< 1 Petro 2 >

1 Kwa hiyo, wekeni mbali nanyi uovu wote na udanganyifu wote, unafiki, wivu na masingizio ya kila namna.
Rid yourselves therefore of all ill-will and all deceitfulness, of insincerity and envy, and of all evil speaking.
2 Kama watoto wachanga, waliozaliwa sasa, yatamanini maziwa ya kiroho yasiyochanganywa na kitu kingine chochote, ili kwa hayo mpate kukua katika wokovu,
Thirst, like newly-born infants, for pure milk for the soul, that by it you may grow up to salvation;
3 ikiwa kweli mmeonja ya kwamba Bwana ni mwema.
if you have had any experience of the goodness of the Lord.
4 Mnapokuja kwake, yeye aliye Jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu bali kwa Mungu ni teule na la thamani kwake,
Come to Him, the ever-living Stone, rejected indeed by men as worthless, but in God's esteem chosen and held in honour.
5 ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mnajengwa kuwa nyumba ya kiroho, ili mpate kuwa ukuhani mtakatifu, mkitoa dhabihu za kiroho zinazokubaliwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
And be yourselves also like living stones that are being built up into a spiritual house, to become a holy priesthood to offer spiritual sacrifices acceptable to God through Jesus Christ.
6 Kwa maana imeandikwa katika Maandiko: “Tazama, naweka katika Sayuni, jiwe la pembeni teule lenye thamani, na yeyote atakayemwamini hataaibika kamwe.”
For it is contained in Scripture, "See, I am placing on Mount Zion a Cornerstone, chosen, and held in honour, and he whose faith rests on Him shall never have reason to feel ashamed."
7 Kwenu ninyi mnaoamini, jiwe hili ni la thamani. Lakini kwao wasioamini, “Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni,”
To you believers, therefore, that honour belongs; but for unbelievers-- "A Stone which the builders rejected has been made the Cornerstone,"
8 tena, “Jiwe lenye kuwafanya watu wajikwae, na mwamba wa kuwaangusha.” Wanajikwaa kwa sababu hawakulitii lile neno, kama walivyowekewa tangu zamani.
and "a Stone for the foot to strike against, and a Rock to stumble over." Their foot strikes against it because they are disobedient to God's Message, and to this they were appointed.
9 Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio milki ya Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.
But you are a chosen race, a priesthood of kingly lineage, a holy nation, a people belonging specially to God, that you may make known the perfections of Him who called you out of darkness into His marvellous light.
10 Mwanzo ninyi mlikuwa si taifa, lakini sasa ninyi ni taifa la Mungu. Mwanzo mlikuwa hamjapata rehema, lakini sasa mmepata rehema.
Once you were not a people, but now you are the people of God. Once you had not found mercy, but now you have.
11 Wapenzi, ninawasihi, mkiwa kama wageni na wapitaji hapa ulimwenguni, epukeni tamaa mbaya za mwili ambazo hupigana vita na roho zenu.
Dear friends, I entreat you as pilgrims and foreigners not to indulge the cravings of your lower natures: for all such cravings wage war upon the soul.
12 Kuweni na mwenendo mzuri mbele ya watu wasiomjua Mungu, ili kama wanawasingizia kuwa watenda mabaya, wayaone matendo yenu mema nao wamtukuze Mungu siku atakapokuja kwetu.
Live honourable lives among the Gentiles, in order that, although they now speak against you as evil-doers, they may yet witness your good conduct, and may glorify God on the day of reward and retribution.
13 Kwa ajili ya Bwana, tiini kila mamlaka iliyowekwa na wanadamu: Kwa mfalme kwani ndiye aliye na mamlaka ya juu zaidi,
Submit, for the Lord's sake, to every authority set up by man, whether it be to the Emperor as supreme ruler,
14 au kwa maafisa aliowaweka, kwa kuwa mfalme amewatuma ili kuwaadhibu wale wanaokosa, na kuwapongeza wale watendao mema.
or to provincial Governors as sent by him for the punishment of evil-doers and the encouragement of those who do what is right.
15 Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema mnyamazishe maneno ya kijinga ya watu wapumbavu.
For it is God's will that by doing what is right you should thus silence the ignorant talk of foolish persons.
16 Ishini kama watu huru, lakini msitumie uhuru wenu kama kisingizio cha kutenda uovu, bali ishini kama watumishi wa Mungu.
Be free men, and yet do not make your freedom an excuse for base conduct, but be God's bondservants.
17 Mheshimuni kila mtu ipasavyo: Wapendeni jamaa ya ndugu waumini, mcheni Mungu, mpeni heshima mfalme.
Honour every one. Love the brotherhood, fear God, honour the Emperor.
18 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wema na wapole peke yao, bali pia wale walio wakali.
Household servants, be submissive to your masters, and show them the utmost respect--not only if they are kind and thoughtful, but also if they are unreasonable.
19 Kwa maana ni jambo la sifa kama mtu akivumilia anapoteswa kwa uonevu kwa ajili ya Mungu.
For it is an acceptable thing with God, if, from a sense of duty to Him, a man patiently submits to wrong, when treated unjustly.
20 Kwani ni faida gani kwa mtu kustahimili anapopigwa kwa sababu ya makosa yake? Lakini kama mkiteswa kwa sababu ya kutenda mema, nanyi mkastahimili, hili ni jambo la kusifiwa mbele za Mungu.
If you do wrong and receive a blow for it, what credit is there in your bearing it patiently? But if when you do right and suffer for it you bear it patiently, this is an acceptable thing with God.
21 Ninyi mliitwa kwa ajili ya haya, kwa sababu Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akiwaachia kielelezo, ili mzifuate nyayo zake.
And it is to this you were called; because Christ also suffered on your behalf, leaving you an example so that you should follow in His steps.
22 “Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.”
He never sinned, and no deceitful language was ever heard from His mouth.
23 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutishia, bali alijikabidhi kwa yeye ahukumuye kwa haki.
When He was reviled, He did not answer with reviling; when He suffered He uttered no threats, but left His wrongs in the hands of the righteous Judge.
24 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, ili tufe kwa mambo ya dhambi, bali tupate kuishi katika haki. Kwa kupigwa kwake, ninyi mmeponywa.
The burden of our sins He Himself carried in His own body to the Cross and bore it there, so that we, having died so far as our sins are concerned, may live righteous lives. By His wounds yours have been healed.
25 Kwa maana mlikuwa mmepotea kama kondoo, lakini sasa mmerudi kwa Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.
For you were straying like lost sheep, but now you have come back to the Shepherd and Protector of your souls.

< 1 Petro 2 >