< 1 Wakorintho 2 >

1 Ndugu zangu nilipokuja kwenu, sikuja na maneno ya ushawishi wala hekima ya hali ya juu nilipowahubiria siri ya Mungu.
And as for myself, brethren, when I came to you, it was not with surpassing power of eloquence or earthly wisdom that I came, announcing to you that which God had commanded me to bear witness to.
2 Kwa kuwa niliamua kutokujua kitu chochote wakati nikiwa nanyi isipokuwa Yesu Kristo aliyesulubiwa.
For I determined to be utterly ignorant, when among you, of everything except of Jesus Christ, and of Him as having been crucified.
3 Mimi nilikuja kwenu nikiwa dhaifu na mwenye hofu na kwa kutetemeka sana.
And so far as I myself was concerned, I came to you in conscious feebleness and in fear and in deep anxiety.
4 Kuhubiri kwangu na ujumbe wangu haukuwa kwa hekima na maneno ya ushawishi bali kwa madhihirisho ya nguvu za Roho
And my language and the Message that I proclaimed were not adorned with persuasive words of earthly wisdom, but depended upon truths which the Spirit taught and mightily carried home;
5 ili imani yenu isiwe imejengwa katika hekima ya wanadamu bali katika nguvu za Mungu.
so that your trust might rest not on the wisdom of man but on the power of God.
6 Lakini miongoni mwa watu waliokomaa twanena hekima, wala si hekima ya ulimwengu huu au ya watawala wa dunia hii wanaobatilika. (aiōn g165)
Yet when we are among mature believers we do speak words of wisdom; a wisdom not belonging, however, to the present age nor to the leaders of the present age who are soon to pass away. (aiōn g165)
7 Sisi tunanena hekima ya Mungu ambayo ni siri, tena iliyofichika, ambayo Mungu aliikusudia kabla ya ulimwengu kuwepo, kwa ajili ya utukufu wetu. (aiōn g165)
But in dealing with truths hitherto kept secret we speak of God's wisdom--that hidden wisdom which, before the world began, God pre-destined, so that it should result in glory to us; (aiōn g165)
8 Hakuna hata mtawala mmoja wa nyakati hizi aliyeelewa jambo hili. Kwa maana kama wangelielewa, wasingemsulubisha Bwana wa utukufu. (aiōn g165)
a wisdom which not one of the leaders of the present age possesses, for if they had possessed it, they would never have crucified the Lord of glory. (aiōn g165)
9 Lakini ni kama ilivyoandikwa: “Hakuna jicho limepata kuona, wala sikio limepata kusikia, wala hayakuingia moyoni wowote, yale Mungu amewaandalia wale wampendao”:
But--to use the words of Scripture--we speak of things which eye has not seen nor ear heard, and which have never entered the heart of man: all that God has in readiness for them that love Him.
10 Lakini mambo haya Mungu ametufunulia kwa Roho wake. Roho huchunguza kila kitu, hata mambo ya ndani sana ya Mungu.
For us, however, God has drawn aside the veil through the teaching of the Spirit; for the Spirit searches everything, including the depths of the divine nature.
11 Kwa maana ni nani anayejua mawazo ya mtu isipokuwa roho iliyo ndani ya huyo mtu? Vivyo hivyo hakuna mtu ajuaye mawazo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.
For, among human beings, who knows a man's inner thoughts except the man's own spirit within him? In the same way, also, only God's Spirit is acquainted with God's inner thoughts.
12 Basi hatukupokea roho ya dunia bali Roho atokaye kwa Mungu, ili tuweze kuelewa kile kipawa ambacho Mungu ametupatia bure.
But we have not received the spirit of the world, but the Spirit which comes forth from God, that we may know the blessings that have been so freely given to us by God.
13 Haya ndiyo tusemayo, si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya wanadamu bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua kweli za kiroho kwa maneno ya kiroho.
Of these we speak--not in language which man's wisdom teaches us, but in that which the Spirit teaches--adapting, as we do, spiritual words to spiritual truths.
14 Mtu ambaye hana Roho hawezi kupokea mambo yatokayo kwa Roho wa Mungu, kwa kuwa ni upuzi kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa sababu hayo yanaeleweka tu kwa upambanuzi wa rohoni.
The unspiritual man rejects the things of the Spirit of God, and cannot attain to the knowledge of them, because they are spiritually judged.
15 Mtu wa kiroho hubainisha mambo yote, lakini yeye mwenyewe habainishwi na mtu yeyote.
But the spiritual man judges of everything, although he is himself judged by no one.
16 “Kwa maana ni nani aliyefahamu mawazo ya Bwana ili apate kumfundisha?” Lakini sisi tunayo mawazo ya Kristo.
For who has penetrated the mind of the Lord, and will instruct Him? But we have the mind of Christ.

< 1 Wakorintho 2 >