< Job 8 >

1 Y RESPONDIÓ Bildad Suhita, y dijo:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 ¿Hasta cuándo hablarás tales cosas, y las palabras de tu boca serán [como] un viento fuerte?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 ¿Acaso pervertirá Dios el derecho, ó el Todopoderoso pervertirá la justicia?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 Si tus hijos pecaron contra él, él los echó en el lugar de su pecado.
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 Si tú de mañana buscares á Dios, y rogares al Todopoderoso;
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 Si fueres limpio y derecho, cierto luego se despertará sobre ti, y hará próspera la morada de tu justicia.
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 Y tu principio habrá sido pequeño, y tu postrimería acrecerá en gran manera.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 Porque pregunta ahora á la edad pasada, y disponte para inquirir de sus padres de ellos;
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 Pues nosotros somos de ayer, y no sabemos, siendo nuestros días sobre la tierra como sombra.
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 ¿No te enseñarán ellos, te dirán, y de su corazón sacarán palabras?
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 ¿Crece el junco sin lodo? ¿crece el prado sin agua?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 Aun él en su verdor no será cortado, y antes de toda hierba se secará.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 Tales son los caminos de todos los que olvidan á Dios: y la esperanza del impío perecerá:
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 Porque su esperanza será cortada, y su confianza es casa de araña.
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 Apoyaráse él sobre su casa, mas no permanecerá en pie; atendráse á ella, mas no se afirmará.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 [A manera de un árbol], está verde delante del sol, y sus renuevos salen sobre su huerto;
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 Vanse entretejiendo sus raíces junto á [una] fuente, y enlazándose hasta un lugar pedregoso.
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 Si le arrancaren de su lugar, éste negarále entonces, [diciendo]: Nunca te vi.
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Ciertamente éste será el gozo de su camino; y de la tierra de donde se [traspusiere], nacerán otros.
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 He aquí, Dios no aborrece al perfecto, ni toma la mano de los malignos.
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 Aun henchirá tu boca de risa, y tus labios de júbilo.
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 Los que te aborrecen, serán vestidos de confusión; y la habitación de los impíos perecerá.
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.

< Job 8 >