uje ule wokovu ulio tayari kufunuliwa nyakati za mwisho.
whom God in His power is guarding through faith for a salvation that even now stands ready for unveiling at the End of the Age.
6 Katika hili mnafurahi sana, ingawa sasa kwa kitambo kidogo mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna nyingi.
Rejoice triumphantly in the prospect of this, even if now, for a short time, you are compelled to sorrow amid various trials.
7 Haya yamewajia ili kwamba imani yenu, iliyo ya thamani kuliko dhahabu ipoteayo, ingawa hujaribiwa kwa moto, ionekane kuwa halisi na imalizie katika sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atadhihirishwa.
The sorrow comes in order that the testing of your faith--being more precious than that of gold, which perishes and yet is proved by fire--may be found to result in praise and glory and honour at the re-appearing of Jesus Christ.
8 Ingawa hamjamwona, mnampenda; tena ingawa sasa hammwoni, mnamwamini na kujawa na furaha isiyoneneka yenye utukufu usioelezeka.
Him you love, though your eyes have never looked on Him. In Him, though at present you cannot see Him, you nevertheless trust, and triumph with a joy which is unspeakable and is crowned with glory,
9 Maana mnaupokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.
while you are securing as the outcome of your faith the salvation of your souls.
10 Kwa habari ya wokovu huu, wale manabii waliosema kuhusu neema ambayo ingewajia ninyi, walitafuta kwa bidii na kwa uangalifu mkubwa,
There were Prophets who earnestly inquired about that salvation, and closely searched into it--even those who spoke beforehand of the grace which was to come to you.
11 wakijaribu kujua ni wakati upi na katika mazingira gani ambayo Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alionyesha, alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu ule ambao ungefuata.
They were eager to know the time which the Spirit of Christ within them kept indicating, or the characteristics of that time, when they solemnly made known beforehand the sufferings that were to come upon Christ and the glories which would follow.
12 Walidhihirishiwa kwamba walikuwa hawajihudumii wao wenyewe, bali waliwahudumia ninyi, waliponena kuhusu mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.
To them it was revealed that they were serving not themselves but you, when they foretold the very things which have now been openly declared to you by those who, having been taught by the Holy Spirit which had been sent from Heaven, brought you the Good News. Angels long to stoop and look into these things.
13 Kwa hiyo, tayarisheni nia zenu kwa kazi; mwe na kiasi, mkitumainia kikamilifu ile neema mtakayopewa Yesu Kristo atakapodhihirishwa.
Therefore gird up your minds and fix your hopes calmly and unfalteringly upon the boon that is soon to be yours, at the re-appearing of Jesus Christ.
14 Kama watoto watiifu, msifuate tamaa zenu mbaya wakati mlipoishi kwa ujinga.
And, since you delight in obedience, do not shape your lives by the cravings which used to dominate you in the time of your ignorance,
15 Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi kuweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.
but--in imitation of the holy One who has called you--you also must be holy in all your habits of life.
16 Kwa maana imeandikwa: “Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
Because it stands written, "You are to be holy, because I am holy."
17 Kwa sababu mnamwita Baba ahukumuye kila mtu kulingana na matendo yake pasipo upendeleo, enendeni kwa hofu ya kumcha Mungu wakati wenu wa kukaa hapa duniani kama wageni.
And if you address as your Father Him who judges impartially in accordance with each man's actions, then spend in fear the time of your stay here on earth,
18 Kwa maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutoka mwenendo wenu usiofaa ambao mliurithi kutoka kwa baba zenu, si kwa vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu,
knowing, as you do, that it was not with a ransom of perishable wealth, such as silver or gold, that you were set free from your frivolous habits of life which had been handed down to you from your forefathers,
19 bali kwa damu ya thamani ya Kristo, yule Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa.
but with the precious blood of Christ--as of an unblemished and spotless lamb.
20 Yeye alichaguliwa kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
He was pre-destined indeed to this work, even before the creation of the world, but has been plainly manifested in these last days for the sake of you who, through Him,
21 Kupitia kwake mmemwamini Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu na akampa utukufu, ili imani yenu na tumaini lenu ziwe kwa Mungu.
are faithful to God, who raised Him from among the dead and gave Him glory, so that your faith and hope are resting upon God.
22 Basi kwa kuwa mmejitakasa nafsi zenu kwa kuitii ile kweli hata mkawa na upendo wa ndugu usio na unafiki, basi pendaneni kwa dhati kutoka moyoni.
Now that, through your obedience to the truth, you have purified your souls for cherishing sincere brotherly love, you must love another heartily and fervently.
23 Kwa maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika, kupitia kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu milele. (aiōn g165)
For you have been begotten again by God's ever-living and enduring word from a germ not of perishable, but of imperishable life. (aiōn g165)
24 Maana, “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao ni kama maua ya kondeni; majani hunyauka na maua huanguka,
"All mankind resemble the herbage, and all their beauty is like its flowers. The herbage dries up, and its flowers drop off;
25 lakini neno la Bwana ladumu milele.” Hili ndilo neno lililohubiriwa kwenu. (aiōn g165)
But the word of the Lord remains for ever." And that means the Message which has been proclaimed among you in the Good News. (aiōn g165)

< 1 Petro 1 >