< Job 36 >

1 Y AÑADIÓ Eliú, y dijo:
Elihu aliendelea na kusema,
2 Espérame un poco, y enseñarte he; porque todavía [tengo] razones en orden á Dios.
“Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 Tomaré mi noticia de lejos, y atribuiré justicia á mi Hacedor.
Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
4 Porque de cierto no son mentira mis palabras; contigo [está] el que es íntegro en [sus] conceptos.
Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
5 He aquí que Dios es grande, mas no desestima á nadie: es poderoso en fuerza de sabiduría.
Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
6 No otorgará vida al impío, y á los afligidos dará su derecho.
Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
7 No quitará sus ojos del justo; antes bien con los reyes los pondrá en solio para siempre, y serán ensalzados.
Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
8 Y si estuvieren prendidos en grillos, y aprisionados en las cuerdas de aflicción,
Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
9 El les dará á conocer la obra de ellos, y que prevalecieron sus rebeliones.
kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
10 Despierta además el oído de ellos para la corrección, y díce[les] que se conviertan de la iniquidad.
Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
11 Si oyeren, y [le] sirvieren, acabarán sus días en bien, y sus años en deleites.
Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
12 Mas si no oyeren, serán pasados á cuchillo, y perecerán sin sabiduría.
Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
13 Empero los hipócritas de corazón lo irritarán más, y no clamarán cuando él los atare.
Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
14 Fallecerá el alma de ellos en su mocedad, y su vida entre los sodomitas.
Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
15 Al pobre librará de su pobreza, y en la aflicción despertará su oído.
Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
16 Asimismo te apartaría de la boca de la angustia á lugar espacioso, [libre] de todo apuro; y te asentará mesa llena de grosura.
Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
17 Mas tú has llenado el juicio del impío, [en vez] de sustentar el juicio y la justicia.
Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
18 Por lo cual [teme] que [en su] ira no te quite con golpe, el cual no puedas apartar de ti con gran rescate.
Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
19 ¿Hará él estima de tus riquezas, ni del oro, ni de todas las fuerzas del poder?
Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
20 No anheles la noche, en que desaparecen los pueblos de su lugar.
Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
21 Guárdate, no tornes á la iniquidad; pues ésta escogiste más bien que la aflicción.
Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
22 He aquí que Dios es excelso con su potencia: ¿qué enseñador semejante á él?
Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 ¿Quién le ha prescrito su camino? ¿y quién [le] dirá: Iniquidad has hecho?
Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
24 Acuérdate de engrandecer su obra, la cual contemplan los hombres.
Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
25 Los hombres todos la ven; mírala el hombre de lejos.
Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
26 He aquí, Dios es grande, y nosotros no le conocemos; ni se puede rastrear el número de sus años.
Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
27 El reduce las gotas de las aguas, al derramarse la lluvia según el vapor;
Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
28 Las cuales destilan las nubes, goteando en abundancia sobre los hombres.
ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
29 ¿Quién podrá tampoco comprender la extensión de las nubes, y el sonido estrepitoso de su pabellón?
Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
30 He aquí que sobre él extiende su luz, y cobija [con ella] las raíces de la mar.
Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
31 Bien que por esos medios castiga á los pueblos, á la multitud da comida.
Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
32 Con las nubes encubre la luz, y mándale [no brillar], interponiendo [aquéllas].
Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
33 Tocante á ella anunciará [el trueno], su compañero, [que hay] acumulación de ira sobre el que se eleva.
Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.

< Job 36 >