< 1 Petro 4 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni nia iyo hiyo kwa maana mtu aliyekwisha kuteswa katika mwili ameachana na dhambi.
Since, then, Christ has suffered in the flesh, you also must arm yourselves with a determination to do the same--because he who has suffered in the flesh has done with sin--
2 Kwa hivyo, haishi maisha yake yaliyobaki ya kuishi hapa duniani kwa tamaa mbaya za wanadamu, bali anaishi kwa mapenzi ya Mungu.
that in future you may spend the rest of your earthly lives, governed not by human passions, but by the will of God.
3 Maana wakati uliopita mmekwisha kutumia muda wa kutosha katika maisha yenu mkifanya yale ambayo wapagani hupenda kutenda: wakiishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, vileo, ngoma mbaya, na ibada chukizo za sanamu.
For you have given time enough in the past to the doing of the things which the Gentiles delight in-- pursuing, as you did, a course of habitual licence, debauchery, hard drinking, noisy revelry, drunkenness and unholy image-worship.
4 Wao hushangaa kwamba ninyi hamjiingizi pamoja nao katika huo wingi wa maisha ya ufisadi, nao huwatukana ninyi.
At this they are astonished--that you do not run into the same excess of profligacy as they do; and they speak abusively of you.
5 Lakini itawapasa wao kutoa hesabu mbele zake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.
But they will have to give account to Him who stands ready to pronounce judgement on the living and the dead.
6 Kwa kuwa hii ndiyo sababu Injili ilihubiriwa hata kwa wale waliokufa, ili wahukumiwe sawasawa na wanadamu wengine katika mwili, lakini katika roho waishi kulingana na Mungu aishivyo.
For it is with this end in view that the Good News was proclaimed even to some who were dead, that they may be judged, as all mankind will be judged, in the body, but may be living a godly life in the spirit.
7 Mwisho wa mambo yote umekaribia. Kwa hiyo kuweni na akili tulivu na kiasi, mkikesha katika kuomba.
But the end of all things is now close at hand: therefore be sober-minded and temperate, so that you may give yourselves to prayer.
8 Zaidi ya yote, dumuni katika upendo kwa maana upendo husitiri wingi wa dhambi.
Above all continue to love one another fervently, for love throws a veil over a multitude of faults.
9 Kuweni wakarimu kila mtu na mwenzake pasipo manungʼuniko.
Extend ungrudging hospitality towards one another.
10 Kila mmoja na atumie kipawa chochote alichopewa kuwahudumia wengine, kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu.
Whatever be the gifts which each has received, you must use them for one another's benefit, as good stewards of God's many-sided kindness.
11 Yeyote asemaye hana budi kusema kama mtu asemaye maneno ya Mungu mwenyewe. Yeyote ahudumuye hana budi kuhudumu kwa nguvu zile anazopewa na Mungu, ili Mungu apate kutukuzwa katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
If any one preaches, let it be as uttering God's truth; if any one renders a service to others, let it be in the strength which God supplies; so that in everything glory may be given to God in the name of Jesus Christ, to whom belong the glory and the might to the Ages of the Ages. Amen. (aiōn g165)
12 Wapenzi, msione ajabu kwa yale mateso yanayotukia miongoni mwenu, kana kwamba ni kitu kigeni kinachowapata.
Dear friends, do not be surprised at finding that that scorching flame of persecution is raging among you to put you to the test--as though some surprising thing were accidentally happening to you.
13 Bali furahini kuwa mnashiriki katika mateso ya Kristo, ili mpate kufurahi zaidi wakati utukufu wake utakapofunuliwa.
On the contrary, in the degree that you share in the sufferings of the Christ, rejoice, so that at the unveiling of His glory you may also rejoice with triumphant gladness.
14 Kama mkitukanwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu Roho wa utukufu na wa Mungu anakaa juu yenu.
You are to be envied, if you are being reproached for bearing the name of Christ; for in that case the Spirit of glory-- even the Spirit of God--is resting upon you.
15 Lakini asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu anayeteswa kwa kuwa ni muuaji, au mwizi, au mhalifu wa aina yoyote, au anayejishughulisha na mambo ya watu wengine.
But let not one of you suffer as a murderer or a thief or an evil-doer, or as a spy upon other people's business.
16 Lakini kama ukiteseka kwa kuwa Mkristo, usihesabu jambo hilo kuwa ni aibu, bali mtukuze Mungu kwa sababu umeitwa kwa jina hilo.
If, however, any one suffers because he is a Christian, let him not be ashamed, but let him glorify God for being permitted to bear that name.
17 Kwa maana wakati umewadia wa hukumu kuanzia katika nyumba ya Mungu. Basi kama ikianzia kwetu sisi, mwisho wa hao wasiotii Injili ya Mungu utakuwaje?
For the time has come for judgement to begin, and to begin at the house of God; and if it begins with us, what will be the end of those who reject God's Good News?
18 Basi, “Ikiwa ni vigumu kwa mwenye haki kuokoka, itakuwaje kwa mtu asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?”
And if it is difficult even for a righteous man to be saved, what will become of irreligious men and sinners?
19 Kwa hiyo, wale wanaoteswa kulingana na mapenzi ya Mungu, wajikabidhi kwa Muumba wao aliye mwaminifu, huku wakizidi kutenda mema.
Therefore also, let those who are suffering in accordance with the will of God entrust their souls in well-doing to a faithful Creator.

< 1 Petro 4 >