< 1 Wakorintho 1 >

1 Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.
Paul, called to be an Apostle of Christ Jesus through the will of God--and our brother Sosthenes:
2 Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:
To the Church of God in Corinth, men and women consecrated in Christ Jesus, called to be saints, with all in every place who call on the name of our Lord Jesus Christ-- their Lord as well as ours.
3 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
May grace and peace be granted to you from God our Father and the Lord Jesus Christ.
4 Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.
I thank my God continually on your behalf for the grace of God bestowed on you in Christ Jesus--
5 Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,
that you have been so richly blessed in Him, with readiness of speech and fulness of knowledge.
6 kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.
Thus my testimony as to the Christ has been confirmed in your experience,
7 Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
so that there is no gift of God in which you consciously come short while patiently waiting for the reappearing of our Lord Jesus Christ,
8 Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
who will also keep you stedfast to the very End, so that you will be free from reproach on the day of our Lord Jesus Christ.
9 Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.
God is ever true to His promises, and it was by Him that you were, one and all, called into fellowship with his Son Jesus Christ, our Lord.
10 Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.
Now I entreat you, brethren, in the name of our Lord Jesus Christ, to cultivate a spirit of harmony--all of you--and that there be no divisions among you, but rather a perfect union through your having one mind and one judgement.
11 Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.
For I have been distinctly informed, my brethren, about you by Chloe's people, that there are dissensions among you.
12 Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”
What I mean is that each of you is a partisan. One man says "I belong to Paul;" another "I belong to Apollos;" a third "I belong to Peter;" a fourth "I belong to Christ."
13 Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Is the Christ in fragments? Is it Paul who was crucified on your behalf? Or were you baptized to be Paul's adherents?
14 Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.
I thank God that I did not baptize any of you except Crispus and Gaius--
15 Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.
for fear people should say that you were baptized to be my adherents.
16 (Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
I did, however, baptize Stephanas' household also: but I do not think that I baptized any one else.
17 Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.
Christ did not send me to baptize, but to proclaim the Good News; and not in merely wise words--lest the Cross of Christ should be deprived of its power.
18 Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
For the Message of the Cross is foolishness to those who are on the way to perdition, but it is the power of God to those whom He is saving.
19 Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”
For so it stands written, "I will exhibit the nothingness of the wisdom of the wise, and the intelligence of the intelligent I will bring to nought."
20 Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn g165)
Where is your wise man? Where your expounder of the Law? Where your investigator of the questions of this present age? Has not God shown the world's wisdom to be utter foolishness? (aiōn g165)
21 Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.
For after the world by its wisdom--as God in His wisdom had ordained--had failed to gain the knowledge of God, God was pleased, by the apparent foolishness of the Message which we preach, to save those who accepted it.
22 Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.
Seeing that Jews demand miracles, and Greeks go in search of wisdom,
23 Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.
while we proclaim a Christ who has been crucified--to the Jews a stumbling-block, to Gentiles foolishness,
24 Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.
but to those who have received the Call, whether Jews or Greeks, Christ the power of God and the wisdom of God.
25 Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.
Because that which the world deems foolish in God is wiser than men's wisdom, and that which it deems feeble in God is mightier than men's might.
26 Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo.
For consider, brethren, God's call to you. Not many who are wise with merely human wisdom, not many of position and influence, not many of noble birth have been called.
27 Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu.
But God has chosen the things which the world regards as foolish, in order to put its wise men to shame; and God has chosen the things which the world regards as destitute of influence, in order to put its powerful things to shame;
28 Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko,
and the things which the world regards as base, and those which it sets utterly at nought--things that have no existence--God has chosen in order to reduce to nothing things that do exist;
29 ili mtu yeyote asijisifu mbele zake.
to prevent any mortal man from boasting in the presence of God.
30 Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi.
But you--and it is all God's doing--are in Christ Jesus: He has become for us a wisdom which is from God, consisting of righteousness and sanctification and deliverance;
31 Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
in order that it may be as Scripture says, "He who boasts--let his boast be in the Lord."

< 1 Wakorintho 1 >